Kutoka kwa Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na ya Kristo Yesu aliye tumaini letu. Kwa

Walimu Wa Uongo

Kama nilivyokusihi wakati nikienda Makedonia, napenda ukae hapo Efeso uwaamuru watu fulani wasiendelee kufundisha mafund isho ya uongo. Pia wasiendelee kupoteza wakati wao kwa hadithi na orodha ndefu zisizo na mwisho za majina ya vizazi ambazo huchochea mabishano badala ya kuwajenga katika maarifa ya kimungu yatokanayo na imani. Shabaha ya maagizo haya ni upendo utokao katika moyo safi, dhamiri njema na imani ya kweli. Watu wengine wamepotoka na kuingia katika majadiliano yasiyo na maana kwa kuwa hawakuzingatia mambo haya. Wanataka kuwa walimu wa sheria ingawa hawaelewi mambo wanayosema wala hayo wanayotilia mkazo.

Tunajua kwamba sheria ni njema iwapo inatumika ipasavyo. Lakini tuelewe kwamba sheria haikuwekwa kwa ajili ya wenye haki, bali kwa ajili ya waasi na wasiotii: wasiomcha Mungu na wenye dhambi; wale wasio watakatifu, walio wachafu; wale wanaow aua baba zao na mama zao; wale wanaoua binadamu; 10 wale wal iowazinzi, wafiraji; wale wanaoteka watu nyara, na waongo, na wanaoapa kwa uwongo; na mengine mengi ambayo ni kinyume cha mafundisho ya kweli, 11 ambayo yanaambatana na Injili tukufu ya Mungu Mbarikiwa, ambayo nimekabidhiwa. 12 Nami namshukuru Kristo Yesu Bwana wetu, aliyenitia nguvu na kunihesabu kuwa ni mwaminifu kwa kunichagua nimtumikie. 13 Ingawa hapo mwanzo nilimkufuru na kumtesa na kumtukana, nili hurumiwa kwa sababu nilitenda hayo katika ujinga wangu na kutoku amini kwangu. 14 Na neema ya Bwana wetu ilimiminika tele kwa ajili yangu pamoja na imani na upendo uliomo ndani ya Kristo Yesu. 15 Neno hili ni la hakika tena linastahili kukubalika kabisa, kwamba Kristo Yesu alikuja duniani kuokoa wenye dhambi, ambao kati yao, mimi ni mwenye dhambi kuliko wote. 16 Lakini nilihurumiwa kwa sababu hii kwamba, kwa kunitumia mimi niliyekuwa mwenye dhambi kuliko wote, Kristo aonyeshe uvumilivu wake, niwe mfano kwa wote watakaomwamini na kupata uzima wa milele. 17 Basi, heshima na utukufu ni wake yeye Mfalme wa milele, asi yekufa wala asiyeonekana, aliye peke yake Mungu, milele na milele. Amina.

18 Mwanangu Timotheo, ninakukabidhi agizo hili, kufuatana na maneno ya unabii yaliyosemwa juu yako, ili kwa kuyafuata uweze kupigana ile vita njema, 19 ukishikilia imani na dhamiri njema. Watu wengine, kwa kukataa kuisikiliza dhamiri yao, wameangamiza imani yao. 20 Miongoni mwa watu hao wamo Himenayo na Aleksanda ambao nimewakabidhi kwa shetani, ili wajifunze wasimtukane Mungu.

Salamu kutoka kwa Paulo, mtume wa Kristo Yesu.[a] Mimi ni mtume kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na Kristo Yesu atupaye tumaini.

Ninakuandikia wewe, Timotheo. Wewe ni kama mwanangu halisi kwa sababu ya imani yetu.

Neema, rehema na amani kutoka kwa Mungu Baba na Kristo Yesu Bwana wetu ziwe pamoja nawe.

