Add parallel Print Page Options

Paulo Katika Kisiwa cha Malta

28 Tulipokuwa salama nchi kavu, tukatambua kuwa kisiwa kile kinaitwa Malta. Watu walioishi pale walikuwa wema sana kwetu. Mvua ilikuwa inanyesha na kulikuwa baridi sana, hivyo walitengeneza moto na kutukaribisha sote. Paulo alikusanya kuni nyingi kwa ajili ya moto. Alipokuwa akiweka kuni kwenye moto, nyoka mwenye sumu kali akajitokeza kwa sababu ya joto na kumuuma kwenye mkono. Wenyeji wa kisiwa kile walipomwona nyoka ananing'inia kwenye mkono wa Paulo, walisema, “Mtu huyu lazima ni mwuaji! Hakufa baharini, lakini Haki[a] hataki aishi.”

Lakini Paulo alimku'ngutia nyoka kwenye moto na hakudhurika. Watu wakadhani atavimba au ataanguka na kufa. Walisubiri na kumwangalia kwa muda mrefu, lakini hakuna kibaya kilichomtokea. Hivyo wakabadili mawazo yao. Wakasema, “Paulo ni mungu!”

Yalikuwepo mashamba kuzunguka eneo lile. Yaliyomilikiwa na ofisa wa juu sana wa Rumi katika kisiwa hicho aliyeitwa Pablio. Alitukaribisha nyumbani kwake na alikuwa mwema sana kwetu. Tulikaa nyumbani kwake kwa siku tatu. Baba yake Pablio alikuwa mgonjwa sana. Alikuwa na homa na alikuwa anaharisha damu, lakini Paulo alikwenda kwake na kumuombea. Aliweka mikono juu yake naye akapona. Baada ya hili kutokea, wagonjwa wengine wote kisiwani walikuja kwa Paulo, naye aliwaombea na wakaponywa pia.

10-11 Watu katika kisiwa hiki walituheshimu sana. Na baada ya kuwa pale kwa miezi mitatu, tukawa tayari kuondoka, walitupa kila kitu tulichohitaji kwa ajili ya safari yetu.

Paulo Aenda Rumi

Tulipanda meli iliyotoka Iskanderia iliyokaa katika kisiwa cha Malta wakati majira ya baridi. Mbele ya meli kulikuwa alama ya miungu pacha.[b] 12 Tulisimama katika mji wa Sirakuse. Tulikaa pale kwa siku tatu kisha tukaondoka. 13 Tulifika katika mji wa Regio. Siku iliyofuata upepo ulianza kuvuma kutokea Kusini-Magharibi, hivyo tuliweza kuondoka. Baada ya siku moja tukafika katika mji wa Puteoli. 14 Tuliwapata baadhi ya waamini pale, walituomba tukae nao kwa wiki moja. Mwishowe tulifika Rumi. 15 Ndugu na dada waliokaa Rumi walisikia habari zetu, walikuja kutupokea kwenye Soko la Apio[c] na kwenye Migahawa Mitatu.[d] Paulo alipowaona waamini hawa, alimshukuru Mungu na alifarijika.

Paulo Akiwa Rumi

16 Tulipofika Rumi, Paulo aliruhisiwa kuishi peke yake. Lakini askari alikaa pamoja naye kumlinda.

17 Siku tatu baadaye Paulo aliagiza baadhi ya Wayahudi muhimu waje kwake. Walipokusanyika, akasema, “Ndugu zangu, sijafanya lolote kinyume na watu wetu au kinyume na desturi za baba zetu. Lakini nilikamatwa Yerusalemu na kukabidhiwa kwa Warumi. 18 Waliniuliza maswali mengi, lakini hawakupata sababu yoyote kwa nini niuawe. Hivyo walitaka kuniachia huru. 19 Lakini Wayahudi kule hawakutaka hilo. Hivyo ilinibidi niombe kuja Rumi kuweka mashitaka yangu mbele ya Kaisari. Kwa kufanya hivi haimaanishi kuwa ninawashutumu watu wangu kwa kufanya chochote kibaya. 20 Ndiyo sababu nilitaka kuonana na kuzungumza nanyi. Nimefungwa kwa minyororo hii kwa sababu ninaamini katika tumaini la Israeli.”

21 Wayahudi walimjibu Paulo, “Hakuna barua tuliyoipokea kutoka Uyahudi kuhusu wewe. Hakuna ndugu yetu yeyote Myahudi aliyesafiri kutoka huko aliyeleta habari zako au kutwambia chochote kibaya juu yako. 22 Tunataka kusikia mawazo yako. Tunafahamu kuwa watu kila mahali wanapinga kundi hili jipya.”

23 Paulo na Wayahudi walichagua siku kwa ajili ya mkutano. Siku hiyo Wayahudi wengi walikutana na Paulo katika nyumba yake. Aliwaambia kwa siku nzima, akawafafanulia kuhusu ufalme wa Mungu. Alitumia Sheria ya Musa na maandishi ya manabii kuwashawishi kumwamini Yesu. 24 Baadhi ya Wayahudi waliamini alichosema, lakini wengine hawakuamini. 25 Walibishana wao wenyewe na wakaanza kuondoka. Lakini aliwaambia kitu kimoja zaidi: “Roho Mtakatifu aliwaambia ukweli baba zenu kupitia nabii Isaya, aliposema,

