Wakolosai 1
Neno: Bibilia Takatifu
1 Kutoka kwa Paulo, mtume wa Kristo Yesu na Timotheo ndugu yetu. 2 Kwa ndugu katika Kristo, watakatifu na waaminifu waishio Kolosai. Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu.
Shukrani Na Maombi
3 Siku zote tunamshukuru Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, tunapowaombea. 4 Kwa maana tumepata habari juu ya imani yenu katika Kristo Yesu na upendo wenu kwa watu wote wa Mungu. 5 Imani hii na upendo umetokana na tumaini mlilowekewa mbinguni na ambalo mmelisikia katika neno la kweli, yaani Habari Njema. 6 Duniani kote, hii Habari Njema iliyowajia inaenea na kuzaa mat unda kama ilivyokuwa kwenu mlipoisikia na kuelewa neema ya Mungu kwa kina.
7 Mlijifunza juu ya Habari Njema kutoka kwa mtumishi mwenzenu mpendwa, Epafra. Yeye ni mhudumu mwaminifu wa Kristo ambaye ana fanya kazi kwa niaba yetu, 8 naye ametufahamisha juu ya upendo wenu mliopewa na Roho.
9 Kwa sababu hii, tangu tuliposikia habari zenu, hatujaacha kuwaombea. Tunamsihi Mungu awape kwa wingi, maarifa ya kujua mapenzi yake, kwa njia ya hekima ya kiroho na ufahamu. 10 Ili mpate kuishi maisha yanayomtukuza Bwana na kumpendeza kabisa: mkizaa matunda kwa kila kazi njema na kukua katika kumjua Mungu. 11 Tunawaombea pia muimarishwe na nguvu zote kwa kadiri ya nguvu ya utukufu wake; mpate kuwa na subira na uvumilivu, huku 12 mkimshukuru kwa furaha Baba aliyewafanya mustahili kuwa na fungu katika urithi wa watakatifu, katika ufalme wa nuru. 13 Kwa maana ametuokoa kutoka katika nguvu za giza, akatuweka katika ufalme wa Mwanae mpendwa, 14 ambaye ametukomboa kwa damu yake, tukapata msamaha wa dhambi.
Ukuu Wa Kristo
15 Kristo anafanana kabisa na Mungu asiyeonekana. Yeye ali kuwepo kabla Mungu hajaumba kitu cho chote. 16 Yeye ndiye ali yeumba vitu vyote mbinguni na duniani; vitu vinavyoonekana na visivyoonekana; kama ni viti vya enzi au nguvu, au watawala au milki na mamlaka: vyote viliumbwa na yeye kwa ajili yake. 17 Yeye alikuwapo kabla ya vitu vingine vyote na kwa uwezo wake vitu vyote vinahusiana kwa mpango. 18 Yeye ni kichwa cha mwili, yaani kanisa lake; naye ni wa kwanza na mzaliwa wa kwanza wa wale wote wanaofufuka kutoka kwa wafu, ili yeye peke yake awe mkuu katika vitu vyote. 19 Kwa kuwa ilimpendeza Mungu kwamba ukamil ifu wake wote wa kimungu uwe ndani ya Mwanae; 20 na kwamba kwa njia ya mwanae vitu vyote vilivyoko duniani na vilivyoko mbinguni vipatanishwe na Mungu, kwa ajili ya damu yake iliyomwagwa msala bani kuleta amani.
21 Hapo kwanza ninyi mlikuwa mmefarakana na Mungu na mlikuwa maadui zake kwa sababu ya mawazo na matendo yenu maovu. 22 Lakini sasa Mungu amewapatanisha naye kwa njia ya mwili wa Kristo katika kifo, ili awaweke mbele yake mkiwa watakatifu, bila doa wala lawama. 23 Lakini hamna budi kuendelea kuwa imara na thabiti katika imani yenu, pasipo kuyumba katika tumaini lililomo katika Injili. Hii ndio ile Injili mliyoisikia na ambayo imetan gazwa kwa kila kiumbe duniani na ambayo mimi, Paulo, nimekuwa mtumishi wake.
