Marko 2
Neno: Bibilia Takatifu
Yesu Amponya Mtu Aliyepooza
2 Baada ya siku kadhaa Yesu alirudi Kapernaumu; watu waka pata habari kuwa amerudi nyumbani. 2 Wakakusanyika kwa wingi isibaki nafasi hata mlangoni! Naye akawahubiria. 3 Wakaja watu wanamletea Yesu mtu aliyepooza, akiwa amebebwa na watu wanne. 4 Waliposhindwa kumfikia Yesu kwa ajili ya msongamano wa watu, wakatoboa tundu darini, wakamshusha ndani yule aliyepooza kwa kitanda alichokuwa amelalia.
5 Yesu alipoona imani yao, akamwambia yule mgonjwa, “Mwa nangu, dhambi zako zimesamehewa.” 6 Baadhi ya walimu wa sheria waliokuwepo wakawaza mioyoni mwao, 7 “Mbona mtu huyu anasema maneno haya? Anakufuru! Hajui kuwa ni Mungu peke yake awezaye kusamehe dhambi?”
8 Yesu akatambua mawazo yao, kwa hiyo akawaambia, “Kwa nini mnawaza hivyo? 9 Ni jambo gani lililo rahisi zaidi, kumwambia huyu aliyepooza, ‘Umesamehewa dhambi zako,’? Au, ‘Inuka, chukua kitanda chako uende’? 10 Lakini ili kuwahakikishia kwamba mimi Mwana wa Adamu ninao uwezo hapa duniani wa kusamehe dhambi,” - akamwambia yule aliyepooza 11 “Nakuambia, inuka, chukua kitanda chako uende nyumbani.”
12 Yule mtu aliyekuwa amepooza akainuka, akachukua kitanda chake akatembea mbele yao wote! Tukio hili likawashangaza watu wote, wakamsifu Mungu, wakasema, “Hatujapata kuona jambo kama hili kamwe!”
Yesu Amwita Mathayo
13 Yesu akaenda tena kando kando ya Ziwa la Galilaya. Umati wa watu ukamfuata naye akaanza kuwafundisha. 14 Alipokuwa aki tembea, akamwona Lawi mwana wa Alfayo ameketi katika kibanda cha kukusanyia kodi, akamwambia, “Nifuate”. Lawi akatoka, akamfuata Yesu. 15 Yesu alipokuwa akila chakula nyumbani kwa Lawi, watoza ushuru wengi pamoja na wenye dhambi walikuwa wameketi mezani pamoja naye na wanafunzi wake; kwa maana watu wengi wa aina hii walikuwa wamemfuata. 16 Baadhi ya walimu wa sheria ambao wali kuwa Mafarisayo walipomwona anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi, wakawauliza wanafunzi wake, “Yesu anawezaje kula na watoza ushuru na wenye dhambi?” 17 Yesu aliposikia haya aka waambia, “Wenye afya nzuri hawahitaji daktari, bali wagonjwa wanamhitaji. Sikuja kuwaalika wenye haki, bali wenye dhambi.”
Yesu Afundisha Kuhusu Kufunga
18 Wakati mmoja wanafunzi wa Yohana pamoja na Mafarisayo walikuwa wamefunga. Baadhi ya watu wakaja kwa Yesu wakamwuliza, “Mbona wanafunzi wa Yohana na wa Mafarisayo hufunga na wako hawafungi?”
19 Yesu akawajibu, “Inawezekanaje wageni wa bwana harusi wafunge wakati bwana harusi yungali nao? Maadamu bwana harusi yupo, haiwezekani wafunge. 20 Lakini wakati utafika ambapo bwana harusi atachukuliwa. Siku hiyo ndipo watakapofunga.
21 “Hakuna mtu anayeshonea kiraka cha nguo mpya kwenye nguo iliyochakaa. Akifanya hivyo, ile nguo iliyochakaa itachanika zaidi pale penye kiraka kipya na kuharibika zaidi. 22 Wala hakuna mtu anayeweka divai mpya katika viriba vya zamani. Akifa nya hivyo, ile divai mpya itavipasua hivyo viriba, kwa hiyo ata poteza divai na viriba pia. Divai mpya huwekwa kwenye viriba vipya.”