26 ‘Nenda kwa watu hawa na uwaambie:
Mtasikiliza na kusikiliza,
    lakini hamtaelewa.
Mtatazama na kutazama,
    lakini hakika hamtaona.
27 Watu hawa hawawezi kuelewa.
    Masikio yao yamezibwa.
    Na macho yao yamefumbwa.
Hivyo hawawezi kuona kwa macho yao,
    au kusikia kwa masikio yao;
    au kuelewa kwa akili zao;
    au kuelewa kwa akili zao.
Ikiwa wangeelewa, wangeweza kunirudia,
    na ningewaponya.’(A)

28 Ninataka ninyi Wayahudi mjue kuwa Mungu ameupeleka wokovu wake kwa watu wasio Wayahudi. Watasikia!” 29 [e]

30 Paulo alikaa katika nyumba yake mwenyewe aliyopanga kwa miaka miwili kamili. Aliwakaribisha watu wote waliokuja kumtembelea. 31 Aliwaambia kuhusu ufalme wa Mungu na kuwafundisha kuhusu Bwana Yesu Kristo. Alikuwa na ujasiri sana, na hakuna aliyejaribu kumzuia asizungumze.

Footnotes

  1. 28:4 Haki Wenyeji wa kisiwa kile waliamini kuwa kuna mungu mke aliyeitwa Haki ambaye angewaadhibu waovu.
  2. 28:10-11 miungu pacha Sanamu ya Kasto na Polu, miungu wa Kiyunani.
  3. 28:15 Soko la Apio Mji ulio kama maili 43 (kilomita 69) kutoka mji wa Rumi.
  4. 28:15 Migahawa Mitatu Mji ulio kama maili 30 (kilomita 48) kutoka mji wa Rumi.
  5. 28:29 Nakala zingine za baadaye za Matendo zimeongeza mstari wa 29: “Baada ya Paulo kusema hivi, Wayahudi walianza kuondoka, wakiwa bado wanabishana wao kwa wao.”

在馬爾他島

28 我們安全上岸後,才知道那個島的名字叫馬爾他。 島上的居民對我們非常友善。因為下雨,天氣又冷,他們就生火接待我們。 保羅拿起一捆柴放進火堆裡,不料有一條毒蛇經不住熱鑽了出來,咬住了他的手。 那裡的居民看見毒蛇吊在保羅手上,就交頭接耳地說:「這人一定是個兇手,雖然僥倖沒有淹死,天理卻不容他活下去。」 可是保羅把蛇甩進火裡,並沒有受傷。 他們以為保羅的手一定會腫起來或者他會突然倒斃,但是等了很久,見他還是安然無恙,就改變了態度,說他是個神明。

那個島的首領名叫部百流,他的田產就在附近。他接待我們,熱情款待了我們三天。 當時,部百流的父親患痢疾,正發熱躺在床上。保羅去為他禱告,把手按在他身上治好了他。 這事以後,島上其他的病人都來了,他們都得了醫治。 10 他們處處尊敬我們,在我們啟航的時候,又贈送我們途中所需用的物品。

保羅抵達羅馬

11 三個月後,我們搭乘一艘停在該島過冬的船離開。這船叫「雙神號」,來自亞歷山大。 12 我們先到敘拉古港,在那裡停泊三天, 13 然後繼續前行,到達利基翁。第二天,起了南風,第三天我們抵達部丟利, 14 在那裡遇見幾位弟兄姊妹,應邀和他們同住了七天,然後前往羅馬。 15 那裡的弟兄姊妹聽說我們來了,便到亞比烏和三館迎接我們。保羅見到他們後,就感謝上帝,心中受到鼓勵。 16 進了羅馬城後,保羅獲准在衛兵的看守下自己一個人住。

繼續傳道

17 三天後,保羅請來當地猶太人的首領,對他們說:「弟兄們,雖然我沒有做過任何對不起同胞或違背祖先規矩的事,卻在耶路撒冷遭囚禁,又被交到羅馬人的手裡。 18 羅馬官員審訊了我,發現我沒有什麼該死的罪,想釋放我, 19 猶太人卻反對,我不得已只好上訴凱撒。我並非有什麼事要控告自己的同胞。 20 為此,我才請你們來當面談,我受捆綁是為了以色列人所盼望的那位。」

21 他們說:「猶太境內的同胞沒有給我們寫信提及你的事,也沒有弟兄到這裡說你的壞話。 22 不過,我們倒很想聽聽你的觀點,因為我們知道你們這一派的人到處受人抨擊。」

23 於是,他們和保羅約定了會面的日期。那一天,很多人來到保羅住的地方。從早到晚,保羅向他們傳揚上帝國的道,引用摩西律法和先知書勸他們相信有關耶穌的事。 24 有些人聽後相信了他的話,有些人不相信, 25 他們彼此意見不一。在他們散去之前,保羅說了一句話:「聖靈藉以賽亞先知對你們祖先所說的話真是一點不錯, 26 祂說,

『你去告訴百姓,
你們聽了又聽,卻不明白;
看了又看,卻不領悟。
27 因為這百姓心靈麻木,
耳朵發背,眼睛昏花,
以致眼睛看不見,
耳朵聽不見,心裡不明白,無法回心轉意,
得不到我的醫治。』

28 所以你們當知道,上帝的救恩已經傳給了外族人,他們也必聽。」

29 聽完保羅的話後,那些猶太人就回去了,他們中間起了激烈的爭論。[a]

30 後來,保羅租了一間房子,在那裡住了整整兩年,接待所有到訪的人。 31 他勇敢地傳講上帝的國,教導有關主耶穌基督的事,沒有受到任何攔阻。

Footnotes

  1. 28·29 有古卷無「聽完保羅的話後,那些猶太人就回去了,他們中間起了激烈的爭論。」