Huduma Ya Paulo Kwa Makanisa
24 Na sasa nafurahi kuteseka kwa ajili yenu na kwa mateso yangu ninakamilisha kile ambacho kimepungua katika mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, yaani kanisa lake. 25 Mimi nime kuwa mtumishi wa kanisa kufuatana na wajibu niliopewa na Mungu, kuwasilisha kwenu neno la Mungu kwa ukamilifu. 26 Hii ni siri ambayo ilikuwa imefichika kwa karne nyingi na vizazi vingi viliv yopita, lakini sasa imefunuliwa kwa watu wa Mungu. 27 Kwao, Mungu amependa kudhihirisha kati ya mataifa utukufu wa utajiri wa siri hii, yaani, Kristo ndani yenu ndiye tumaini pekee la utu kufu.
28 Kwa sababu hii tunamtangaza Kristo, tukiwaonya na kuwa fundisha watu wote kwa hekima yote ili tuweze kumleta kila mmoja mbele ya Mungu akiwa amekamilika katika Kristo. 29 Kwa shabaha hii nina fanya kazi, nikijitahidi kwa nguvu kuu ya Kristo inay ofanya kazi kwa uwezo mkuu ndani yangu.
歌罗西书 1
Chinese Contemporary Bible (Simplified)
1 我是奉上帝旨意做基督耶稣使徒的保罗, 2 和提摩太弟兄写信给歌罗西的圣徒,就是忠于基督的弟兄姊妹。
愿我们的父上帝赐给你们恩典和平安!
感恩与祷告
3-4 我们听说了你们对基督耶稣的信心和对众圣徒的爱心,为你们祷告的时候,常常感谢我们主耶稣基督的父上帝。 5 你们能有这样的信心和爱心是因为那给你们存在天上的盼望,就是你们从前从福音真道中听到的盼望。 6 这福音不但传到了你们那里,也传到了世界各地,并且开花结果,信主的人数不断增长,正如你们当初听了福音,因为明白真理而认识上帝的恩典后的情形。 7 这福音是你们从我们亲爱的同工以巴弗那里得知的。他代表我们[a]做基督的忠仆, 8 并把圣灵赐给你们的爱心告诉了我们。
9 因此,从听到你们的消息那天起,我们便不断地为你们祷告,求上帝使你们在一切属灵的智慧和悟性上完全明白祂的旨意, 10 以便你们行事为人对得起主,凡事蒙祂喜悦,在一切良善的事上结出果实,对上帝的认识不断增加。 11 愿上帝以祂荣耀的权能使你们刚强,无论遇到什么事都能长久忍耐, 12 欢喜地感谢天父,因祂使你们有资格跟众圣徒在光明中同享基业。 13 祂把我们从黑暗的权势下拯救出来,带进祂爱子的国度里。 14 我们借着祂的爱子蒙救赎,罪过得到赦免。
基督超越一切
15 基督是那不能看见之上帝的真像,超越[b]一切受造之物。 16 因为万物都是借着祂创造的,天上的、地上的、有形的、无形的、做王的、统治的、执政的、掌权的,一切都是借着祂也是为了祂而创造的。 17 祂存在于万物之前,万物都靠祂而维系。 18 祂是教会的头,教会是祂的身体;祂是源头,是首先从死里复活的,这样祂可以在一切事上居首位。 19 因为上帝乐意让一切的丰盛住在祂里面, 20 又借着祂在十字架上所流的血成就了和平,使天地万物借着祂与上帝和好。
21 你们从前与上帝隔绝,行事邪恶,心思意念与祂为敌; 22 但现在上帝借着基督肉身的死使你们与祂和好了,让你们在祂面前成为圣洁无瑕、无可指责的人。 23 只是你们必须恒心持守所信的道,根基稳固,坚定不移,不要失去你们听到福音后所得到的盼望。这福音传给了天下万民。我保罗也做了这福音的使者。
保罗为教会受苦
24 现在我因能够为你们受苦而欢喜,并且我是为基督的身体——教会的缘故,在自己身上补满基督未受的苦难。 25 我受上帝的委派成为教会的仆人,要把上帝的道完整地传给你们。 26 这道是历世历代一直隐藏的奥秘,现在已经向祂的众圣徒显明了。 27 上帝要他们知道这奥秘在外族人中有何等丰富的荣耀,这奥秘就是基督在你们里面,使你们有荣耀的盼望。 28 我们传扬基督,用各样的智慧劝诫、教导众人,使他们在基督里长大成熟,好把他们带到上帝面前。 29 为此,我按着祂在我身上运行的大能尽心竭力,不辞劳苦。
Wakolosai 1
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
1 Salamu kutoka kwa Paulo, mtume wa Kristo Yesu.[a] Mimi ni mtume kwa sababu ndivyo Mungu alivyotaka niwe. Salamu pia kutoka kwa Timotheo ndugu yetu katika Kristo.
