Font Size
Warumi 7:13-15
Neno: Bibilia Takatifu
Warumi 7:13-15
Neno: Bibilia Takatifu
13 Je, hii ina maana kwamba sheria ambayo ni njema ilinile tea kifo? La, sivyo. Lakini ili dhambi itambuliwe kuwa ni dhambi, iliniletea kifo kwa njia ya sheria ambayo ni nzuri; kusudi kwa njia ya sheria, dhambi ionekane kuwa mbaya kabisa.
Mgongano Kati Ya Mwili Na Roho
14 Tunafahamu kwamba sheria ni ya kiroho. Lakini mimi si wa kiroho; mimi nimeuzwa utumwani, ni mtumwa wa dhambi. 15 Sielewi nitendalo: kwa maana lile ninalotaka kulifanya, sifanyi; badala yake, ninafanya lile ambalo nachukia kulifanya.
Read full chapter
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Copyright © 1989 by Biblica