Mafundisho Ya Kale

Mafarisayo na baadhi ya walimu wa sheria waliokuwa wametoka Yerusalemu walikusanyika mbele ya Yesu. Wakawaona baadhi ya wanafunzi wake wakila chakula bila kunawa kama ilivyotakiwa na sheria ya dini ya Wayahudi. Wayahudi, na hasa Mafarisayo, hawali chakula pasipo kunawa kwa kufuata mila za wazee wao. Na kwa sheria wanapotoka sokoni hawawezi kula pasipo kunawa. Pia kuna desturi nyingine nyingi wanazofuata kama vile jinsi ya kuosha vikombe, vyungu, na vyombo vya shaba.

Kwa hiyo wale Mafarisayo na walimu wa sheria walimwuliza Yesu, “Mbona wanafunzi wako hawafuati desturi za wazee wetu, na badala yake wa nakula kwa mikono najisi?”

Yesu akawajibu, “Nabii Isaya alisema ukweli alipotabiri juu yenu, ninyi wanafiki, kama ilivyoandikwa: ‘Watu hawa wanani heshimu kwa midomo yao, lakini mioyoni mwao wako mbali nami. Kuniabudu kwao ni bure. Wanafundisha watu amri zao badala ya sheria yangu.’ Ninyi mmeziacha amri za Mungu na kushikilia desturi za watu.” Akawaambia, “Mnaepuka kwa ujanja amri za Mungu ili mpate kutimiza desturi zenu! 10 Kwa mfano, Musa alisema, ‘Waheshimu baba yako na mama yako’ na ‘Ye yote amtuka naye baba au mama auawe.’ 11 Lakini ninyi mnasema mtu akimwambia baba yake au mama yake kuwa, “Msaada ambao ningekupa ni Kor bani,” yaani umetengwa kama sadaka kwa Mungu, 12 basi hawaji biki tena kumsaidia baba yake au mama yake. 13 Kwa njia hiyo mnadhalilisha neno la Mungu kwa taratibu zenu mlizojiwekea. Na mnafanya mambo mengi ya jinsi hii.”

14 Yesu akaita tena ule umati wa watu akawaambia, “Nisiki lizeni nyote kwa makini na muelewe. 15 Hakuna kitu kinachomwin gia mtu kutoka nje ambacho kinaweza kumfanya mchafu. Kitu kina chotoka ndani yake ndicho kinachomfanya mchafu. 16 Mwenye nia ya kusikia na asikie.”

17 Alipoachana na wale watu aliingia ndani. Wanafunzi wake wakamwuliza maana ya mfano ule. 18 Akawajibu, “Hata nanyi hamwelewi? Hamtambui kwamba kitu kimwingiacho mtu kutoka nje hakiwezi kumfanya mchafu? 19 Mtu akila kitu hakiingii moyoni mwake bali tumboni, na baadaye hutolewa nje. Kwa kusema hivi, Yesu alifundisha kuwa aina zote za vyakula ni halali kuliwa.

20 Akaendelea kusema, “Kile kitokacho ndani ya mtu ndicho kinachomfanya awe mchafu. 21 Kwa maana ndani ya mtu, yaani moy oni mwake, hutoka: mawazo mabaya, uasherati, 22 wizi, uuaji, uzinzi, tamaa mbaya, uovu, udanganyifu, ufisadi, wivu, matusi, kiburi na upumbavu. 23 Maovu haya yote hutoka ndani ya mtu, na ndio yanayomfanya mchafu.”

Yesu Amponya Binti Ya Mama Mtaifa

24 Ndipo Yesu akaondoka hapo akaenda sehemu za Tiro. Akaingia nyumba moja, ambapo hakupenda mtu afahamu yupo. Lakini hakuweza kujificha. 25 Mama mmoja ambaye binti yake mdogo ali kuwa na pepo mchafu aliposikia habari za Yesu, alikuja mara moja akajiangusha miguuni pake. 26 Huyo mama hakuwa Myahudi, alikuwa Mgiriki aliyezaliwa Siria-Foinike. Akamsihi Yesu amtoe binti yake huyo pepo mchafu.

27 Yesu akamwambia, “Tuwaache watoto wale washibe kwanza, kwa maana si halali kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.”

28 Yule mama akajibu, “Ni kweli Bwana, lakini hata mbwa walio chini ya meza hula makombo ya watoto.” 29 Yesu akamjibu, “Kwa sababu ya jibu lako, unaweza kwenda nyumbani. Yule pepo ameshamtoka binti yako.”

