Matendo 28
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Paulo Katika Kisiwa cha Malta
28 Tulipokuwa salama nchi kavu, tukatambua kuwa kisiwa kile kinaitwa Malta. 2 Watu walioishi pale walikuwa wema sana kwetu. Mvua ilikuwa inanyesha na kulikuwa baridi sana, hivyo walitengeneza moto na kutukaribisha sote. 3 Paulo alikusanya kuni nyingi kwa ajili ya moto. Alipokuwa akiweka kuni kwenye moto, nyoka mwenye sumu kali akajitokeza kwa sababu ya joto na kumuuma kwenye mkono. 4 Wenyeji wa kisiwa kile walipomwona nyoka ananing'inia kwenye mkono wa Paulo, walisema, “Mtu huyu lazima ni mwuaji! Hakufa baharini, lakini Haki[a] hataki aishi.”
5 Lakini Paulo alimku'ngutia nyoka kwenye moto na hakudhurika. 6 Watu wakadhani atavimba au ataanguka na kufa. Walisubiri na kumwangalia kwa muda mrefu, lakini hakuna kibaya kilichomtokea. Hivyo wakabadili mawazo yao. Wakasema, “Paulo ni mungu!”
7 Yalikuwepo mashamba kuzunguka eneo lile. Yaliyomilikiwa na ofisa wa juu sana wa Rumi katika kisiwa hicho aliyeitwa Pablio. Alitukaribisha nyumbani kwake na alikuwa mwema sana kwetu. Tulikaa nyumbani kwake kwa siku tatu. 8 Baba yake Pablio alikuwa mgonjwa sana. Alikuwa na homa na alikuwa anaharisha damu, lakini Paulo alikwenda kwake na kumuombea. Aliweka mikono juu yake naye akapona. 9 Baada ya hili kutokea, wagonjwa wengine wote kisiwani walikuja kwa Paulo, naye aliwaombea na wakaponywa pia.
10-11 Watu katika kisiwa hiki walituheshimu sana. Na baada ya kuwa pale kwa miezi mitatu, tukawa tayari kuondoka, walitupa kila kitu tulichohitaji kwa ajili ya safari yetu.
Paulo Aenda Rumi
Tulipanda meli iliyotoka Iskanderia iliyokaa katika kisiwa cha Malta wakati majira ya baridi. Mbele ya meli kulikuwa alama ya miungu pacha.[b] 12 Tulisimama katika mji wa Sirakuse. Tulikaa pale kwa siku tatu kisha tukaondoka. 13 Tulifika katika mji wa Regio. Siku iliyofuata upepo ulianza kuvuma kutokea Kusini-Magharibi, hivyo tuliweza kuondoka. Baada ya siku moja tukafika katika mji wa Puteoli. 14 Tuliwapata baadhi ya waamini pale, walituomba tukae nao kwa wiki moja. Mwishowe tulifika Rumi. 15 Ndugu na dada waliokaa Rumi walisikia habari zetu, walikuja kutupokea kwenye Soko la Apio[c] na kwenye Migahawa Mitatu.[d] Paulo alipowaona waamini hawa, alimshukuru Mungu na alifarijika.
Paulo Akiwa Rumi
16 Tulipofika Rumi, Paulo aliruhisiwa kuishi peke yake. Lakini askari alikaa pamoja naye kumlinda.
17 Siku tatu baadaye Paulo aliagiza baadhi ya Wayahudi muhimu waje kwake. Walipokusanyika, akasema, “Ndugu zangu, sijafanya lolote kinyume na watu wetu au kinyume na desturi za baba zetu. Lakini nilikamatwa Yerusalemu na kukabidhiwa kwa Warumi. 18 Waliniuliza maswali mengi, lakini hawakupata sababu yoyote kwa nini niuawe. Hivyo walitaka kuniachia huru. 19 Lakini Wayahudi kule hawakutaka hilo. Hivyo ilinibidi niombe kuja Rumi kuweka mashitaka yangu mbele ya Kaisari. Kwa kufanya hivi haimaanishi kuwa ninawashutumu watu wangu kwa kufanya chochote kibaya. 20 Ndiyo sababu nilitaka kuonana na kuzungumza nanyi. Nimefungwa kwa minyororo hii kwa sababu ninaamini katika tumaini la Israeli.”
21 Wayahudi walimjibu Paulo, “Hakuna barua tuliyoipokea kutoka Uyahudi kuhusu wewe. Hakuna ndugu yetu yeyote Myahudi aliyesafiri kutoka huko aliyeleta habari zako au kutwambia chochote kibaya juu yako. 22 Tunataka kusikia mawazo yako. Tunafahamu kuwa watu kila mahali wanapinga kundi hili jipya.”
