Add parallel Print Page Options

Salamu kutoka kwa Paulo, Sila na Timotheo.

Kwa kanisa la Thesalonike lililo mali ya Mungu baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.

Neema na amani viwe kwenu kutoka kwa Mungu Baba na Bwana wetu Yesu Kristo.

Kaka na dada zetu, tunamshukuru Mungu kwa ajili yenu. Na hivyo ndivyo tunavyopaswa kufanya, kwani mnatupa sababu ya kushukuru na imani yenu inakua zaidi na zaidi. Pamoja na hilo upendo ambao kila mmoja wenu anao kwa mwenzake nao unakua. Hivyo tunayaeleza makanisa mengine ya Mungu namna tunavyojivuna kuhusu ninyi. Tunawaeleza jinsi mlivyoendelea kwa subira kuwa imara na waaminifu, ingawa mnateswa na kusumbuliwa na matatizo mengi.

Read full chapter