Maonyo kuhusu Mafundisho ya Uongo

Nilipokwenda Makedonia, nilikuomba ubaki Efeso. Baadhi ya watu huko wanafundisha mambo yasiyo ya kweli, nami ninataka uwaonye waache. Uwaambie wasitumie muda wao kusimulia simulizi zisizo na maana za mambo ya kale na kutengeneza orodha ndefu ya mababu. Mambo hayo husababisha mabishano tu na hayaisaidii katika kuikamilisha kazi ya Mungu tuliyopewa, ambayo ni lazima tuikamilishe kwa imani. Kusudi langu la kukueleza ufanye jambo hili ni kutaka kukuza upendo; aina ya upendo unaooneshwa na wale ambao mawazo yao ni safi; watu ambao hufanya yale wanayojua kuwa ni sahihi na ambao imani yao kwa Mungu ni ya kweli. Lakini wengine wamekosa jambo hili la msingi katika mafundisho yao na wamepoteza mwelekeo. Sasa wanazungumza juu ya mambo yasiyo na msaada kwa mtu yeyote. Wanataka kuwa walimu wa sheria,[b] lakini hawafahamu mambo wanayosema, wanasema kwa ujasiri wote juu ya mambo wasiyoyaelewa wenyewe.

Tunajua kwamba sheria ni nzuri ikiwa mtu anaitumia kwa usahihi. Pia tunajua kwamba sheria haikutengenezwa kwa ajili ya wale wanaotenda haki. Imetengenezwa kwa ajili ya wale wanayoipinga na kukataa kuifuata. Sheria ipo kwa ajili ya wenye dhambi wanaompinga Mungu na mambo yote yanayompendeza. Ipo kwa ajili ya wale wasio na hamu ya mambo ya kiroho na kwa ajili ya wale wanaowaua baba au mama zao au mtu yeyote yule. 10 Ipo kwa ajili ya watu wanaotenda dhambi ya uasherati, kwa wanaume wanaolala na wanaume wenzao au wavulana, kwa wote wanaoteka watu na kuwauza kama watumwa, kwa wote wanaodanganya au wale wasiosema ukweli wakiwa katika kiapo, na kwa ajili ya wale walio kinyume na mafundisho ya kweli ya Mungu. 11 Mafundisho hayo ni sehemu ya Habari Njema ambayo Mungu wetu wa utukufu alinipa kuhubiri na ndani yake tunauona utukufu wake.

Shukrani kwa Rehema za Mungu

12 Ninamshukuru Kristo Yesu Bwana wetu kwa sababu aliniamini na kunipa kazi hii ya kumtumikia. Yeye hunitia nguvu ya kufanya kazi hii. 13 Hapo zamani nilimtukana Kristo. Nikiwa mtu mwenye majivuno na mkorofi, niliwatesa watu wake. Lakini Mungu alinihurumia kwa sababu sikujua nilichokuwa nafanya. Nilifanya hayo kabla sijaamini. 14 Lakini Bwana wetu alinipa kiwango kikubwa cha neema yake. Na pamoja na neema hiyo imani na upendo ulio katika Kristo Yesu vilifuata.

15 Huu ndiyo usemi wa kweli unaopaswa kukubaliwa pasipo kuuliza maswali; kwamba Kristo Yesu alikuja ulimwenguni kuokoa wenye dhambi, nami ni mbaya zaidi ya wote. 16 Lakini nilipata rehema kwa sababu ili Kristo Yesu aweze kunitumia, mimi mtenda dhambi kuliko wote, ili kuonesha uvumilivu wake usio na kikomo. Alitaka niwe mfano kwa wale ambao wangemwamini na kupata uzima wa milele. 17 Heshima na utukufu kwa mfalme anayetawala milele. Hawezi kuharibiwa wala kuonekana. Heshima na utukufu apewe Mungu wa pekee milele na milele, Amina.