2 Salamu kwenu kaka na dada zetu watakatifu na walio waaminifu katika Kristo mlioko Kolosai.
Neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu ziwe pamoja nanyi.
3 Katika maombi yetu tunamshukuru Mungu daima kwa ajili yenu. Yeye ndiye Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo. 4 Nasi tunamshukuru Yeye kwa sababu tumesikia kuhusu imani yenu katika Kristo Yesu na upendo wenu kwa watu wa Mungu wote. 5 Imani yenu na upendo wenu vinatokana na ufahamu kwamba mtapokea kile mnachotumaini. Hicho ambacho Mungu amekihifadhi salama mbinguni kwa ajili yenu. Hilo ni tumaini lile lile ambalo mmekuwa nalo tangu mliposikia kwa mara ya kwanza ujumbe wa kweli, yaani Habari Njema. 6 Habari Njema hii imezaa matunda na imeenea ulimwenguni kote. Na hicho ndicho kilichokuwa kikitokea tangu siku mliposikia kwa mara ya kwanza na kuelewa ukweli wa neema ya Mungu. 7 Kweli hiyo mliisikia kutoka kwa Epafra, aliye mtumwa wa Bwana pamoja nasi. Yeye anatusaidia sisi[b] kama mtumishi mwaminifu wa Kristo. 8 Naye ametueleza pia kuhusu upendo mlioupokea kutoka kwa Roho Mtakatifu.
9 Ndugu zangu tangu siku tuliposikia mambo haya juu yenu, tumeendelea kuwaombea, na haya ndiyo maombi yetu kwa ajili yenu:
Kwamba Mungu awajaze ufahamu wa mapenzi yake kwa kuwapa hekima na ufahamu wote wa kiroho mnaohitaji; 10 ili hayo yawasaidie kuishi maisha yanayomletea Bwana heshima na kumpendeza yeye katika hali zote; ili maisha yenu yazae matunda mema ya aina mbalimbali na mpate kuongezeka katika maarifa yenu ya Mungu;[c] 11 ili Mungu mwenyewe awaimarishe kwa uwezo wake mkuu, ili muwe na uvumilivu pasipo kukata tamaa mnapokutana na shida.
Ndipo nanyi mtakapofurahi, 12 na kumshukuru Mungu Baba. Kwani yeye amewastahilisha kupokea kile alichowaahidi watakatifu wake, wanaoishi katika nuru. 13 Mungu ametuweka huru kutoka katika nguvu za giza. Naye ametuingiza katika ufalme wa Mwanaye mpendwa. 14 Na huyo Mwana amelipa gharama ya kutuweka huru, kwani ndani yake tuna msamaha wa dhambi zetu.
Mwana wa Mungu yu sawa na Mungu
15 Hakuna anayeweza kumwona Mungu,
lakini Mwana anafanana kabisa na Mungu.
Anatawala juu ya kila kitu kilichoumbwa.
16 Kwa uweza wake, vitu vyote viliumbwa:
vitu vya angani na ardhini, vinavyoonekana na visivyoonekana,
watawala wote wa kiroho, wakuu, enzi, na mamlaka.
Kila kitu kiliumbwa kupitia Yeye na kwa ajili yake.
17 Mwana alikuwapo kabla ya kuumbwa kitu chochote,
na vyote vinaendelea kuwepo kwa sababu yake.
18 Yeye ni kichwa cha mwili,
yaani kanisa.
