1 Petro 1
Neno: Bibilia Takatifu
1 Kutoka kwa Petro, mtume wa Yesu Kristo. Kwa wateule wa Mungu ambao wametawanyika, wanaoishi ugenini huko Ponto, Galatia, Kapadokia, Asia na Bithinia. 2 Ninyi mlichaguliwa tangu mwanzo na Mungu Baba na kutakaswa na Roho, mpate kumtii Yesu Kristo na kunyunyiziwa damu yake. Nawatakieni neema na amani tele.
Tumaini Lenye Uzima
3 Asifiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa rehema yake kuu ametufanya tuzaliwe upya ili tupate tumaini lenye uzima kwa kufufuka kwa Bwana wetu Yesu Kristo kutoka kwa wafu; 4 na tupokee urithi usioharibika, usiooza na usiochuja, ambao umewekwa mbinguni kwa ajili yenu. 5 Nanyi, kwa imani, mnalindwa na nguvu ya Mungu mpaka utakapofika wokovu ambao uko tayari kufunuliwa wakati wa mwisho.
6 Furahini sana katika hilo, ingawa sasa kwa kitambo kidogo ni lazima mpate majaribu ya kila aina. 7 Majaribu yataifanya imani yenu, ambayo ina thamani kuliko dhahabu, iwe imepimwa na kuthibitishwa kuwa ya kweli kama vile dhahabu ambayo ingawa ni kitu kiharibikacho, hupimwa kwa moto. Ndipo mtapata sifa, utukufu na heshima siku ile Yesu Kristo atakapofunuliwa. 8 Ingawa hamja pata kumwona, mnampenda. Na ingawa hamumwoni sasa mnamwamini na kujawa na furaha tukufu isiyoelezeka. 9 Maana mnapokea wokovu wa roho zenu, ambao ndio lengo la imani yenu.
10 Manabii waliotabiri kuhusu neema hiyo ambayo ninyi mnge pewa, walitafuta sana na kwa makini habari za wokovu huu. 11 Walijaribu kutafuta kujua ni nani au ni wakati upi uliomaan ishwa na Roho wa Kristo aliyekuwa akisema ndani yao alipotabiri kuhusu mateso ya Kristo na utukufu utakaofuata. 12 Walidhihir ishiwa kuwa kazi waliyokuwa wakifanya si kwa faida yao bali ni kwa ajili yenu. Kwa maana walinena nanyi habari za mambo ambayo sasa mmekwisha elezwa na wale waliowahubiria Injili kwa uwezo wa Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni. Hata malaika wanata mani kufahamu mambo haya.
Mwito Wa Kuishi Maisha Matakatifu
13 Kwa hiyo, ziandaeni nia zenu, muwe na kiasi, wekeni tumaini lenu lote katika neema ile mtakayopewa wakati ule Yesu Kristo atakapodhihirishwa. 14 Kama watoto watiifu, msikubali kutawaliwa na tamaa mbaya mlizokuwa nazo wakati mkiishi katika ujinga. 15 Bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, kadhalika ninyi muwe watakatifu katika mwenendo wenu; 16 maana imeandikwa: “Muwe watakatifu kwa sababu mimi ni mtakatifu.”
17 Kwa kuwa mnamwita “Baba” yeye ahukumuye matendo ya kila mtu pasipo upendeleo, ishini maisha yenu hapa duniani kama wageni, kwa kumcha Mungu. 18 Maana mnafahamu kwamba mlikombolewa kutokana na maisha duni yasiyofaa ambayo mlirithi kutoka kwa baba zenu. Hamkukombolewa kwa kutumia vitu viharibikavyo kama fedha na dhahabu, 19 bali mlikombolewa kwa damu ya thamani ya Kristo, Mwana-Kondoo asiye na dosari wala doa. 20 Yeye alichaguliwa kabla ya dunia kuumbwa lakini akadhihirishwa katika siku hizi za mwisho kwa ajili yenu. 21 Kwa ajili yake ninyi mnamwamini Mungu aliyemfufua kutoka kwa wafu akampa utukufu, na kwa hiyo imani yenu na matumaini yenu yako kwa Mungu.
