15 Kulipopambazuka, makuhani wakuu walifanya mkutano pamoja na wazee na walimu wa sheria, na Baraza zima likafanya mashauri. Wakamfunga Yesu, wakamchukua na kumkabidhi kwa Pilato. Pilato akamwuliza, “Wewe ndiye Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe ndiye uliyesema maneno hayo.” Makuhani wakuu wakamsh taki kwa mambo mengi. Pilato akamwuliza tena, “Huna la kujibu?

Unasikia mashtaka yao!”

Yesu hakusema neno. Pilato akashangaa.

Yesu Ahukumiwa Kifo

Ilikuwa desturi wakati wa sherehe za Pasaka kumfungulia mfungwa ye yote ambaye watu walimtaka . Wakati huo, mtu mmoja aitwaye Baraba alikuwa amefungwa gerezani pamoja na wahalifu wen gine kwa makosa ya kusababisha uasi ambapo mauaji yalitokea. Basi watu waliokusanyika walimjia Pilato wakamwomba awafanyie kama ilivyokuwa desturi wakati wa Pasaka. Pilato akawauliza, “Mnataka nimfungue huyu mfalme wa Wayahudi?” 10 Alikuwa ana fahamu kwamba wakuu wa makuhani walikuwa wanamwonea Yesu wivu ndio sababu wakamshtaki kwake. 11 Lakini makuhani wakuu wakawa chochea watu wamwombe awafungulie Baraba.

12 Pilato akawauliza tena watu, “Nimfanye nini huyu mtu mnayemwita mfalme wa Wayahudi?” 13 Wakapiga kelele, “Msulub ishe!” 14 Akawauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakapiga kelele kwa nguvu zaidi, “Msulubishe!”

15 Pilato alitaka kuwaridhisha watu, kwa hiyo akamfungulia Baraba; na baada ya kuamuru Yesu apigwe mijeledi, akamtoa asulub ishwe.

Maaskari Wamdhihaki Yesu

16 Maaskari wakampeleka Yesu hadi kwenye ukumbi wa ndani ya Ikulu iliyoitwa Praitoria, wakakusanya kikosi kizima cha askari. 17 Wakamvika Yesu vazi la zambarau, wakatengeneza taji ya miiba, wakamvika. 18 Wakaanza kumsalimu kwa dhihaka, “Salamu, Mfalme wa Wayahudi!” 19 Wakampiga kwa fimbo kichwani, wakamte mea mate. Wakamdhihaki kwa kupiga magoti kama vile wanamheshimu mfalme. 20 Walipokwisha kumdhihaki, walimvua lile vazi la zam barau, wakamvika nguo zake. Kisha wakamtoa nje wakamsulubishe.

Yesu Asulubishwa

21 Walipokuwa wakienda kumsulubisha, njiani walikutana na mtu mmoja aitwaye Simoni, raia wa Kirene. Yeye alikuwa baba yao Aleksanda na Rufas. Alikuwa anakuja mjini kutoka shamba. Wakamla zimisha abebe msalaba wa Yesu. 22 Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgota, -yaani Mahali pa Fuvu la Kichwa.

23 Wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini akaikataa. 24 Basi wakamsulubisha, wakagawana nguo zake kwa kuzipigia kura kuamua kila mtu achukue nini.

25 Ilikuwa yapata saa tatu asubuhi walipomsulubisha. 26 Tangazo la mashtaka yake liliandikwa maneno haya: “MFALME WA WAYAHUDI.” 27 Majambazi wawili walisulubiwa pamoja naye, mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wa kushoto. [ 28 Na kwa njia hii yale Maandiko yasemayo, “Alihesabiwa pamoja na wenye hatia,” yalitimia.] 29 Watu waliokuwa wakipita, walimtukana na kutikisa vichwa vyao kwa mzaha wakasema, “Si ulikuwa ukisema kwamba unaweza kulivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu? 30 Shuka msalabani basi, ujiokoe mwenyewe!” 31 Hali kadhalika makuhani wakuu na walimu wa sheria walimdhihaki wakisema, “Ali waokoa wengine lakini anashindwa kujiokoa mwenyewe. 32 Kristo mfalme wa Wayahudi ashuke basi msalabani ili tupate kuona na kuamini!” Na wale waliosulubiwa pamoja naye pia walimtukana.

