Warumi 3
Neno: Bibilia Takatifu
Uaminifu Wa Mungu
3 Basi kuna faida gani kuwa Myahudi? Je, kutahiriwa kuna faida yo yote? 2 Ndio, zipo faida nyingi. Kwanza, Mungu aliwaka bidhi Wayahudi maagizo yake. 3 Na hata kama baadhi yao hawaku amini,je, kutokuamini kwao kutamfanya Mungu aache kuwa mwaminifu? 4 Hata kidogo!Mungu ataendelea kuwa wa kweli hata kama kila mwan adamu atakuwa mwongo. Kama ilivyoandikwa katika Maandiko,“Wewe Mungu, uthibitishwe kuwa wahaki katika maneno yako, na mshindi katika hukumu.”
5 Lakini iwapo uovu wetu unadhihirisha wazi kwamba Mungu ni mwenye haki, tusemeje basi? Je, tuseme kuwa Mungu hana haki kutuadhibu? Hapa ninasema kibinadamu. 6 La hasha! Mun gu ana haki kabisa kutughadhibikia! Kama sivyo, Mungu angewezaje kuuhukumu ulimwengu? 7 Mtu anaweza kusema,“Kama uongo wangu unasaidia kuonyesha ukweli wa Mungu na hivyo kudhihirisha utukufu wake, kwa nini basi ninahukumiwa kama mwenye dhambi?” 8 Kwa nini tusiseme, kama wengine wanavyotusingizia kuwa tunasema, “Tutende maovu ili wema udhihirike”? Hakika hukumu wanayoipata ni ya haki.
Wote Wametenda Dhambi
9 Tusemeje basi? Sisi Wayahudi tunayo nafuu yo yote? Hata kidogo! Kama tulivyokwisha kusema, Wayahudi na Wagiriki, wote wanatawaliwa na nguvu ya dhambi. 10 Kama Maandiko yase mavyo:“Hakuna hata mmoja mwenye haki; 11 hakuna hata mmoja mwe nye kuelewa, hakuna hata mmoja amtafutaye Mungu. 1 2Wote wamepotoka na kwa pamoja hawana thamani yo yote; hakuna atendaye mema hata mmoja. 13 Makoo yao ni kama makaburi wazi, wanatumia ndimi zao kudanganya. Kwenye midomo yao mnasumu kama ya nyoka. 14 Vinywa vyao vimejaa laana na ukali. 15 Miguu yao huen da mbio kumwaga damu, 16 njia zote wanazopita huacha uharibifu na huzuni kuu, na 17 wala njia ya amani hawaifahamu. 18 Kumcha Mungu hakupo machonipao.”
Mungu hakupo machonipao.”
19 Basi tunafahamu ya kwamba maagizo yote ya sheria ya Musa yanawahusu wale walio chini ya sheria hiyo. Kusudi la sheria ni kuwafanya watu wote wasiwe na kisingizio na kuuweka ulimwengu wote chini ya hukumu ya Mungu. 20 Kwa hiyo hakuna binadamu hata mmoja atakayehesabiwa kuwa na haki mbele za Mungu kwa kufuata sheria; bali sheria hutufanya tutambue dhambi.
Haki Kwa Njia Ya Imani
21 Lakini sasa, njia ya Mungu ya kuwahesabia watu haki pasipo sheria, njia ambayo sheria na manabii huishuhudia, imekwisha dhihirishwa. 22 Haki hii itokayo kwa Mungu hupatikana kwa kumwaminiYesu Kristo. Mungu huwatendea hivi watu wote wamwa minio Kristo pasipo kubagua, 23 kwa maana wote wametenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu; 24 wote wanahesabiwa haki bure kwa neema yake kwa ukombozi ulioletwa na Yesu Kristo. 25 Mungu alimtoa awe dhabihu ya upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake. Alifanya hivi ili kuonyesha haki yake, kwani kwa uvumilivu wake hakuziadhibu dhambi za zamani. 26 Pia alifanya hivi ili kuonyesha kwa wakati huu kuwa yeye ni wa haki na kwamba yeye ndiye anayewahesabia haki watu wote wamwaminio Yesu.