22 Na sasa kwa kuwa mmekwisha kujitakasa kwa kuitii ile kweli na kuwapenda ndugu zenu kwa kweli, pendaneni kwa moyo wote. 23 Maana mmezaliwa upya, si kwa mbegu iharibikayo, bali kwa mbegu isiyoharibika, kwa neno la Mungu lililo hai na linalodumu hata milele. 24 Maana, “Binadamu wote ni kama nyasi na utukufu wao ni kama ua la mwituni. Nyasi hunyauka na ua huanguka, 25 lakini neno la Mungu hudumu milele.” Na neno hilo ni Habari Njema ambayo mlihubiriwa.
1 Peter 1
King James Version
1 Peter, an apostle of Jesus Christ, to the strangers scattered throughout Pontus, Galatia, Cappadocia, Asia, and Bithynia,
2 Elect according to the foreknowledge of God the Father, through sanctification of the Spirit, unto obedience and sprinkling of the blood of Jesus Christ: Grace unto you, and peace, be multiplied.
3 Blessed be the God and Father of our Lord Jesus Christ, which according to his abundant mercy hath begotten us again unto a lively hope by the resurrection of Jesus Christ from the dead,
4 To an inheritance incorruptible, and undefiled, and that fadeth not away, reserved in heaven for you,
5 Who are kept by the power of God through faith unto salvation ready to be revealed in the last time.
6 Wherein ye greatly rejoice, though now for a season, if need be, ye are in heaviness through manifold temptations:
7 That the trial of your faith, being much more precious than of gold that perisheth, though it be tried with fire, might be found unto praise and honour and glory at the appearing of Jesus Christ:
8 Whom having not seen, ye love; in whom, though now ye see him not, yet believing, ye rejoice with joy unspeakable and full of glory:
9 Receiving the end of your faith, even the salvation of your souls.
10 Of which salvation the prophets have enquired and searched diligently, who prophesied of the grace that should come unto you:
11 Searching what, or what manner of time the Spirit of Christ which was in them did signify, when it testified beforehand the sufferings of Christ, and the glory that should follow.
12 Unto whom it was revealed, that not unto themselves, but unto us they did minister the things, which are now reported unto you by them that have preached the gospel unto you with the Holy Ghost sent down from heaven; which things the angels desire to look into.
13 Wherefore gird up the loins of your mind, be sober, and hope to the end for the grace that is to be brought unto you at the revelation of Jesus Christ;
14 As obedient children, not fashioning yourselves according to the former lusts in your ignorance:
15 But as he which hath called you is holy, so be ye holy in all manner of conversation;
16 Because it is written, Be ye holy; for I am holy.
17 And if ye call on the Father, who without respect of persons judgeth according to every man's work, pass the time of your sojourning here in fear:
18 Forasmuch as ye know that ye were not redeemed with corruptible things, as silver and gold, from your vain conversation received by tradition from your fathers;
19 But with the precious blood of Christ, as of a lamb without blemish and without spot:
20 Who verily was foreordained before the foundation of the world, but was manifest in these last times for you,
21 Who by him do believe in God, that raised him up from the dead, and gave him glory; that your faith and hope might be in God.
22 Seeing ye have purified your souls in obeying the truth through the Spirit unto unfeigned love of the brethren, see that ye love one another with a pure heart fervently:
23 Being born again, not of corruptible seed, but of incorruptible, by the word of God, which liveth and abideth for ever.
24 For all flesh is as grass, and all the glory of man as the flower of grass. The grass withereth, and the flower thereof falleth away:
25 But the word of the Lord endureth for ever. And this is the word which by the gospel is preached unto you.
Copyright © 1989 by Biblica