Add parallel Print Page Options

Yohana Atayarisha Njia kwa Ajili ya Yesu

(Mt 3:1-12; Lk 3:1-9,15-17; Yh 1:19-28)

Mwanzo wa Habari Njema za Yesu Masihi,[a] Mwana wa Mungu,[b] zilianza kama vile Nabii Isaya alivyosema zitaanza, aliandika,

“Sikiliza! Nitamtuma mjumbe mbele yako.
    Yeye ataandaa njia kwa ajili yako.”(A)
“Kuna mtu anayeipaza sauti yake toka nyikani:
‘Tayarisheni njia kwa ajili ya Bwana;
    nyoosheni njia kwa ajili yake.’”(B)

Naye Yohana akaja, akiwabatiza watu huko nyikani huku akiwahubiri watu ujumbe kutoka kwa Mungu. Aliwaambia wabatizwe kuonesha kuwa wamekubali kubadili maisha yao ndipo dhambi zao zitasamehewa. Watu kutoka Yerusalemu na maeneo yote ya Uyahudi walikwenda kwa Yohana Mbatizaji; huko waliungama matendo yao mabaya kwake naye akawabatiza katika Mto Yordani.

Huyo Yohana alivaa mavazi yaliyofumwa kutokana na manyoya ya ngamia. Naye alijifunga mkanda wa ngozi kuzunguka kiuno chake, na alikula nzige na asali mbichi.

Yeye alitangaza yafuatayo: “Yupo mwingine ajaye baada yangu, mwenye nguvu zaidi kuliko mimi. Nami niliye mtumwa wa chini kabisa sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake.[c] Mimi nawabatiza katika maji, lakini yeye huyo atawabatiza katika Roho Mtakatifu.”

Read full chapter

Footnotes

  1. 1:1 Masihi Yaani “Kristo”, tafsiri ya Kiyunani ya neno la Kiebrania “Masihi”. Tazama Kristo na Masihi katika Orodha ya Maneno. Pia katika mstari wa 20 na katika kitabu chote hiki.
  2. 1:1 Mwana wa Mungu Nakala zingine za Kiyunani hazina maneno haya.
  3. 1:7 viatu vyake “Mimi sistahili kuwa hata kama mmoja wa watumishi wake anayeinama kumfungua kamba za viatu vyake.”

John the Baptist Prepares the Way(A)

The beginning of the good news about Jesus the Messiah,[a] the Son of God,[b](B) as it is written in Isaiah the prophet:

“I will send my messenger ahead of you,
    who will prepare your way”[c](C)
“a voice of one calling in the wilderness,
‘Prepare the way for the Lord,
    make straight paths for him.’”[d](D)

And so John the Baptist(E) appeared in the wilderness, preaching a baptism of repentance(F) for the forgiveness of sins.(G) The whole Judean countryside and all the people of Jerusalem went out to him. Confessing their sins, they were baptized by him in the Jordan River. John wore clothing made of camel’s hair, with a leather belt around his waist,(H) and he ate locusts(I) and wild honey. And this was his message: “After me comes the one more powerful than I, the straps of whose sandals I am not worthy to stoop down and untie.(J) I baptize you with[e] water, but he will baptize you with[f] the Holy Spirit.”(K)

Read full chapter

Footnotes

  1. Mark 1:1 Or Jesus Christ. Messiah (Hebrew) and Christ (Greek) both mean Anointed One.
  2. Mark 1:1 Some manuscripts do not have the Son of God.
  3. Mark 1:2 Mal. 3:1
  4. Mark 1:3 Isaiah 40:3
  5. Mark 1:8 Or in
  6. Mark 1:8 Or in