Umuhimu Wa Kuwa Na Imani
27 Sasa kujivuna kwetu kuko wapi basi? Hakupo. Je kumeondo lewa kwa msingi gani? Kwa msingi wa kutimiza sheria? La. Kumeon dolewa kwa msingi wa imani. 28 Kwa maana tunasisitiza kwamba mwanadamu anahesabiwa haki kwa njia ya imani na wala si kwa kutenda maagizo ya sheria. 29 Je, Mungu ni Mungu wa Wayahudi peke yao? Je, yeye si Mungu wa watu wa mataifa mengine pia? Ndio, yeye ni Mungu wa watu wa mataifa mengine pia. 30 Basi kwa kuwa Mungu ni mmoja, atawahesabia haki wale waliotahiriwa kutokana na imani yao na wale wasiotahiriwa kutokana na imani yao. 31 Je, ina maana kwamba tunaifuta sheria kwa imani hii? La, sivyo. Kiny ume chake: tunaithibitisha sheria.
Romans 3
King James Version
3 What advantage then hath the Jew? or what profit is there of circumcision?
2 Much every way: chiefly, because that unto them were committed the oracles of God.
3 For what if some did not believe? shall their unbelief make the faith of God without effect?
4 God forbid: yea, let God be true, but every man a liar; as it is written, That thou mightest be justified in thy sayings, and mightest overcome when thou art judged.
5 But if our unrighteousness commend the righteousness of God, what shall we say? Is God unrighteous who taketh vengeance? (I speak as a man)
6 God forbid: for then how shall God judge the world?
7 For if the truth of God hath more abounded through my lie unto his glory; why yet am I also judged as a sinner?
8 And not rather, (as we be slanderously reported, and as some affirm that we say,) Let us do evil, that good may come? whose damnation is just.
9 What then? are we better than they? No, in no wise: for we have before proved both Jews and Gentiles, that they are all under sin;
10 As it is written, There is none righteous, no, not one:
11 There is none that understandeth, there is none that seeketh after God.
12 They are all gone out of the way, they are together become unprofitable; there is none that doeth good, no, not one.
13 Their throat is an open sepulchre; with their tongues they have used deceit; the poison of asps is under their lips:
14 Whose mouth is full of cursing and bitterness:
15 Their feet are swift to shed blood:
16 Destruction and misery are in their ways:
17 And the way of peace have they not known:
18 There is no fear of God before their eyes.
19 Now we know that what things soever the law saith, it saith to them who are under the law: that every mouth may be stopped, and all the world may become guilty before God.
20 Therefore by the deeds of the law there shall no flesh be justified in his sight: for by the law is the knowledge of sin.
21 But now the righteousness of God without the law is manifested, being witnessed by the law and the prophets;
22 Even the righteousness of God which is by faith of Jesus Christ unto all and upon all them that believe: for there is no difference:
23 For all have sinned, and come short of the glory of God;
24 Being justified freely by his grace through the redemption that is in Christ Jesus:
25 Whom God hath set forth to be a propitiation through faith in his blood, to declare his righteousness for the remission of sins that are past, through the forbearance of God;
26 To declare, I say, at this time his righteousness: that he might be just, and the justifier of him which believeth in Jesus.
27 Where is boasting then? It is excluded. By what law? of works? Nay: but by the law of faith.
28 Therefore we conclude that a man is justified by faith without the deeds of the law.
29 Is he the God of the Jews only? is he not also of the Gentiles? Yes, of the Gentiles also:
30 Seeing it is one God, which shall justify the circumcision by faith, and uncircumcision through faith.
31 Do we then make void the law through faith? God forbid: yea, we establish the law.
Copyright © 1989 by Biblica