Yesu Afundisha Kuhusu Sabato
23 Siku moja ya sabato, Yesu pamoja na wanafunzi wake, wal ikuwa wakipita katikati ya mashamba ya ngano. Wanafunzi wake wakaanza kuvunja masuke ya ngano. 24 Mafarisayo wakamwambia, “Mbona wanafanya jambo ambalo si halali kufanywa siku ya sabato?”
25 Yesu akawaambia, “Hamjasoma alivyofanya Daudi wakati yeye na wafuasi wake walipokuwa na njaa? 26 Aliingia katika nyumba ya Mungu wakati Abiatha akiwa kuhani mkuu, akala mkate wa sadaka walioruhusiwa kuula ni makuhani peke yao - na akawagawia wafuasi wake.” 27 Kisha akawaambia, “Sabato iliwekwa kwa faida ya mwanadamu, lakini mwanadamu hakuwekwa kwa ajili ya sabato. 28 Na mimi, Mwana wa Adamu, ni Bwana hata wa sabato.”
Marko 2
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yesu Amponya Aliyepooza
(Mt 9:1-8; Lk 5:17-26)
2 Siku chache baadaye Yesu alirudi Kapernaumu na habari zikaenea kuwa yupo nyumbani. 2 Hivyo watu wengi walikusanyika kumsikiliza akifundisha na haikuwapo nafasi iliyobaki kabisa ndani ya nyumba, hata nje ya mlango. Yesu alipokuwa akifundisha, 3 baadhi ya watu walimleta kwake mtu aliyepooza amwone. Mtu huyo alikuwa amebebwa na rafiki wanne. 4 Watu hao hawakuweza kumfikisha mgonjwa kwa Yesu kwa sababu ya umati wa watu ulioijaza nyumba yote. Hivyo walipanda na kuondoa paa juu ya sehemu aliposimama Yesu. Baada ya kutoboa tundu darini[a] kwenye paa, wakateremsha kirago alimokuwa amelala yule aliyepooza. 5 Yesu alipoona imani waliyokuwa nayo wale waliomleta na yule mwenye kupooza, alimwambia, “Mtoto wangu, dhambi zako zimesamehewa.”
6 Baadhi ya walimu wa sheria walikuwa wamekaa pale. Nao waliona kile alichokifanya Yesu na wakawaza miongoni mwa wenyewe, 7 “Kwa nini mtu huyu anasema maneno kama hayo? Si anamtukana Mungu! Kwani hakuna awezaye kusamehe dhambi ila Mungu.”
8 Mara moja Yesu alifahamu walichokuwa wakikifikiri wale walimu wa sheria, hivyo akawaambia, “Kwa nini mna maswali kama hayo mioyoni mwenu? 9 Wakati akiwa duniani Mwana wa Adamu anayo mamlaka ya kusamehe dhambi. Lakini nitawezaje kulithibitisha hili kwenu? Pengine mnafikiri ilikuwa rahisi kwangu kumwambia mtu huyu aliyepooza ‘Dhambi zako zimesamehewa,’ kwa sababu hilo haliwezi kuthibitishwa kwamba hakika limetokea. Lakini vipi nikimwambia mtu huyu, ‘Simama! Beba kirago chako na utembee’? 10 Hapo ndipo mtakapoweza kuona kama kweli ninayo mamlaka hayo ama sina!” Kwa hiyo Yesu akamwambia mtu yule aliyepooza, “Nitalithibitishaje hili kwako? 11 Ninakwambia hivi, ‘Inuka! Beba kirago chako uende nyumbani!’”
12 Yule mtu aliyepooza alisimama na bila kusita, akabeba kirago chake na akatoka nje ya nyumba wakati kila mmoja akiona. Matokeo yake ni kuwa wote walishangazwa na mambo hayo. Wakamsifu Mungu na kusema, “Hatujawahi kuona kitu kama hiki!”