Kifo Cha Yesu Msalabani

33 Ilipofika saa sita, giza lilikumba nchi nzima kwa muda wa saa tatu. 34 Ilipofika saa tisa, Yesu akalia kwa sauti kuu “Eloi, Eloi lama Sabaktani?” Yaani, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?” 35 Baadhi ya watu waliokuwa wanasimama karibu waliposikia maneno hayo, walisema, “Mnamsikia? Anamwita

Eliya!”

36 Mtu mmoja akaenda mbio, akachovya sponji kwenye divai na siki, akaiweka kwenye ufito akamwinulia Yesu ili anywe huku akisema, “Hebu tuone kama Eliya atakuja kumshusha kutoka msala bani!”

37 Yesu akatoa sauti kuu, akakata roho. 38 Pazia la hekalu likapasuka vipande viwili kuanzia juu hadi chini.

39 Yule askari aliyekuwa amesimama mbele ya msalaba alipoona jinsi alivyokata roho, akasema, “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”

40 Walikuwapo pia wanawake walio kuwa wakiangalia mambo haya kwa mbali. Kati yao walikuwapo Mariamu Magdalena, na Mariamu mama yao Yakobo mdogo na Yose, na pia Salome . 41 Hawa walifuatana na Yesu alipokuwa Galilaya na kumhudumia. Pia walikuwapo wanawake wengine wengi waliokuwa wamekuja naye Yerusalemu.

Mazishi Ya Yesu

42 Ilipofika jioni, kwa kuwa ilikuwa siku ya Maandalizi, siku moja kabla ya Pasaka, 43 Yusufu wa Arimathea alijikaza akamwendea Pilato akamwomba auchukue mwili wa Yesu. Yeye alikuwa ni mjumbe wa Baraza aliyeheshimika, ambaye alikuwa anatazamia kuja kwa Ufalme wa Mungu. 44 Pilato alishangaa kusikia kwamba Yesu amekwisha kufa. Kwa hiyo akamwita askari amhakikishie kuwa kweli amekufa. 45 Baada ya kuhakikishiwa na yule askari kwamba kweli amekufa, Pilato alimpa Yusufu ruhusa ya kuuchukua mwili wa Yesu. 46 Basi Yusufu alinunua sanda ya kitani, akautoa mwili wa Yesu msalabani; akamzungushia sanda, akamweka ndani ya kaburi lililochongwa kwenye mwamba. Kisha akaviringisha jiwe akaufunika mlango wa kaburi. 47 Mariamu Magdalena na Mariamu mama wa Yose walipaona mahali alipozikwa Yesu.

彼拉多审问耶稣

15 第二天一大早,祭司长、年长的犹太首领和律法师们以及全议会的人们定好了对付耶稣的计划。他们叫人把耶稣绑起来,押到彼拉多那里去。

彼拉多审问耶稣。他问∶“你是犹太人的王吗?”

耶稣回答说∶“你说的对。”

祭司长们列举了耶稣的许多罪状。 彼拉多又问道∶“难道你什么也不说吗?你看,他们控告你这么多事情!”

但是耶稣仍旧沉默,这让彼拉多感到十分惊讶。

彼拉多想放却放不了耶稣

每逢逾越节期间,按照惯例,总督都会按众人的要求,释放一名囚犯。 有个叫巴拉巴的人正和叛乱的同伙们一起关在牢里,这些人在叛乱中杀过人。 人们来请求彼拉多,请他像以往一样释放囚犯。

彼拉多问他们∶“你们是要我释放犹太人之王吗?” 10 他这样问,是因为他知道祭司长们把耶稣交给他是出于嫉妒。 11 可是祭司长们煽动人们,让他们请求释放巴拉巴。

12 彼拉多又问道∶“但是,我该怎样处置你们称为犹太王的那个人呢?”

13 人们大声喊道∶“把他钉死在十字架上。”

14 彼拉多说∶“为什么呢?他犯了什么罪?”

可是人们叫喊得更响了∶“把他钉死在十字架上!”

