Ibada Ya Kiroho

12 Kwa hiyo ndugu zangu nawasihi kwa sababu ya huruma zake Mungu, jitoeni kwake muwe sadaka hai, takatifu na inayompendeza Mungu, ambayo ndio ibada yenu ya kiroho. Msiige tabia na mien endo ya dunia hii bali mbadilishwe, nia zenu zikifanywa kuwa mpya, ili mpate kuwa na hakika ni nini mapenzi ya Mungu: yaliyo mema, yanayopendeza machoni pake na makamilifu.

Kwa sababu ya neema niliyopewa nawaambia kila mmoja wenu: Msijifikirie kuwa watu wa juu kuliko mlivyo. Badala yake, muwe na kiasi katika mawazo yenu, kila mmoja wenu ajipime kutokana na kiasi cha imani aliyopewa na Mungu. Kama vile ambavyo kila mmoja wenu ana mwili mmoja wenye viungo vingi, na kila kiungo kina kazi yake, hali kadhalika, ndani ya Kristo sisi tulio wengi tunakuwa mwili mmoja na kila mmoja wetu ni sehemu ya we ngine wote. Tumepewa vipawa tofauti kulingana na neema tuliy opokea kutoka kwa Mungu. Kama mtu ana kipawa cha kutoa unabii basi akitumie kulingana na imani yake. Kama kipawa chake ni kuwahudumia wengine, basi awahudumie. Kama ni kufundisha, basi na afundishe. Kama kipawa chake ni kuwatia moyo wengine, na afanye hivyo. Kama ni ukarimu, basi na atoe kwa moyo. Mwenye kipawa cha uongozi na afanye hivyo kwa bidii. Mwenye kipawa cha huruma na aonyeshe huruma yake kwa furaha.

Upendo Wa Kweli

Upendo wenu uwe wa kweli. Chukieni uovu, mshikilie yaliyo mema. 10 Pendaneni ninyi kwa ninyi kwa upendo wa kindugu. Waheshimuni wengine kuliko mnavyojiheshimu wenyewe. 11 Juhudi yenu isipungue, moto wenu wa kiroho uendelee kuwaka mkimtumikia Mungu. 12 Muwe na furaha katika tumaini lenu, na katika dhiki muwe na subira. Ombeni wakati wote. 13 Wasaidieni watu wa Mungu walio na shida. Muwe wakarimu kwa matendo.

14 Waombeeni baraka za Mungu wanaowatesa. Wabarikini wala msiwalaani. 15 Furahini pamoja na wenye furaha; huzunikeni pamoja na wenye huzuni. 16 Muishi kwa amani ninyi kwa ninyi. Msitake makuu bali muwe tayari kushirikiana na wanyonge. Kamwe msiwe watu wenye majivuno.

17 Msimlipe mtu uovu kwa uovu. Jitahidini kutenda yaliyo mema machoni pa watu wote. 18 Kama ikiwezekana, kaeni kwa amani na watu wote. 19 Wapendwa, msijilipizie kisasi, bali mtoe nafasi kwa ghadhabu ya Mungu, maana imeandikwa:“Kisasi ni juu yangu; Mimi nitalipa, asema Bwana. 20 Badala yake, adui yakoakiwa na njaa, mpe chakula; akiwa na kiu, mpe kitu anywe. Maana ukifanya hivyo, utampalia mkaa wa moto kichwani pake. 21 Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema.

为事奉上帝而活

12 所以,弟兄姊妹,我凭上帝的怜悯劝你们献上自己的身体,作圣洁、蒙上帝悦纳的活祭。你们理当这样事奉。 你们不可追随世界的潮流,要随着思想的不断更新而改变,这样就能明辨上帝的旨意,知道什么是良善、纯全、蒙祂悦纳的。

我凭上帝赐给我的恩典劝告各位,不要自视过高,要照着上帝赐给各人的信心中肯地看待自己。 就像我们身体的各部分有不同的功能, 我们众人在基督里组成一个身体,彼此联结,息息相关。 我们照所得的恩典各有不同的恩赐。说预言的,要按着信心的程度说预言; 服侍的,要忠心服侍;教导的,要专一教导; 劝勉的,要诚心劝勉;施舍的,要慷慨施舍;治理的,要殷勤治理;怜悯的,要甘心怜悯。

相爱相顾

不可虚情假意地爱人。要疾恶如仇,一心向善。 10 要彼此相爱如同手足,互相尊重,彼此谦让。 11 要殷勤,不可懒惰,要常常火热地事奉主。 12 盼望中要有喜乐,患难中要坚忍,祷告要恒切。 13 信徒有缺乏,要慷慨帮助;客人来访,要热诚款待。 14 迫害你们的,要为他们祝福;要祝福,不可咒诅。 15 要与喜乐的人同乐,与哀哭的人同哭。 16 要彼此和睦,不可心高气傲,反要俯就卑微的人,不可自以为聪明。

17 不要以恶报恶。要尊重别人,众人都认为好的事,应该竭力去做。 18 如果可能,总要尽力与人和睦相处。 19 亲爱的弟兄姊妹,不要私自报复,要让上帝来审判,因为圣经上说:

“主说,‘申冤在我,我必报应。’”

20 所以,

“你的仇敌若饿了,就给他吃的;
若渴了,就给他喝的;
你这样做是把炭火堆在他头上。”

21 你不可被恶所胜,反要以善胜恶。