Lawi (Mathayo) Amfuata Yesu
(Mt 9:9-13; Lk 5:27-32)
13 Mara nyingine tena Yesu akaelekea kandoni mwa ziwa, na watu wengi walikuwa wakimwendea, naye akawafundisha. 14 Alipokuwa akitembea kando ya ufukwe wa ziwa, alimwona Lawi mwana wa Alfayo ameketi katika mahala pake pa kukusanyia kodi. Yesu akamwambia, “Nifuate!” Hivyo Lawi akainuka na kumfuata.
15 Baadaye Yesu na wafuasi wake wa karibu walikuwa wakila chakula cha jioni nyumbani kwa Lawi. Wakusanya kodi wengi na watu wengine wenye sifa mbaya nao wakamfuata Yesu. Hivyo wengi wao walikuwa wakila pamoja na Yesu na wanafunzi wake. 16 Baadhi ya walimu wa sheria waliokuwa pamoja na Mafarisayo walipomwona Yesu akila na wenye dhambi na wanaokusanya kodi, wakawauliza wanafunzi wake, “Kwa nini Yesu anakula na wenye kukusanya kodi na watu wengine wenye dhambi?”
17 Yesu alipolisikia hili akawaambia, “Wale walio wagonjwa ndio wanaomhitaji daktari si wale walio wazima wa afya. Mimi nimekuja kuwakaribisha wenye dhambi waje kwangu sikuja kwa ajili ya wale wanaotenda kila kitu kwa haki.”
Swali Kuhusu Kufunga
(Mt 9:14-17; Lk 5:33-39)
18 Siku moja wafuasi wa Yohana Mbatizaji na Mafarisayo walikuwa wanafunga. Baadhi ya watu walimjia Yesu na kumwuliza, “Mbona wafuasi wa Yohana na wafuasi wa Mafarisayo wanafunga, lakini kwa nini wanafunzi wako hawafungi.”
19 Yesu akawajibu, “Katika sherehe ya arusi hutarajii marafiki wa bwana arusi wawe na huzuni wakati yeye mwenyewe yupo pamoja nao. Hakika hawatafunga ikiwa bwana arusi bado yuko pamoja nao. 20 Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kwao, na wakati huo ndipo watakapofunga.
21 Hakuna anayeshona kiraka kipya cha nguo kwenye vazi la zamani. Ikiwa atafanya hivyo kiraka hicho kipya kitajikunjakunja na kulinyofoa vazi hilo zee nalo litachanika vibaya zaidi. 22 Vivyo hivyo hakuna awekaye divai mpya ndani ya viriba vya zamani[b] vilivyozeeka. Akifanya hivyo, divai ile itachacha na hewa yake itavipasua vibuyu hivyo vya ngozi na kuviharibu kabisa pamoja na divai yenyewe. Badala yake mtu anaweka divai mpya ndani ya vibuyu vipya vya ngozi vya kuwekea divai.”
Yesu ni Bwana Juu ya Siku ya Sabato
(Mt 12:1-8; Lk 6:1-5)
23 Ikatokea kwamba katika siku ya Sabato Yesu na wanafunzi wake walikuwa wakipita katika mashamba ya nafaka. Wanafunzi wake walianza kuchuma masuke ya nafaka ile walipopita. 24 Baadhi ya Mafarisayo walipoliona hilo wakamwambia Yesu, “Tazama, kwa nini wanafunzi wako wanafanya hivi? Ni kinyume cha sheria kuchuma masuke ya nafaka katika siku ya Sabato?”
25 Yesu akajibu, “Hakika mmesoma kile alichofanya Daudi pale yeye pamoja na watu aliokuwa nao walipopata njaa na kuhitaji chakula. 26 Ilikuwa wakati wa Abiathari Kuhani Mkuu. Daudi aliingia katika nyumba ya Mungu na kula mkate uliotolewa kwa Bwana. Sheria ya Musa inasema ni makuhani peke yao ndio watakaoweza kuula mkate ule. Daudi aliwapa pia ule mkate mtakatifu watu waliokuwa pamoja naye.”