15 彼拉多为了取悦众人,释放了巴拉巴。他下令鞭打耶稣,然后叫士兵把他钉死在十字架上。

16 士兵们把耶稣带到总督的府邸,然后集合起全营的士兵。 17 他们给耶稣披了件紫袍子,又用荆棘编了个王冠戴在他头上。 18 然后向耶稣敬礼,嘴里喊着∶“我们向您敬礼,犹太王!” 19 他们不停地用棍子打耶稣的头,朝他吐唾沫,还跪在地上给他磕头,假装把他当王来荣耀他。 20 他们戏弄完了耶稣,就把紫袍子从他身上剥下来,给他穿上他自己的衣服,然后他们才把耶稣带出来,准备将他钉在十字架上。

耶稣被钉在十字架上

21 这些士兵带着耶稣走到半路时,遇见了一个刚从乡下来的古利奈人,他名叫西门,是亚力山大和鲁孚的父亲,士兵们强迫他背着耶稣的十字架。 22 他们把耶稣带到一个叫各各他 [a]的地方。 23 士兵们把掺了没药 [b]的酒拿给耶稣,可耶稣不肯喝。 24 他们把耶稣钉在了十字架上,又用掷骰子的方式瓜分了耶稣的衣服。

25 上午九点钟时,耶稣被钉在十字架上。 26 一个牌子上写着耶稣的罪名,上面有“犹太人之王”几个字。 27 他们还把两个强盗也钉在耶稣旁边的十字架上,一个在左边,另一个在右边。

28  [c] 29 过路的人也辱骂耶稣,摇着头说∶“哈,你就是那个要毁大殿并在三天之内重建的人。 30 救救你自己吧,从十字架上下来吧!”

31 祭司长和律法师们也在那里同样地戏弄耶稣。他们彼此说∶“他拯救了别人,却救不了自己! 32 如果他真正是基督、以色列王,他就该从十字架上下来救救他自己,让我们亲眼看看,也好相信他呀。”和耶稣一起被钉在十字架上的强盗也侮辱他。

耶稣之死

33 从中午一直到下午三点,遍地都陷入了黑暗之中。 34 三点钟时,耶稣大声呼喊∶“以罗伊、以罗伊 [d]、拉马撒巴各大尼。”意思是“我的上帝!我的上帝!您为什么抛弃了我?” [e]

35 站在那里的一些人听见了,便说∶“听啊,他在呼喊以利亚 [f]呢!”

36 在场的一个人跑去找来一块海绵,蘸了些酸酒,然后把它绑在棍子上,伸到耶稣嘴边,让他喝。他说∶“等一等,让咱们看看以利亚会不会来,把他从十字架上解救下来。”

37 耶稣一声大喊,就死去了。

38 与此同时,大殿里的帘幕从上到下一裂两半。 39 那个罗马军官 [g]站在十字架前目睹了所发生的这一切,就说道∶“这人真的是上帝之子啊!”

40 一些女子站在远处观望,她们当中有马利亚抹大拉,雅各和约西的母亲马利亚(雅各是她的小儿子),还有撒罗米。 41 耶稣在加利利的时候,这几个人就都跟着他并且照顾过他。还有其他许多和他一起到耶路撒冷来的女子也站在远处观望。

埋葬耶稣

42 此时是晚上了,这天是预备日(也就是安息日的前一天), 43 亚利马太的约瑟来了。他在犹太议会里是一个很受尊敬的人物,同时也在等待着上帝的王国的降临。约瑟大胆地去找彼拉多,向他要耶稣的尸体。 44 彼拉多听说耶稣这么快就死了,不禁吃了一惊。他把那军官叫来,问他耶稣是不是已死了。 45 彼拉多听了军官的报告,就把耶稣的尸体交给约瑟。 46 约瑟买了些亚麻布,把耶稣从十字架上取下,用亚麻布裹好,放进用岩石凿成的墓穴里,然后滚过一块石头挡住墓门。 47 抹大拉的马利亚和约瑟的母亲马利亚都看清了安放耶稣的地方。

Footnotes

  1. 馬 可 福 音 15:22 各各它: 即“骷髅之地”。
  2. 馬 可 福 音 15:23 没药: 曾被用作镇痛药。
  3. 馬 可 福 音 15:28 有些希腊文版本增有第28节∶“经上写着∶‘他是和犯人们押在一起的!’这话也应验了。”
  4. 馬 可 福 音 15:34 以罗伊: 为我的上帝,人们听起来像是以利亚的名字。
  5. 馬 可 福 音 15:34 参见《诗篇》22:1。
  6. 馬 可 福 音 15:35 以利亚: 公元前850年的一位先知。
  7. 馬 可 福 音 15:39 罗马军官: 古罗马军队中的百人队长。