23 Paulo na Wayahudi walichagua siku kwa ajili ya mkutano. Siku hiyo Wayahudi wengi walikutana na Paulo katika nyumba yake. Aliwaambia kwa siku nzima, akawafafanulia kuhusu ufalme wa Mungu. Alitumia Sheria ya Musa na maandishi ya manabii kuwashawishi kumwamini Yesu. 24 Baadhi ya Wayahudi waliamini alichosema, lakini wengine hawakuamini. 25 Walibishana wao wenyewe na wakaanza kuondoka. Lakini aliwaambia kitu kimoja zaidi: “Roho Mtakatifu aliwaambia ukweli baba zenu kupitia nabii Isaya, aliposema,
26 ‘Nenda kwa watu hawa na uwaambie:
Mtasikiliza na kusikiliza,
lakini hamtaelewa.
Mtatazama na kutazama,
lakini hakika hamtaona.
27 Watu hawa hawawezi kuelewa.
Masikio yao yamezibwa.
Na macho yao yamefumbwa.
Hivyo hawawezi kuona kwa macho yao,
au kusikia kwa masikio yao;
au kuelewa kwa akili zao;
au kuelewa kwa akili zao.
Ikiwa wangeelewa, wangeweza kunirudia,
na ningewaponya.’(A)
28 Ninataka ninyi Wayahudi mjue kuwa Mungu ameupeleka wokovu wake kwa watu wasio Wayahudi. Watasikia!” 29 [e]
30 Paulo alikaa katika nyumba yake mwenyewe aliyopanga kwa miaka miwili kamili. Aliwakaribisha watu wote waliokuja kumtembelea. 31 Aliwaambia kuhusu ufalme wa Mungu na kuwafundisha kuhusu Bwana Yesu Kristo. Alikuwa na ujasiri sana, na hakuna aliyejaribu kumzuia asizungumze.
Footnotes
- 28:4 Haki Wenyeji wa kisiwa kile waliamini kuwa kuna mungu mke aliyeitwa Haki ambaye angewaadhibu waovu.
- 28:10-11 miungu pacha Sanamu ya Kasto na Polu, miungu wa Kiyunani.
- 28:15 Soko la Apio Mji ulio kama maili 43 (kilomita 69) kutoka mji wa Rumi.
- 28:15 Migahawa Mitatu Mji ulio kama maili 30 (kilomita 48) kutoka mji wa Rumi.
- 28:29 Nakala zingine za baadaye za Matendo zimeongeza mstari wa 29: “Baada ya Paulo kusema hivi, Wayahudi walianza kuondoka, wakiwa bado wanabishana wao kwa wao.”
Acts 28
Jubilee Bible 2000
28 ¶ And when they were escaped, then we knew that the island was called Melita. {or Malta}
2 And the barbarous people showed us no little kindness; for they kindled a great fire and received all of us because of the present rain and because of the cold.
3 And when Paul had gathered a bundle of sticks and laid them on the fire, a viper came out of the heat and fastened on his hand.
4 And when the barbarians saw the venomous beast hang on his hand, they said among themselves, No doubt this man is a murderer, whom, though he has escaped the sea, yet vengeance does not suffer him to live.
5 And he shook off the beast into the fire and felt no harm.
6 But they were waiting to see when he should have swollen or fallen down dead suddenly; but after they had waited a great while and saw no harm come to him, they changed their minds and said that he was a god.
7 In the same quarters were possessions of a principal man of the island, whose name was Publius, who received us and lodged us three days courteously.
8 And it came to pass that the father of Publius lay sick of a fever and of dysentery, to whom Paul entered in and prayed and laid his hands on him and healed him.
9 So when this was done, others also, who had diseases in the island, came and were healed,
10 who also honoured us with many gifts; and when we departed, they laded us with such things as were necessary.
11 ¶ And after three months we departed in a ship of Alexandria, which had wintered in the isle, whose ensign was Castor and Pollux.
12 And landing at Syracuse, we tarried there three days.
13 And having gone around, we came to Rhegium, and after one day the south wind blew, and we came the next day to Puteoli,
14 where we found brethren, who asked us to tarry with them seven days, and so we went toward Rome.
15 And from there, when the brethren heard of us, they came to meet us as far as Appii Forum and The Three Taverns whom when Paul saw, he thanked God and took courage.
16 And when we came to Rome, the centurion delivered the prisoners to the praetorian prefect, but Paul was allowed to dwell by himself with a soldier that kept him.
17 ¶ And it came to pass, that after three days Paul called the principals of the Jews together, and when they were come together, he said unto them, Men and brethren, though I have committed nothing against the people or customs of our fathers, yet was I delivered prisoner from Jerusalem into the hands of the Romans,
18 who, when they had examined me, would have let me go because there was no cause of death in me.
19 But when the Jews spoke against it, I was constrained to appeal unto Caesar, not that I had anything to accuse my nation of.
20 For this cause therefore I have called for you, to see you and to speak with you: because for the hope of Israel I am bound with this chain.
21 And they said unto him, We neither received letters out of Judaea concerning thee, neither any of the brethren that came showed or spoke any harm of thee.
22 But we desire to hear of thee what thou thinkest; for as concerning this sect, we know that everywhere it is spoken against.