27 Ndipo Yesu akawaambia mafarisayo, “Siku ya Sabato ilifanywa kwa faida ya watu. Watu hawakuumbwa ili watawaliwe na Sabato. 28 Kwa hiyo Mwana wa Adamu ambaye ni Bwana juu ya kila kitu, pia ni Bwana juu ya siku ya Sabato.”
Mark 2
New International Version
Jesus Forgives and Heals a Paralyzed Man(A)
2 A few days later, when Jesus again entered Capernaum, the people heard that he had come home. 2 They gathered in such large numbers(B) that there was no room left, not even outside the door, and he preached the word to them. 3 Some men came, bringing to him a paralyzed man,(C) carried by four of them. 4 Since they could not get him to Jesus because of the crowd, they made an opening in the roof above Jesus by digging through it and then lowered the mat the man was lying on. 5 When Jesus saw their faith, he said to the paralyzed man, “Son, your sins are forgiven.”(D)
6 Now some teachers of the law were sitting there, thinking to themselves, 7 “Why does this fellow talk like that? He’s blaspheming! Who can forgive sins but God alone?”(E)
8 Immediately Jesus knew in his spirit that this was what they were thinking in their hearts, and he said to them, “Why are you thinking these things? 9 Which is easier: to say to this paralyzed man, ‘Your sins are forgiven,’ or to say, ‘Get up, take your mat and walk’? 10 But I want you to know that the Son of Man(F) has authority on earth to forgive sins.” So he said to the man, 11 “I tell you, get up, take your mat and go home.” 12 He got up, took his mat and walked out in full view of them all. This amazed everyone and they praised God,(G) saying, “We have never seen anything like this!”(H)
Jesus Calls Levi and Eats With Sinners(I)
13 Once again Jesus went out beside the lake. A large crowd came to him,(J) and he began to teach them. 14 As he walked along, he saw Levi son of Alphaeus sitting at the tax collector’s booth. “Follow me,”(K) Jesus told him, and Levi got up and followed him.
15 While Jesus was having dinner at Levi’s house, many tax collectors and sinners were eating with him and his disciples, for there were many who followed him. 16 When the teachers of the law who were Pharisees(L) saw him eating with the sinners and tax collectors, they asked his disciples: “Why does he eat with tax collectors and sinners?”(M)
17 On hearing this, Jesus said to them, “It is not the healthy who need a doctor, but the sick. I have not come to call the righteous, but sinners.”(N)
Jesus Questioned About Fasting(O)
18 Now John’s disciples and the Pharisees were fasting.(P) Some people came and asked Jesus, “How is it that John’s disciples and the disciples of the Pharisees are fasting, but yours are not?”
19 Jesus answered, “How can the guests of the bridegroom fast while he is with them? They cannot, so long as they have him with them. 20 But the time will come when the bridegroom will be taken from them,(Q) and on that day they will fast.
21 “No one sews a patch of unshrunk cloth on an old garment. Otherwise, the new piece will pull away from the old, making the tear worse. 22 And no one pours new wine into old wineskins. Otherwise, the wine will burst the skins, and both the wine and the wineskins will be ruined. No, they pour new wine into new wineskins.”
Jesus Is Lord of the Sabbath(R)(S)
23 One Sabbath Jesus was going through the grainfields, and as his disciples walked along, they began to pick some heads of grain.(T) 24 The Pharisees said to him, “Look, why are they doing what is unlawful on the Sabbath?”(U)
25 He answered, “Have you never read what David did when he and his companions were hungry and in need? 26 In the days of Abiathar the high priest,(V) he entered the house of God and ate the consecrated bread, which is lawful only for priests to eat.(W) And he also gave some to his companions.”(X)
27 Then he said to them, “The Sabbath was made for man,(Y) not man for the Sabbath.(Z) 28 So the Son of Man(AA) is Lord even of the Sabbath.”
Copyright © 1989 by Biblica
© 2017 Bible League International
Holy Bible, New International Version®, NIV® Copyright ©1973, 1978, 1984, 2011 by Biblica, Inc.® Used by permission. All rights reserved worldwide.
NIV Reverse Interlinear Bible: English to Hebrew and English to Greek. Copyright © 2019 by Zondervan.