1 Wakorintho 5
Neno: Bibilia Takatifu
Mwasherati Atengwe
5 Kuna habari thabiti kwamba miongoni mwenu kuna uasherati unaotendeka; tena ni uasherati wa aina ambayo hata watu wasiomjua Mungu hawafanyi. Nimesikia kwamba kuna mtu anazini na mama yake wa kambo! 2 Mnawezaje basi kujivuna! Badala yake mngepaswa kuom boleza. Huyo aliyefanya tendo hili afukuzwe na kutengwa nanyi. 3 Japokuwa sipo nanyi katika mwili, lakini nipo nanyi katika roho. Na nimekwisha toa hukumu kuhusu huyo mtu aliyetenda jambo hili, kama vile ningekuwapo. 4 Mnapokutana katika jina la Bwana wetu Yesu nami nikiwepo katika roho, na nguvu ya Bwana wetu Yesu ikiwepo, 5 mtoeni mtu huyu kwa shetani, ili asili yake ya dhambi iangamizwe lakini roho yake iokolewe siku ile ya Bwana.
6 Kiburi chenu hakifai. Hamjui kwamba hamira kidogo tu huumua donge lote la unga? 7 Ondoeni chachu ya zamani ili mpate kuwa donge lisilo na chachu, kama mnavyotakiwa kuwa. Kwa maana Kristo ambaye ndiye Mwana-kondoo wetu wa Pasaka amekwisha tolewa kama dhabihu. 8 Kwa hiyo, tusherehekee sikukuu hii, sio kwa chachu ya zamani, chachu ya nia mbaya na uovu bali kwa mkate usiotiwa hamira, wa moyo safi na kweli.
9 Niliwaandikia katika barua yangu kuwa msishirikiane na waasherati. 10 Sikuwa na maana kwamba msishirikiane na watu wa dunia walio waasherati, au wenye tamaa mbaya, wanyang’anyi au waabudu sanamu. Kufanya hivyo ingewabidi mtoke duniani. 11 Lakini nilikuwa namaanisha kwamba msishirikiane na mtu ye yote anayejiita ndugu lakini ni mwasherati, mwenye tamaa mbaya, mwabudu sanamu, mtukanaji, mlevi na laghai. Wala msile na mtu kama huyo.
12 Si kazi yangu kuhukumu watu walio nje ya kanisa. Je, si hao walio ndani ya kanisa mnaopaswa kuwahukumu? 13 Mungu anawa hukumu walio nje ya kanisa. “Mfukuzeni mtu mwovu atoke kutoka katika ushirika wenu.”
1 Corinthians 5
New Living Translation
Paul Condemns Spiritual Pride
5 I can hardly believe the report about the sexual immorality going on among you—something that even pagans don’t do. I am told that a man in your church is living in sin with his stepmother.[a] 2 You are so proud of yourselves, but you should be mourning in sorrow and shame. And you should remove this man from your fellowship.
3 Even though I am not with you in person, I am with you in the Spirit.[b] And as though I were there, I have already passed judgment on this man 4 in the name of the Lord Jesus. You must call a meeting of the church.[c] I will be present with you in spirit, and so will the power of our Lord Jesus. 5 Then you must throw this man out and hand him over to Satan so that his sinful nature will be destroyed[d] and he himself[e] will be saved on the day the Lord[f] returns.
6 Your boasting about this is terrible. Don’t you realize that this sin is like a little yeast that spreads through the whole batch of dough? 7 Get rid of the old “yeast” by removing this wicked person from among you. Then you will be like a fresh batch of dough made without yeast, which is what you really are. Christ, our Passover Lamb, has been sacrificed for us.[g] 8 So let us celebrate the festival, not with the old bread[h] of wickedness and evil, but with the new bread[i] of sincerity and truth.
9 When I wrote to you before, I told you not to associate with people who indulge in sexual sin. 10 But I wasn’t talking about unbelievers who indulge in sexual sin, or are greedy, or cheat people, or worship idols. You would have to leave this world to avoid people like that. 11 I meant that you are not to associate with anyone who claims to be a believer[j] yet indulges in sexual sin, or is greedy, or worships idols, or is abusive, or is a drunkard, or cheats people. Don’t even eat with such people.
12 It isn’t my responsibility to judge outsiders, but it certainly is your responsibility to judge those inside the church who are sinning. 13 God will judge those on the outside; but as the Scriptures say, “You must remove the evil person from among you.”[k]
Footnotes
- 5:1 Greek his father’s wife.
- 5:3 Or in spirit.
- 5:4 Or In the name of the Lord Jesus, you must call a meeting of the church.
- 5:5a Or so that his body will be destroyed; Greek reads for the destruction of the flesh.
- 5:5b Greek and the spirit.
- 5:5c Other manuscripts read the Lord Jesus; still others read our Lord Jesus Christ.
- 5:7 Greek has been sacrificed.
- 5:8a Greek not with old leaven.
- 5:8b Greek but with unleavened [bread].
- 5:11 Greek a brother.
- 5:13 Deut 17:7.
Copyright © 1989 by Biblica
Holy Bible, New Living Translation, copyright © 1996, 2004, 2015 by Tyndale House Foundation. Used by permission of Tyndale House Publishers, Inc., Carol Stream, Illinois 60188. All rights reserved.