2 Wathesalonike 2
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Mambo Maovu Yatatokea
2 Kaka na dada, tuna jambo la kuwaambia juu ya kuja kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Tunataka kuzungumza nanyi juu ya wakati huo tutakapokusanyika pamoja naye. 2 Msikubali kufadhaishwa na kutiwa kuhofu ikiwa mtasikia kwamba siku ya Bwana tayari imekwishawadia. Wengine wanaweza kusema kwamba wazo hili limetoka kwetu katika jambo alilotuambia Roho, au tulilosema, au katika barua tuliyoiandika. 3 Msidanganywe na chochote wanachoweza kusema kuhusu kuja kwa Bwana. Siku hiyo ya Bwana haitakuja mpaka itanguliwe na kukengeuka kwa wanadamu na kumwacha Mungu. Na siku hiyo haitakuja mpaka ajitokeze kwanza Mtu wa Uovu, yule ambaye ana uhakika kuwa ataangamizwa.[a] 4 Huyo atasimama kinyume na kujiweka mwenyewe juu ya kila kitu ambacho watu wanaabudu au kudhani kuwa kinafaa kuabudiwa. Ataenda na kuingia ndani ya Hekalu[b] na kukikalia kiti cha enzi, akidai kuwa yeye ni Mungu.
5 Niliwaambia zaidi ya mara moja nilipokuwa huko kwamba mambo yote haya yangetokea. Je, mnakumbuka? 6 Na mnafahamu kinachomzuia Mtu wa Uovu. Huyo hataruhusiwa kuonekana mpaka wakati sahihi utakapofika. 7 Tayari nguvu ya uovu inatenda kazi ulimwenguni sasa. Lakini yupo mmoja anayeizuia nguvu hiyo. Na ataendelea kuizuia mpaka atakapoondolewa. 8 Kisha huyo Mtu wa Uovu atatokea. Lakini Bwana Yesu atamuua kwa pumzi inayotoka katika kinywa chake. Bwana atakuja katika namna ambayo kila mtu atamwona, na huo utakuwa mwisho wa Mtu wa Uovu.
9 Kuja kwa Mtu wa Uovu itakuwa kazi ya Shetani. Atakuja na nguvu kuu, na atafanya aina zote za miujiza ya uongo, ishara, na maajabu. 10 Mtu wa Uovu atatumia kila aina ya uovu kuwatia ujinga wote walio njiani kuelekea kuangamia. Wamepotea kwa sababu walikataa kuupenda ujumbe wenye ukweli kuhusu Yesu na kuokolewa. 11 Hivyo Mungu atawaacha wadanganyike hata kuamini uongo.[c] 12 Wote watahukumiwa kwa sababu hawakuamini ujumbe wa kweli na kwa kuwa walifurahia kufanya maovu.
Mmechaguliwa kwa ajili ya Wokovu
13 Ndugu zangu, ninyi ni watu mnaopendwa na Bwana. Na imetupasa tumshukuru Mungu daima kwa sababu yenu. Hayo ndiyo tunayotakiwa kuyatenda, kwa sababu Mungu aliwaita kuwa miongoni mwa watu[d] wa kwanza kuokolewa. Mmeokolewa na Roho aliyewafanya muwe watu wa Mungu walio watakatifu kupitia kuiamini kweli. 14 Mungu aliwaita ninyi mpate wokovu. Aliwaita kwa kutumia Habari Njema tuliwahubiri. Mliitwa ili mshiriki katika utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo. 15 Hivyo simameni imara na kuendelea kuamini mafundisho tuliyowapa tulipokuwa huko na kupitia barua yetu.
16-17 Tunaomba kwamba Bwana Yesu Kristo na Mungu Baba yetu awafariji na kuwaimairisha katika kila jambo jema mnalotenda na kusema. Mungu alitupenda na kutupa kupitia neema matumaini ya ajabu na faraja isiyo na mwisho.
Footnotes
- 2:3 ataangamizwa Au “Kusababisha uharibifu”. Kwa maana ya kawaida, “ni mwana wa uharibifu”.
- 2:4 Hekalu Pengine Hekalu katika Yerusalemu. Tazama Hekalu katika Orodha ya Maneno.
- 2:11 uongo Ina maana ya kuamini uongo (mkubwa) juu ya Muasi (ya kwamba Muasi ndiye Mungu).
- 2:13 kuwa … watu Nakala zingine za Kiyunani zimeongeza, “kuanzia mwanzo”.
帖 撒 羅 尼 迦 後 書 2
Chinese New Testament: Easy-to-Read Version
邪恶的事情将会出现
2 兄弟们,关于我们的主耶稣基督再次降临以及我们与他相聚的事情,我们现在请求你们, 2 如果你们听说主的日子已经来临了,不要感到困惑,也不要害怕。也许有人会说这说法是在某个预言或信息之中,或者是你们从某人声称是从我们写的信中读到了它。 3 不要让任何人用任何方式欺骗你们,因为主来临的日子要等到大叛乱发生后,以及那个注定要毁灭的不法之徒出现之后。 4 那不法之徒将反对任何称为上帝的或任何崇拜对象,并置自己于这一切之上。他甚至还会来到上帝的大殿,坐在宝座上,宣称自己就是上帝。
5 你们难道不记得我和你们在一起时,总是告诉你们这些事情吗? 6 因此,你们现在知道是什么阻止了他的出现,以便他能够在适当的时刻出现。 7 我这么说,是因为现在这个不法之徒的秘密力量已经开始工作了,然而,阻止这秘密力量的他会继续这么做,直到他被移开为止。 8 然后不法之徒将会出现。主耶稣用一口气就会将他杀死,并在主再次降临时把他毁灭。 9 这个不法之徒将借着撒旦的力量,伴着巨大的力量、虚假的迹象和奇迹出现, 10 并用各种不义的方式欺骗那些即将毁灭的人,因为他们不爱使他们得到拯救的真理。 11 为此,上帝派引导他们偏离真理的力量来到他们中间,使他们去相信虚妄的, 12 并使所有不相信真理和沉缅于邪恶的人被定罪。
你们被选为拯救的对象
13 主所爱的兄弟们,我们必须时常为你们感谢上帝。因为从一开始上帝就选择了你们,让你们借圣灵的神圣而得到拯救。 14 为了这拯救,上帝通过我们向你们传播的福音来召唤你们,好让你们获得属于我们主耶稣基督的荣耀。 15 因此,兄弟们,要站稳,要坚持我们传给你们的教导,不论是口头上的,还是书面上的。
© 2017 Bible League International
Copyright © 2004 by World Bible Translation Center