18 Timotheo wewe ni mwanangu mwenyewe kwa sababu ya ushirika wetu wa imani ya kweli. Ninayokuambia kuyatenda yanakubaliana na unabii[c] ambao ulisemwa juu yako hapo zamani. Nataka uukumbuke unabii huo na kupigana vita vizuri vya imani. 19 Endelea kumwamini Mungu na kutenda yale unayojua kuwa ni sahihi. Watu wengine hawajatenda haya, na imani yao sasa imeharibiwa. 20 Himenayo na Iskanda ni mfano wa watu hao. Nimewakabidhi kwa Shetani ili wafundishwe kutosema kinyume cha Mungu.

Footnotes

  1. 1:1 Kristo Yesu Au “Mfalme Yesu”. Neno “Kristo” ni tafsiri ya Kiyunani ya neno la Kiebrania “Masihi”, ambao ni wadhifa wa kifalme. Tazama Mk 15:32: Lk 23:2. Tazama pia Kristo na Masihi katika Orodha ya Maneno.
  2. 1:7 sheria “Sheria” pengine ni “sheria ya Mungu” ambayo Mungu alimpa Musa kwa ajili ya watu wake. Tazama Sheria katika Orodha ya Maneno. Pia katika mstari wa 8.
  3. 1:18 unabii “Unabii” ina maana mambo ambayo manabii waliyasema juu ya maisha ya Timotheo kabla ya yote kutokea.

Greeting

Paul, an apostle of Jesus Christ, by the commandment of God our Savior and the Lord Jesus Christ, our hope,

To Timothy, a (A)true son in the faith:

(B)Grace, mercy, and peace from God our Father and Jesus Christ our Lord.

No Other Doctrine

As I urged you (C)when I went into Macedonia—remain in Ephesus that you may [a]charge some (D)that they teach no other doctrine, (E)nor give heed to fables and endless genealogies, which cause disputes rather than godly edification which is in faith. Now (F)the purpose of the commandment is love (G)from a pure heart, from a good conscience, and from [b]sincere faith, from which some, having strayed, have turned aside to (H)idle talk, desiring to be teachers of the law, understanding neither what they say nor the things which they affirm.

But we know that the law is (I)good if one uses it lawfully, knowing this: that the law is not made for a righteous person, but for the lawless and insubordinate, for the ungodly and for sinners, for the unholy and profane, for murderers of fathers and murderers of mothers, for manslayers, 10 for fornicators, for sodomites, for kidnappers, for liars, for perjurers, and if there is any other thing that is [c]contrary to sound doctrine, 11 according to the glorious gospel of the (J)blessed God which was (K)committed to my trust.

Glory to God for His Grace(L)

12 And I thank Christ Jesus our Lord who has (M)enabled me, (N)because He counted me faithful, (O)putting me into the ministry, 13 although (P)I was formerly a blasphemer, a persecutor, and an [d]insolent man; but I obtained mercy because (Q)I did it ignorantly in unbelief. 14 (R)And the grace of our Lord was exceedingly abundant, (S)with faith and love which are in Christ Jesus. 15 (T)This is a faithful saying and worthy of all acceptance, that (U)Christ Jesus came into the world to save sinners, of whom I am chief. 16 However, for this reason I obtained mercy, that in me first Jesus Christ might show all longsuffering, as a pattern to those who are going to believe on Him for everlasting life. 17 Now to (V)the King eternal, (W)immortal, (X)invisible, to [e]God (Y)who alone is wise, (Z)be honor and glory forever and ever. Amen.

Fight the Good Fight

18 This [f]charge I commit to you, son Timothy, according to the prophecies previously made concerning you, that by them you may wage the good warfare, 19 having faith and a good conscience, which some having rejected, concerning the faith have suffered shipwreck, 20 of whom are (AA)Hymenaeus and (AB)Alexander, whom I delivered to Satan that they may learn not to (AC)blaspheme.

Footnotes

  1. 1 Timothy 1:3 command
  2. 1 Timothy 1:5 Lit. unhypocritical
  3. 1 Timothy 1:10 opposed
  4. 1 Timothy 1:13 violently arrogant
  5. 1 Timothy 1:17 NU the only God,
  6. 1 Timothy 1:18 command