Yerusalemu, Yudea na kutoka ng’ambo ya mto Yordani.

Yesu alipoona umati wa watu, alipanda mlimani akaketi chini. Wanafunzi wake wakamjia, naye akaanza kuwafundisha akisema:

“Wamebarikiwa walio maskini wa roho; maana Ufalme wa mbin guni ni wao. Wamebarikiwa wanaoomboleza; maana watafarijiwa. Wamebarikiwa walio wapole; maana watairithi nchi. Wamebari kiwa wenye hamu ya kutenda haki; maana wataridhishwa. Wamebari kiwa walio na huruma; maana nao watahurumiwa. Wamebarikiwa walio na moyo safi; maana watamwona Mungu. Wamebarikiwa walio wapatanishi; maana wataitwa wana wa Mungu. 10 Wamebarikiwa wanaoteswa kwa kutenda haki; maana Ufalme wa mbinguni ni wao.

11 Mmebarikiwa ninyi wakati watu watakapowatukana na kuwatesa na kuwasingizia maovu kwa ajili yangu. 12 Shangilieni na kufurahi, kwa maana zawadi yenu huko mbinguni ni kubwa; kwa kuwa ndivyo walivyowatesa manabii waliowatangulia ninyi.

Read full chapter