Font Size
Luka 9:46-48
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Luka 9:46-48
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Nani ni Mkuu Zaidi?
(Mt 18:1-5; Mk 9:33-37)
46 Wafuasi wa Yesu walianza kubishana wakiulizana nani ni mkuu kuliko wote miongoni mwao. 47 Yesu alijua walichokuwa wanafikiri, hivyo akamchukua mtoto mdogo na kumsimamisha karibu yake. 48 Kisha akawaambia, “Yeyote anayemkaribisha mtoto mdogo kama huyu kwa jina langu ananikaribisha mimi. Na yeyote anayenikaribisha mimi anamkaribisha yule aliyenituma. Aliye mnyenyekevu zaidi miongoni mwenu, ndiye mkuu.”
Read full chapter
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International