1 Wakorintho 8
Neno: Bibilia Takatifu
Chakula Kilichotolewa Sadaka Kwa Sanamu
8 Sasa kuhusu chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu. Tuna jua kwamba ‘sisi sote tuna ujuzi.’ Lakini ‘ujuzi’ huleta maji vuno, ila upendo hujenga. 2 Mtu anayedhania kwamba anajua kitu, basi hajafahamu kama inavyompasa kujua. 3 Lakini kama mtu anam penda Mungu, mtu huyo anajulikana na Mungu.
4 Kwa hiyo basi, kuhusu kula chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu: tunajua kwamba ‘sanamu haina uhai wa kweli’ na kwamba ‘kuna Mungu mmoja tu.’ 5 Kwa maana hata kama wapo hao wanaoitwa ‘miungu,’ kama ni mbinguni au duniani; na kwa kweli wapo ‘miungu’ wengi na ‘mabwana’ wengi; 6 sisi tunajua kwamba kuna Mungu mmoja, aliye Baba, ambaye vitu vyote vinatoka kwake, na sisi tunaishi kwa ajili yake; na kuna Bwana mmoja, Yesu Kristo, ambaye vitu vyote vimekuwepo kupitia kwake na tunaishi kutokana naye.
7 Lakini si wote wanajua mambo haya. Watu wengine mpaka leo bado wamezoea miungu ya sanamu kiasi ambacho wanapokula chakula hicho wanadhani ni chakula kilichotolewa kwa sanamu, na kwa kuwa dhamiri yao ni dhaifu, inadhurika. 8 Lakini chakula hakitusaidii kuwa karibu zaidi na Mungu. Hatupotezi cho chote tusipokula, wala hatupati faida yo yote kama tukila.
9 Lakini hata hivyo tuwe waangalifu jinsi tunavyotumia uhuru wetu tusije tukawakwaza walio dhaifu katika imani. 10 Kwa maana kama mtu mwenye dhamiri dhaifu akiwaona ninyi wenye ujuzi mkila katika hekalu la sanamu, je, si atavutwa kula chakula kilichoto lewa kwa sanamu? 11 Kwa njia hiyo, huyo ndugu mwenye dhamiri dhaifu, ambaye Kristo alimfia, atateketea kwa sababu ya ujuzi wako. 12 Mnapowatenda dhambi ndugu zenu kwa njia hii na kuharibu dhamiri zao dhaifu, mnamkosea Kristo. 13 Kwa hiyo kama chakula kitamfanya ndugu yangu aanguke katika dhambi, sitakula nyama kamwe, nisije nikamfanya ndugu yangu aanguke.
1 Corinthians 8
New International Version
Concerning Food Sacrificed to Idols
8 Now about food sacrificed to idols:(A) We know that “We all possess knowledge.”(B) But knowledge puffs up while love builds up. 2 Those who think they know something(C) do not yet know as they ought to know.(D) 3 But whoever loves God is known by God.[a](E)
4 So then, about eating food sacrificed to idols:(F) We know that “An idol is nothing at all in the world”(G) and that “There is no God but one.”(H) 5 For even if there are so-called gods,(I) whether in heaven or on earth (as indeed there are many “gods” and many “lords”), 6 yet for us there is but one God,(J) the Father,(K) from whom all things came(L) and for whom we live; and there is but one Lord,(M) Jesus Christ, through whom all things came(N) and through whom we live.
7 But not everyone possesses this knowledge.(O) Some people are still so accustomed to idols that when they eat sacrificial food they think of it as having been sacrificed to a god, and since their conscience is weak,(P) it is defiled. 8 But food does not bring us near to God;(Q) we are no worse if we do not eat, and no better if we do.
9 Be careful, however, that the exercise of your rights does not become a stumbling block(R) to the weak.(S) 10 For if someone with a weak conscience sees you, with all your knowledge, eating in an idol’s temple, won’t that person be emboldened to eat what is sacrificed to idols?(T) 11 So this weak brother or sister, for whom Christ died, is destroyed(U) by your knowledge. 12 When you sin against them(V) in this way and wound their weak conscience, you sin against Christ.(W) 13 Therefore, if what I eat causes my brother or sister to fall into sin, I will never eat meat again, so that I will not cause them to fall.(X)
Footnotes
- 1 Corinthians 8:3 An early manuscript and another ancient witness think they have knowledge do not yet know as they ought to know. 3 But whoever loves truly knows.
Copyright © 1989 by Biblica
Holy Bible, New International Version®, NIV® Copyright ©1973, 1978, 1984, 2011 by Biblica, Inc.® Used by permission. All rights reserved worldwide.
NIV Reverse Interlinear Bible: English to Hebrew and English to Greek. Copyright © 2019 by Zondervan.