彼得的解釋

11 使徒和猶太全境的弟兄姊妹都聽說外族人接受了上帝的道。 彼得一回到耶路撒冷,嚴守割禮的門徒就指責他: 「你竟然去未受割禮之人的家,還和他們一同吃飯!」

彼得就把事情的經過一一向他們解釋,說: 「我在約帕城禱告的時候,看見一個異象,有一大塊像布的東西四個角吊著從天上降到我面前。 我定睛一看,裡面有牲畜、野獸、爬蟲和飛禽。 接著,我聽見有聲音對我說,『彼得,起來,宰了吃!』 我說,『主啊,這可不行!我從未吃過任何污穢不潔之物!』 那從天上來的聲音又說,『上帝已經潔淨的,你不可再稱之為不潔淨。』 10 這樣一連三次,然後一切都被收回天上去了。 11 就在那時候,有三個從凱撒利亞來的人到我住處的門口來找我。 12 聖靈吩咐我跟他們同去,不要猶豫。就這樣,我和這六位弟兄一同到了哥尼流家。 13 他告訴我們天使如何在他家中向他顯現,並對他說,『你派人去約帕,請一位名叫西門·彼得的人來。 14 他有話告訴你,能使你和你的全家得救。』

15 「我開口講話時,聖靈降在他們身上,跟當初降在我們身上的情形一模一樣。 16 我就想起主的話,『約翰用水施洗,但你們要受聖靈的洗禮。』 17 既然上帝給他們恩賜,就如我們信主耶穌基督時給我們一樣,我是誰,怎能攔阻上帝?」 18 大家聽了便安靜下來,轉而歸榮耀給上帝,說:「如此看來,上帝把悔改得永生的機會也賜給了外族人。」

安提阿的教會

19 司提凡殉道後,信徒們因受迫害而四散到各處,遠至腓尼基、塞浦路斯和安提阿,他們只向那裡的猶太人傳福音。 20 不過,有些塞浦路斯和古利奈的信徒到了安提阿之後,也向希臘人傳講主耶穌的福音。 21 上帝的能力伴隨著他們,有許多人信了主。

22 耶路撒冷教會的人聽到這消息後,就派巴拿巴去安提阿。 23 他到達後,看見上帝所賜的恩典,就萬分高興,勸勉他們要全心地忠於主。

24 巴拿巴是個被聖靈充滿、信心堅定的好人。那時信主的人大大增加。 25 他又到大數去找掃羅, 26 找到後,便帶他回安提阿。他們在教會待了一年之久,教導了許多人。門徒被稱為「基督徒」就是從安提阿開始的。

27 當時,有幾位先知從耶路撒冷下到安提阿。 28 其中一位名叫亞迦布,他得到聖靈的啟示,站起來預言天下將有嚴重的饑荒。後來,這事果然在克勞狄執政期間發生了。 29 門徒決定各盡所能,捐款救濟住在猶太境內的弟兄姊妹。 30 他們捐完後,委託巴拿巴和掃羅將款項送交耶路撒冷教會的長老。

Petro Arudi Yerusalemu

11 Mitume na waamini katika Uyahudi walisikia kwamba watu wasio Wayahudi wameyapokea mafundisho ya Mungu pia. Lakini Petro alipokuja Yerusalemu, baadhi ya waamini wa Kiyahudi[a] walimkosoa. Walisema, “Uliingia katika nyumba za watu wasio Wayahudi ambao hawajatahiriwa na ukala pamoja nao!”

Hivyo Petro akawaelezea namna ilivyotokea. Akasema, “Nilikuwa katika mji wa Yafa. Nilipokuwa nikiomba, niliona maono. Niliona kitu kikishuka chini kutoka mbinguni. Kilionekana kama shuka kubwa ikishushwa chini kwa pembe zake nne. Kikaja chini karibu yangu. Nilipotazama ndani yake, niliona aina zote za wanyama, pamoja na wale wa porini, wanyama wanaotambaa na ndege. Nilisikia sauti ikiniambia. Chinja chochote hapa na ule!”

“Lakini nilisema, ‘Siwezi kufanya hivyo Bwana! Sijawahi kula kitu cho chote kisicho safi au kisichostahili kuliwa kama chakula.’

Lakini sauti kutoka mbinguni ikajibu tena, ‘Mungu amevitakasa vitu hivi. Usiseme havistahili kuliwa!’

10 Hili lilitokea mara tatu. Ndipo kitu chote kikachukuliwa kurudi mbinguni. 11 Saa hiyo hiyo baada ya hayo wakawepo watu watatu wamesimama nje ya nyumba nilimokuwa ninakaa. Walikuwa wametumwa kutoka Kaisaria kunichukua. 12 Roho Mtakatifu aliniambia niende nao bila kuwa na mashaka. Ndugu hawa hapa sita walikwenda pamoja nami, na tulikwenda katika nyumba ya Kornelio. 13 Alitwambia kuhusu malaika aliyemwona amesimama katika nyumba yake. Malaika alimwambia, ‘Tuma baadhi ya watu waenda Yafa kumchukua Simoni, ambaye pia anaitwa Petro. 14 Atazungumza na wewe. Ujumbe atakaokwambia utakuokoa wewe na kila mtu anayeishi katika nyumba yako.’