23 ¶ And when they had appointed him a day, many came to him into his lodging, to whom he expounded and testified the kingdom of God, procuring to persuade them of that concerning Jesus, the Christ, out of the law of Moses and out of the prophets, from morning until evening.
24 And some believed the things which were spoken, and some did not believe.
25 And when they did not agree among themselves, they departed, after Paul had spoken this word, Well spoke the Holy Spirit by Isaiah the prophet unto our fathers,
26 saying, Go unto this people, and say, Hearing ye shall hear and shall not understand; and seeing ye shall see and not perceive;
27 for the heart of this people is waxed gross, and their ears are dull of hearing, and their eyes have they closed; lest they should see with their eyes and hear with their ears and understand with their heart and should be converted and I should heal them.
28 Be it known, therefore, unto you that this saving health of God is sent unto the Gentiles and that they will hear it.
29 And when he had said these words, the Jews departed and had a great dispute among themselves.
30 ¶ And Paul dwelt two whole years in his own hired house and received all that came in unto him,
31 preaching the kingdom of God and teaching those things which concern the Lord Jesus Christ, with all liberty, without hindrance.
Acts 28
King James Version
28 And when they were escaped, then they knew that the island was called Melita.
2 And the barbarous people shewed us no little kindness: for they kindled a fire, and received us every one, because of the present rain, and because of the cold.
3 And when Paul had gathered a bundle of sticks, and laid them on the fire, there came a viper out of the heat, and fastened on his hand.
4 And when the barbarians saw the venomous beast hang on his hand, they said among themselves, No doubt this man is a murderer, whom, though he hath escaped the sea, yet vengeance suffereth not to live.
5 And he shook off the beast into the fire, and felt no harm.
6 Howbeit they looked when he should have swollen, or fallen down dead suddenly: but after they had looked a great while, and saw no harm come to him, they changed their minds, and said that he was a god.
7 In the same quarters were possessions of the chief man of the island, whose name was Publius; who received us, and lodged us three days courteously.
8 And it came to pass, that the father of Publius lay sick of a fever and of a bloody flux: to whom Paul entered in, and prayed, and laid his hands on him, and healed him.
9 So when this was done, others also, which had diseases in the island, came, and were healed:
10 Who also honoured us with many honours; and when we departed, they laded us with such things as were necessary.
11 And after three months we departed in a ship of Alexandria, which had wintered in the isle, whose sign was Castor and Pollux.
12 And landing at Syracuse, we tarried there three days.
13 And from thence we fetched a compass, and came to Rhegium: and after one day the south wind blew, and we came the next day to Puteoli:
14 Where we found brethren, and were desired to tarry with them seven days: and so we went toward Rome.
15 And from thence, when the brethren heard of us, they came to meet us as far as Appii forum, and The three taverns: whom when Paul saw, he thanked God, and took courage.
16 And when we came to Rome, the centurion delivered the prisoners to the captain of the guard: but Paul was suffered to dwell by himself with a soldier that kept him.
17 And it came to pass, that after three days Paul called the chief of the Jews together: and when they were come together, he said unto them, Men and brethren, though I have committed nothing against the people, or customs of our fathers, yet was I delivered prisoner from Jerusalem into the hands of the Romans.
18 Who, when they had examined me, would have let me go, because there was no cause of death in me.
19 But when the Jews spake against it, I was constrained to appeal unto Caesar; not that I had ought to accuse my nation of.
20 For this cause therefore have I called for you, to see you, and to speak with you: because that for the hope of Israel I am bound with this chain.
21 And they said unto him, We neither received letters out of Judaea concerning thee, neither any of the brethren that came shewed or spake any harm of thee.
22 But we desire to hear of thee what thou thinkest: for as concerning this sect, we know that every where it is spoken against.
23 And when they had appointed him a day, there came many to him into his lodging; to whom he expounded and testified the kingdom of God, persuading them concerning Jesus, both out of the law of Moses, and out of the prophets, from morning till evening.
24 And some believed the things which were spoken, and some believed not.
25 And when they agreed not among themselves, they departed, after that Paul had spoken one word, Well spake the Holy Ghost by Esaias the prophet unto our fathers,
26 Saying, Go unto this people, and say, Hearing ye shall hear, and shall not understand; and seeing ye shall see, and not perceive:
27 For the heart of this people is waxed gross, and their ears are dull of hearing, and their eyes have they closed; lest they should see with their eyes, and hear with their ears, and understand with their heart, and should be converted, and I should heal them.
28 Be it known therefore unto you, that the salvation of God is sent unto the Gentiles, and that they will hear it.
29 And when he had said these words, the Jews departed, and had great reasoning among themselves.
30 And Paul dwelt two whole years in his own hired house, and received all that came in unto him,
31 Preaching the kingdom of God, and teaching those things which concern the Lord Jesus Christ, with all confidence, no man forbidding him.
© 2017 Bible League International
Copyright © 2013, 2020 by Ransom Press International