30 Akaenda nyumbani akamkuta binti yake amelala kitandani, na pepo amemtoka.

Yesu Amponya Mtu Aliyekuwa Bubu Na Kiziwi

31 Yesu akaondoka katika eneo la Tiro, akapita katikati ya Sidoni akaenda hadi Ziwa la Galilaya kwa kupitia katika eneo la Dekapoli. 32 Hapo, watu walimletea kiziwi mmoja ambaye pia alikuwa hawezi kusema sawa sawa, wakamwomba amwekee mikono ili apone. 33 Yesu akampeleka yule kiziwi kando mbali na watu, akain giza vidole masikioni mwake kisha akatema mate na akaugusa ulimi wake. 34 Ndipo Yesu akatazama mbinguni, akahema kwa uchungu, akamwambia, “Efatha!” yaani “Funguka!” 35 Wakati huo huo masikio ya yule mtu yakafunguka na ulimi wake ukawa huru akaanza kusema vizuri.

36 Yesu akawaamuru wasimwambie mtu ye yote habari hizi. Lakini kadiri alivyowazuia ndivyo walivyozidi kutangaza habari zake. 37 Watu wakastaajabu mno. Wakasema, “Amefanya mambo yote vizuri mno! Amewawezesha viziwi wasikie na bubu waseme!”

礼上的污秽

有法利赛人和几个文士从耶路撒冷来,到耶稣那里聚集。 他们曾看见他的门徒中有人用俗手,就是没有洗的手吃饭。 (原来法利赛人和犹太人都拘守古人的遗传,若不仔细洗手就不吃饭; 从市上来,若不洗浴也不吃饭;还有好些别的规矩,他们历代拘守,就是洗杯、罐、铜器等物。) 法利赛人和文士问他说:“你的门徒为什么不照古人的遗传,用俗手吃饭呢?” 耶稣说:以赛亚指着你们假冒为善之人所说的预言是不错的,如经上说:‘这百姓用嘴唇尊敬我,心却远离我。 他们将人的吩咐当做道理教导人,所以拜我也是枉然。’ 你们是离弃神的诫命,拘守人的遗传。” 又说:“你们诚然是废弃神的诫命,要守自己的遗传。 10 摩西说:‘当孝敬父母’,又说:‘咒骂父母的,必治死他。’ 11 你们倒说,人若对父母说:‘我所当奉给你的,已经做了各耳板’(“各耳板”就是“供献”的意思) 12 以后你们就不容他再奉养父母。 13 这就是你们承接遗传,废了神的道!你们还做许多这样的事。”

心里的污秽

14 耶稣又叫众人来,对他们说:“你们都要听我的话,也要明白。 15 从外面进去的不能污秽人,唯有从里面出来的乃能污秽人。[a] 17 耶稣离开众人,进了屋子,门徒就问他这比喻的意思。 18 耶稣对他们说:“你们也是这样不明白吗?岂不晓得凡从外面进入的,不能污秽人? 19 因为不是入他的心,乃是入他的肚腹,又落到茅厕里。”这是说,各样的食物都是洁净的。 20 又说:“从人里面出来的,那才能污秽人。 21 因为从里面,就是从人心里发出恶念、苟合、 22 偷盗、凶杀、奸淫、贪婪、邪恶、诡诈、淫荡、嫉妒、谤讟、骄傲、狂妄, 23 这一切的恶都是从里面出来,且能污秽人。”

妇人信心的赏赐

24 耶稣从那里起身,往推罗西顿的境内去。进了一家,不愿意人知道,却隐藏不住。 25 当下有一个妇人,她的小女儿被污鬼附着,听见耶稣的事,就来俯伏在他脚前。 26 这妇人是希腊人,属叙利非尼基族。她求耶稣赶出那鬼离开她的女儿。 27 耶稣对她说:“让儿女们先吃饱,不好拿儿女的饼丢给狗吃。” 28 妇人回答说:“主啊,不错,但是狗在桌子底下也吃孩子们的碎渣儿!” 29 耶稣对她说:“因这句话,你回去吧!鬼已经离开你的女儿了。” 30 她就回家去,见小孩子躺在床上,鬼已经出去了。

医治耳聋舌结的人

31 耶稣又离了推罗的境界,经过西顿,就从低加波利境内来到加利利海。 32 有人带着一个耳聋舌结的人来见耶稣,求他按手在他身上。 33 耶稣领他离开众人到一边去,就用指头探他的耳朵,吐唾沫抹他的舌头, 34 望天叹息,对他说:“以法大!”就是说:“开了吧!” 35 他的耳朵就开了,舌结也解了,说话也清楚了。 36 耶稣嘱咐他们不要告诉人,但他越发嘱咐,他们越发传扬开了。 37 众人分外稀奇,说:“他所做的事都好,他连聋子也叫他们听见,哑巴也叫他们说话!”

Footnotes

  1. 马可福音 7:15 有古卷在此有:16有耳可听的,就应当听!