Yeye ni mwanzo wa maisha yajayo,
ni wa kwanza miongoni mwa wote watakaofufuliwa kutoka kwa wafu.[d]
Hivyo katika mambo yote yeye ni mkuu zaidi.
19 Mungu alipendezwa kwamba ukamilifu wa uungu wake
uishi ndani ya Mwana.
20 Na kupitia Yeye, Mungu alifurahi
kuvipatanisha tena vitu vyote kwake Yeye mwenyewe;
vilivyoko mbinguni na vilivyoko duniani.
Mungu alileta amani kupitia sadaka ya damu ya Mwanaye msalabani.
21 Hapo mwanzo mlitengwa na Mungu, na mlikuwa adui zake katika fikra zenu, kwa sababu ya maovu mliyotenda kinyume naye. 22 Lakini sasa amewafanya kuwa marafiki zake tena, kupitia kifo cha Kristo katika mwili wake. Ili kwa njia hiyo awalete kwake mkiwa watakatifu, msio na lawama na msiohukumiwa jambo lolote mbele zake; 23 na hiki ndicho kitatokea mkiendelea kuiamini Habari Njema mliyoisikia. Mwendelee kuwa imara na kudumu katika imani. Jambo lolote lisiwafanye mkaliacha tumaini lenu mlilopokea mlipoisikia Habari Njema. Habari Njema ile ile ambayo imehubiriwa kwa kila mtu duniani, ndiyo kazi ambayo mimi, Paulo, nilipewa kufanya.
Kazi ya Paulo kwa Ajili ya Kanisa
24 Nina furaha kwa sababu ya mateso ninayopata kwa manufaa yenu. Yapo mambo mengi ambayo kupitia hayo Kristo bado anateseka. Nami ninayapokea mateso haya kwa furaha katika mwili wangu kwa ajili ya mwili wake, yaani Kanisa. 25 Nilifanyika kuwa mtumishi wa kanisa kwa sababu Mungu alinipa kazi maalum ya kufanya. Kazi hii inawasaidia ninyi, nayo ni kuuhubiri ujumbe kamili wa Mungu. 26 Ujumbe huu ni ukweli wenye siri uliofichwa tangu mwanzo wa nyakati. Nao ulifichwa kutoka kwa kila mtu kwa muda mrefu, lakini sasa umedhihirishwa kwa watakatifu wa Mungu. 27 Mungu aliamua kuwajulisha watu wake namna Kweli hii ilivyo na utajiri na utukufu. Siri hii ya kweli hii, ambayo ni kwa ajili ya watu wote, ni kwamba Kristo anaishi ndani yenu. Yeye ndiye tumaini la kushiriki katika utukufu wake. 28 Hivyo tunaendelea kuwaambia watu juu ya Kristo. Tunatumia hekima yote kumshauri na kumfundisha kila mtu. Tunajaribu kumleta kila mtu mbele za Mungu kama watu waliokomaa kiroho katika uhusiano wao na Kristo. 29 Kwa kufanya hivi, ninafanya kazi kwa bidii, nikijitahidi na kutumia nguvu kubwa aliyonipa Kristo. Nguvu hiyo inafanya kazi katika maisha yangu.
Footnotes
- 1:1 Kristo Yesu Au “Mfalme Yesu”. Neno “Kristo” ni tafsiri ya Kiyunani ya neno la Kiebrania “Masihi”, ambao ni wadhifa wa kifalme. Tazama Mk 15:32: Lk 23:2. Tazama pia Kristo na Masihi katika Orodha ya Maneno.
- 1:7 anatusaidia sisi Nakala nyingi za kale za Kiyunani zina neno hili “anakusaidia wewe”.
- 1:10 ili maisha … ya Mungu Au “kwamba maarifa yenu ya Mungu yatazaa matunda zaidi na zaidi pamoja na matunda mema ya kila namna katika maisha yenu.”
- 1:18 wa kwanza miongoni … kwa wafu Ina maana ya wa kwanza kutoka kwa wafu.
Copyright © 1989 by Biblica
Chinese Contemporary Bible Copyright © 1979, 2005, 2007, 2011 by Biblica® Used by permission. All rights reserved worldwide.
© 2017 Bible League International