1 Yohana 3
Neno: Bibilia Takatifu
Watoto Wa Mungu Wanavyopaswa Kuishi
3 Tazameni jinsi Baba alivyotupenda mno, hata tukaitwa watoto wa Mungu! Na hivyo ndivyo tulivyo. Watu wa ulimwengu hawatutambui kwa sababu hawakumjua Mungu. 2 Wapendwa, sisi sasa tu wana wa Mungu. Tutakavyokuwa baadaye haijulikani bado, lakini tunajua kwamba Kristo atakapotokea, tutafanana naye, kwa maana tutamwona kama alivyo.
Kujitakasa Na Kuacha Dhambi
3 Na kila mtu mwenye tumaini hili hujitakasa, kama yeye mwe nyewe alivyo mtakatifu.
4 Kila atendaye dhambi ana hatia ya kuvunja sheria; maana dhambi ni uvunjaji sheria. 5 Mnajua kwamba Kristo alikuja kuondoa dhambi naye hana dhambi yo yote. 6 Hakuna mtu anayedumu ndani ya Kristo ambaye anatenda dhambi; na mtu ye yote anayetenda dhambi, huyo hajapata kumwona Kristo wala kumjua.
7 Watoto wadogo, mtu asije akawadanganya. Kila atendaye haki ni mwenye haki, kama Kristo alivyo wa haki. 8 Kila atendaye dhambi ni wa shetani; kwa maana shetani ametenda dhambi tangu mwanzo. Mwana wa Mungu alikuja ili aziangamize kazi za shetani.
9 Mtu aliyezaliwa na Mungu haendelei na tabia ya kutenda dhambi, kwa maana ana asili ya Mungu; hawezi kuendelea kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa na Mungu.
Kutenda Haki Na Kupendana
10 Na hivi ndivyo tunavyoweza kutambua wazi kati ya walio watoto wa Mungu na walio watoto wa shetani. Mtu ye yote asiyet enda lililo haki si wa Mungu; wala asiyempenda ndugu yake si wa Mungu. 11 Na ujumbe mliosikia tangu mwanzo ndio huu: kwamba tupen dane. 12 Msiwe kama Kaini ambaye alikuwa wa yule mwovu akamwua ndugu yake. Na kwa nini alimwua? Kwa sababu matendo yake yalikuwa maovu lakini matendo ya nduguye yalikuwa ya haki.
13 Ndugu zangu, msishangae watu wa ulimwengu wakiwachukia. 14 Tunajua hakika kwamba tumevuka kutoka kwenye kifo na kuingia kwenye uzima kwa maana tunawapenda ndugu zetu. Asiye na upendo anaishi katika kifo. 15 Kila anayemchukia ndugu yake ni mwuaji, na kama mjuavyo, hakuna mwuaji ambaye ana uzima wa milele ndani yake.
16 Na tumeujua upendo kwa sababu Kristo alitoa maisha yake kwa ajili yetu. Na sisi tunapaswa kuyatoa maisha yetu kwa ajili ya ndugu zetu. 17 Lakini ikiwa mtu ana mali za hapa duniani na akamwona ndugu yake ana shida lakini akawa na moyo mgumu wala asimhurumie, mtu kama huyo anawezaje kusema anao upendo wa Mungu? 18 Wanangu, upendo wetu usiwe wa maneno matupu, bali upendo wetu udhihirishwe kwa vitendo na kweli.
19 Hivi ndivyo tutakavyoweza kuwa na hakika kwamba sisi ni wa kweli na hatutakuwa na wasiwasi mbele ya Mungu 20 hata kama dhamiri zetu zitatuhukumu; kwa maana tunajua kwamba Mungu ni mkuu kuliko dhamiri zetu, naye anajua kila kitu. 21 Wapendwa, ikiwa dhamiri zetu hazituhukumu, tuna ujasiri mbele za Mungu; 22 nasi tunapokea kutoka kwake lo lote tuombalo kwa kuwa tunatii amri zake na kufanya yampendezayo. 23 Na amri yake ndio hii: tuliamini jina la Mwanae Yesu Kristo na kupendana, kama alivyotu agiza. 24 Wote wanaozishika amri zake hukaa ndani yake na yeye ndani yao. Na hivi ndivyo tunavyojua kwamba anaishi ndani yetu: tunajua kwa njia ya yule Roho aliyetupatia.
1 John 3
King James Version
3 Behold, what manner of love the Father hath bestowed upon us, that we should be called the sons of God: therefore the world knoweth us not, because it knew him not.
2 Beloved, now are we the sons of God, and it doth not yet appear what we shall be: but we know that, when he shall appear, we shall be like him; for we shall see him as he is.
3 And every man that hath this hope in him purifieth himself, even as he is pure.
4 Whosoever committeth sin transgresseth also the law: for sin is the transgression of the law.
5 And ye know that he was manifested to take away our sins; and in him is no sin.
6 Whosoever abideth in him sinneth not: whosoever sinneth hath not seen him, neither known him.
7 Little children, let no man deceive you: he that doeth righteousness is righteous, even as he is righteous.
8 He that committeth sin is of the devil; for the devil sinneth from the beginning. For this purpose the Son of God was manifested, that he might destroy the works of the devil.
9 Whosoever is born of God doth not commit sin; for his seed remaineth in him: and he cannot sin, because he is born of God.
10 In this the children of God are manifest, and the children of the devil: whosoever doeth not righteousness is not of God, neither he that loveth not his brother.
11 For this is the message that ye heard from the beginning, that we should love one another.
12 Not as Cain, who was of that wicked one, and slew his brother. And wherefore slew he him? Because his own works were evil, and his brother's righteous.
13 Marvel not, my brethren, if the world hate you.
14 We know that we have passed from death unto life, because we love the brethren. He that loveth not his brother abideth in death.
15 Whosoever hateth his brother is a murderer: and ye know that no murderer hath eternal life abiding in him.
16 Hereby perceive we the love of God, because he laid down his life for us: and we ought to lay down our lives for the brethren.
17 But whoso hath this world's good, and seeth his brother have need, and shutteth up his bowels of compassion from him, how dwelleth the love of God in him?
18 My little children, let us not love in word, neither in tongue; but in deed and in truth.
19 And hereby we know that we are of the truth, and shall assure our hearts before him.
20 For if our heart condemn us, God is greater than our heart, and knoweth all things.
21 Beloved, if our heart condemn us not, then have we confidence toward God.
22 And whatsoever we ask, we receive of him, because we keep his commandments, and do those things that are pleasing in his sight.
23 And this is his commandment, That we should believe on the name of his Son Jesus Christ, and love one another, as he gave us commandment.
24 And he that keepeth his commandments dwelleth in him, and he in him. And hereby we know that he abideth in us, by the Spirit which he hath given us.
Copyright © 1989 by Biblica