15 Nilipoanza kuzungumza, Roho Mtakatifu alikuja juu yao kama vile alivyokuja juu yetu mwanzo.[b] 16 Ndipo nilikumbuka maneno ya Bwana Yesu, aliyosema: ‘Yohana alibatiza katika maji, lakini ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu.’ 17 Mungu amewapa watu hawa karama ile ile aliyotupa sisi tuliomwamini Bwana Yesu Kristo. Hivyo ningewezaje kupinga yale ambayo Mungu alitaka kufanya?”

18 Waamini wa Kiyahudi waliposikia hili, wakaacha kubisha. Wakamsifu Mungu na kusema, “Kwa hiyo Mungu anawaruhusu watu wasio Wayahudi kubadili mioyo yao na kuwa na maisha anayotoa!”

Habari Njema Zafika Antiokia

19 Waamini walitawanyika kwa sababu ya mateso[c] yaliyoanza baada ya Stefano kuuawa. Baadhi ya waamini walikwenda mbali mpaka Foeniki, Kipro na Antiokia. Walihubiri Habari Njema katika maeneo haya, lakini kwa Wayahudi tu. 20 Baadhi ya waamini hawa walikuwa watu kutoka Kipro na Kirene. Watu hawa walipofika Antiokia, walianza kuwahubiri watu wasio Wayahudi.[d] Waliwahubiri Habari Njema kuhusu Bwana Yesu. 21 Nguvu ya Bwana iliambatana na watu hawa, na idadi kubwa ya watu waliamini na kuamua kumfuata Bwana.

22 Kanisa katika mji wa Yerusalemu liliposikia kuhusu hili, lilimtuma Barnaba kwenda Antiokia. 23-24 Barnaba alikuwa mtu mwema, aliyejaa Roho Mtakatifu na imani. Alipokwenda Antiokia na kuona jinsi Mungu alivyowabariki waamini pale, alifurahi sana. Akawatia moyo wote, akasema, “Iweni waaminifu kwa Bwana daima. Mtumikieni Yeye kwa mioyo yenu yote.” Watu wengi zaidi wakawa wafuasi wa Bwana.

25 Kisha Barnaba alikwenda katika mji wa Tarso kumtafuta Sauli. 26 Alipompata, alimpeleka Antiokia. Walikaa pale mwaka mzima. Kila wakati kanisa lilipokusanyika, Barnaba na Sauli walikutana nao na kuwafundisha watu wengi. Ni katika mji wa Antiokia ambako wafuasi wa Bwana Yesu walianza kuitwa “Wafuasi wa Kristo”.[e]

27 Katika wakati huo huo baadhi ya manabii walitoka Yerusalemu na kwenda Antiokia. 28 Mmoja wao, aliyeitwa Agabo, huku akisaidiwa na Roho Mtakatifu, alisimama na kuzungumza. Alisema, “Wakati mbaya sana unakuja katika dunia yote. Hakutakuwa chakula kwa ajili ya watu kula.” (Kipindi hiki cha njaa kilitokea Klaudio alipokuwa mtawala wa Kirumi) 29 Wafuasi wa Bwana wakaamua kwamba kila mmoja wao atatuma kiasi anachoweza kuwasaidia ndugu wote[f] wanaoishi Uyahudi. 30 Walikusanya pesa na kuwapa Barnaba na Sauli, waliozipeleka kwa wazee, katika Uyahudi.

Footnotes

  1. 11:2 waamini wa Kiyahudi Kwa maana ya kawaida, “watu wa tohara”. Hii inaweza kuwa na maana ya Wayahudi waliodhani kuwa wafuasi wote wa Kristo ni lazima watahiriwe na kutii Sheria ya Musa. Tazama Gal 2:12.
  2. 11:15 mwanzo Siku ya Pentekoste katika Matendo 2, Roho Mtakatifu alipowashukia wafuasi wa mwanzo wa Yesu na kuwapa nguvu ya kuanza kuuhubiri ulimwengu Habari Njema za wokovu kupitia Yesu.
  3. 11:19 mateso Au “kipindi cha mateso”. Hiki ni kipindi ambacho viongozi wa Kiyahudi katika mji wa Yerusalemu walikuwa wakiwaadhibu watu wanaomwamini Kristo. Tazama Mdo 8:1-4.
  4. 11:20 watu wasio Wayahudi Kwa maana ya kawaida, “Wa mataifa” au “Wahelenisti”, au watu waliochangamana na kuathiriwa na utamaduni wa Kiyunani (Kigiriki). Nakala zingine za Kiyunani zina “Wayunani” au “Wagiriki”.
  5. 11:26 Wafuasi wa Kristo Yaani, Wakristo.
  6. 11:29 ndugu wote Yaani, Jamaa yote ya Waamini.