罗马书 6
Chinese Contemporary Bible (Simplified)
与基督同死同活
6 那么,我们该怎么说呢?我们可以继续犯罪,使恩典显得更丰富吗? 2 绝不可以!我们既然向罪死了,岂可继续活在罪中? 3 难道你们不知道,我们受洗归属基督耶稣是和祂一同死吗? 4 我们借着洗礼和祂一同死了,埋葬了,这样我们的一举一动可以有新生命的样式,正如基督借着父的荣耀从死里复活一样。
5 如果我们和基督一同死了,也必和祂一同复活。 6 我们知道,我们的旧人已经和祂一同钉在十字架上,使辖制我们身体的罪失去力量,使我们不再做罪的奴隶。 7 因为人一旦死了,便脱离了罪。
8 如果我们与基督同死,相信也必与祂同活。 9 因为我们知道,基督既然从死里复活了,就不会再死,死亡也不能再控制祂。 10 祂死,是向罪死,只死一次;祂活,却是向上帝永远活着。 11 这样,你们应当看自己是向罪死了,但向上帝则看自己是活在基督耶稣里。
12 所以,不要让罪辖制你们必死的身体,使你们顺从身体的私欲; 13 也不要将你们的身体献给罪作不义的工具,而是要像一个从死里复活的人将自己奉献给上帝,把身体献给上帝作义的工具。 14 罪不能再主宰你们,因为你们已经不在律法之下,而是在恩典之中。
做义的奴仆
15 那么,我们在恩典之中,不在律法之下,就可以任意犯罪吗?绝不可以! 16 你们难道不明白吗?你们献身给谁、服从谁,就是谁的奴隶。做罪的奴隶,结局是死亡;做上帝的奴仆,就被称为义人。 17 感谢上帝!你们从前虽然做过罪的奴隶,现在却衷心服从了所传给你们的教导, 18 从罪中得到释放,成为义的奴仆。
19 因为你们有人性的软弱,我就从人的立场向你们解释。以前你们将身体献给肮脏不法的事,任其奴役,助长不法。现在你们要将身体奉献给义,为义效劳,成为圣洁的人。 20 你们做罪的奴隶时,不受义的约束, 21 做了现在想起来也觉得羞耻的事,得到了什么益处呢?那些事只能导致死亡! 22 但现在你们已从罪中得到释放,做了上帝的奴仆,这样会使你们圣洁,最终得到永生。 23 因为罪的代价就是死亡,而上帝借着主基督耶稣赐下的礼物则是永生。
Warumi 6
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Kufa kwa Dhambi Lakini Hai Kwa Ajili ya Mungu
6 Hivyo, je, mnadhani inatupasa tuendelee kutenda dhambi ili Mungu atupe neema nyingi zaidi na zaidi? 2 Hapana! Utu wetu wa zamani wa dhambi ulikwisha. Umekufa. Je, tutaendeleaje kuishi katika dhambi? 3 Je, mmesahau kwamba sisi sote tulifanyika sehemu ya Kristo Yesu tulipobatizwa? Katika ubatizo wetu tulishiriki katika kifo chake. 4 Hivyo, tulipobatizwa, tulizikwa pamoja na Kristo na kushiriki katika kifo chake. Na kama vile Kristo alivyofufuliwa kutoka kwa wafu kwa nguvu ya ajabu ya Baba, ndivyo nasi tunaweza kuishi maisha mapya sasa.
5 Kristo alikufa, nasi tumeunganishwa pamoja naye kwa kufa kama yeye alivyokufa. Kwa hiyo tutaunganishwa pamoja naye kwa kufufuka kutoka katika kifo kama yeye alivyofanya. 6 Tunajua kuwa utu wetu wa zamani ulikufa msalabani pamoja naye. Hivyo ndivyo maisha ya utumwa tuliyokuwa nayo yalivyoangamizwa ili tusiendelee kuitumikia dhambi tena. 7 Yeyote aliyekufa amewekwa huru kutoka katika nguvu za dhambi.
8 Ikiwa tulikufa pamoja na Kristo, tunajua kwamba tutaishi pamoja naye pia. 9 Kristo alifufuliwa kutoka kwa wafu. Na tunajua kuwa hawezi kufa tena. Sasa mauti haina nguvu juu yake. 10 Ndiyo, Kristo alipokufa, alikufa ili aishinde nguvu ya dhambi mara moja, na siyo mara nyingine tena. Sasa anao uzima mpya, na uzima wake huo upo kwa nguvu za Mungu. 11 Kwa namna hiyo hiyo, mnapaswa kujiona kama mliokufa kwa dhambi na mlio hai kwa nguvu za Mungu kupitia Kristo Yesu.
12 Mwili mlionao katika uhai wenu wa sasa hapa duniani utakufa. Msiruhusu dhambi iutawale na kuwafanya ninyi kuzitumikia tamaa zake. 13 Msiitoe sehemu ya miili yenu kwa dhambi kwa ajili ya kutumika kutenda maovu. Jitoeni kwa Mungu, kama watu waliokufa lakini walio hai. Toeni sehemu za miili yenu kwa Mungu ili zitumiwe kwa kutenda mema. 14 Dhambi haitakuwa mtawala wenu, kwa sababu hamko chini ya sheria. Sasa mnaishi chini ya neema ya Mungu.
Watumwa wa Haki
15 Hivyo tufanye nini? Je, tutende dhambi kwa sababu tuko chini ya neema na siyo chini ya sheria? Hapana! 16 Hakika mnajua kuwa unakuwa mtumwa wa jambo lolote unaojitoa kulifanya. Chochote au yeyote unayemtii atakuwa bwana wako. Unaweza kufuata dhambi, au kumtii Mungu. Kufuata dhambi kunaleta kifo cha kiroho, lakini kumtii Mungu kunakufanya uhesabiwe na Mungu. 17 Hapo zamani mlikuwa watumwa wa dhambi na dhambi iliwatawala. Lakini ashukuriwe Mungu, mlitii kwa hiyari mafundisho yote aliyowaelekeza. 18 Mliwekwa huru kutoka katika dhambi, na sasa ninyi ni watumwa wa uaminifu wa wema wa Mungu. 19 Natumia dhana hii ya utumwa kutoka katika maisha ya kila siku kwa sababu mnahitaji msaada katika kuielewa kweli hii ya kiroho. Zamani mliitoa sehemu ya miili yenu kuwa watumwa wa mawazo yenu yaliyo machafu na maovu. Matokeo yake mliishi kwa ajili ya dhambi tu. Kwa njia hiyo hiyo, sasa mnapaswa kujitoa wenyewe kama watumwa wa uaminifu wa wema wa Mungu ili mweze kufaa kabisa kwa utumishi kwake.
20 Zamani mlikuwa watumwa wa dhambi, na wala hamkufikiri juu ya kutenda haki. 21 Mlifanya mambo maovu, na sasa mnaaibishwa kwa yale mliyotenda. Je, mambo haya yaliwasaidia? Hapana, yalileta kifo tu. 22 Lakini sasa mko huru dhidi ya dhambi. Mmekuwa watumwa wa Mungu, na mnaishi kwa ajili ya Mungu tu. Hili litawaletea uzima wa milele. 23 Watu wanapotenda dhambi, wanapokea malipo ya dhambi, ambayo ni kifo. Lakini Mungu huwapa watu wake zawadi ya bure, yaani uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.
Chinese Contemporary Bible Copyright © 1979, 2005, 2007, 2011 by Biblica® Used by permission. All rights reserved worldwide.
© 2017 Bible League International