Font Size
Luka 18:15-17
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Luka 18:15-17
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yesu Awakaribisha Watoto
(Mt 19:13-15; Mk 10:13-16)
15 Baadhi ya watu waliwaleta hata watoto wao wadogo kwa Yesu ili awawekee mikono kuwabariki. Lakini wafuasi walipoona hili, waliwakataza. 16 Lakini Yesu aliwaalika watoto kwake na kuwaambia wafuasi wake, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu. Msiwazuie, kwa kuwa ufalme wa Mungu ni wa watu walio kama watoto wadogo hawa. 17 Ukweli ni kwamba, ni lazima uupokee ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo anavyopokea vitu, la si hivyo hautauingia.”
Read full chapter
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International