罗马书 10
Chinese Contemporary Bible (Simplified)
10 弟兄姊妹,我心里切望并向上帝祈求的,就是以色列人能够得救。 2 我可以证明,他们对上帝有热心,但不是基于真知。 3 他们不知道上帝所赐的义,想努力建立自己的义,不肯服从上帝的义。 4 其实基督是律法的终极目的,使所有信靠祂的人都可以得到义。
求告主名的都必得救
5 关于律法的义,摩西写道:“人若遵行律法的诫命,就必活着。” 6 但是论到以信心为基础的义,圣经上说:“不要心里说,‘谁要升到天上去呢?’意思是谁要把基督领下来, 7 或说,‘谁要下到阴间去呢?’意思是谁要把基督从死人中领上来。” 8 其实这里是说:“这道近在咫尺,就在你口里,在你心中。”这道就是我们所传的信主之道。 9 你若口里承认耶稣是主,心里相信上帝使祂从死里复活,就必得救。 10 因为人心里相信,就可以被称为义人,口里承认,就可以得救。 11 正如圣经上说:“信靠祂的人必不致蒙羞。” 12 犹太人和希腊人并没有分别,因为主是所有人的主,祂厚待所有求告祂的人, 13 因为“凡求告主名的都必得救。”
14 可是,人还没信祂,怎能求告祂呢?还没听说过祂,怎能信祂呢?没有人传道,怎能听说过祂呢? 15 人没有受差遣,怎能传道呢?正如圣经上说:“那传福音之人的脚踪是何等佳美!” 16 只是并非人人都信福音,就像以赛亚先知所说的:“主啊!谁相信我们所传的呢?”
17 由此可见,听了道,才会信道;有了基督的话,才有道可听。 18 但我要问,以色列人没有听过吗?当然听过。因为
“他们的声音传遍天下,
他们的话语传到地极。”
19 我再问,难道以色列人不知道吗?首先,摩西说:
“我要借无名之民挑起你们的嫉妒,
用愚昧的国民激起你们的怒气。”
20 后来,以赛亚先知又放胆地说:
“我让没有寻找我的人寻见,
我向没有求问我的人显现。”
21 至于以色列人,他说:
“我整天伸出双手招呼那悖逆顽固的百姓。”
Warumi 10
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
10 Kaka na dada zangu, ninalotamani zaidi ni kwamba Waisraeli wote waokolewe. Hayo ndiyo maombi yangu kwa Mungu. 2 Naweza kusema hili juu yao: Kwa hakika wana bidii sana ya kumtii Mungu, lakini hawaijui njia iliyo sahihi. 3 Hawakuelewa kile ambacho Mungu alifanya ili kuwaokoa watu. Hivyo walijaribu kwa njia yao wenyewe kupata kibali kwa Mungu kwa kuishika sheria. Na wakakataa kuifuata njia ya Mungu ya kuwaokoa watu. 4 Sheria ilifikia mwisho wake wakati Kristo alipolikamilisha kusudi lake. Sasa kila mtu anayeiweka imani yake kwake anahesabiwa haki mbele za Mungu.
5 Musa anaandika juu ya kuhesabiwa haki kwa kuifuata sheria. Anasema: “Ili kupata uzima katika sheria imempasa mtu kuzitii.”(A) 6 Lakini Maandiko yanasema haya kuhusu kuhesabiwa haki kwa njia ya imani: “Usiyaseme haya kwako wewe mwenyewe, ‘Nani atapanda kwenda mbinguni?’” (Hii inamaanisha “Nani atapanda mbinguni kumchukua Kristo na kumleta chini duniani?”) 7 “Na usiseme, ‘Nani atashuka hadi ulimwengu uliopo chini huko?’” (Hii inamaanisha “Nani atashuka chini na kumchukua Kristo na kumfufua kutoka mauti?”)
8 Hivi ndivyo Maandiko yanavyosema: “Mafundisho ya Mungu yako karibu nawe; yako katika kinywa chako na katika moyo wako.”(B) Ni mafundisho ya imani tunayowaambia watu. 9 Ukikiri wazi kwa kinywa chako, kwamba “Yesu ni Bwana” na kuamini moyoni mwako kuwa Mungu alimfufua kutoka mauti, utaokolewa. 10 Ndiyo, tunamwamini Yesu mioyoni mwetu, na Mungu hutukubali kuwa wenye haki. Na tunakiri wazi wazi kwa vinywa vyetu kwamba tunamwamini Mungu na yeye anatuokoa.
11 Ndiyo, Maandiko yanasema, “Yeyote anayemwamini hataaibika.”(C) 12 Yanasema hivi kwa sababu hakuna tofauti kati ya Wayahudi na wasio Wayahudi. Bwana yule yule ndiye Bwana wa watu wote. Naye humbariki sana kila amwombaye akitaka msaada. 13 Ndiyo, “kila mtu anayemwita Bwana[a] ili kupata msaada, ataokolewa.”[b]
14 Lakini watu watawezaje kumwita Bwana na kupata msaada wake ikiwa hawamwamini yeye? Na watawezaje kumwamini Bwana ikiwa hawajawahi kuzisikia habari zake? Na watawezaje kuzisikia habari zake ikiwa hayupo mtu wa kuwaambia? 15 Na mtu atawezaje kwenda na kuwaambia habari hizo ikiwa hajatumwa? Haya, hii ndiyo sababu Maandiko yanasema, “Ni jambo la kufurahisha kumwona mtu anayepeleka Habari Njema!”(D)
16 Lakini si watu wote walizipokea Habari Njema hizo. Na hii ndiyo sababu Isaya alisema, “Bwana, nani aliyeamini yale tuliyowaeleza?”(E) 17 Kwa hiyo imani hupatikana kutokana na kusikia Habari Njema. Na watu husikia Habari Njema wakati mtu anapowaeleza kuhusu Kristo.
18 Lakini nauliza, “Je, watu hao walizisikia Habari Njema?” Ndio Kwa kweli walizisikia kama Maandiko yanavyosema,
“Sauti zao zilitoka na kuenea duniani kote.
Maneno yao yakaenda kila mahali ulimwenguni.”(F)
19 Lakini tena nauliza, “Je, watu wa Israeli hawakuelewa?” Ndiyo, walielewa. Musa alikuwa wa kwanza kujibu swali hili. Na anasema haya kwa ajili ya Mungu:
“Nitawatumia wale ambao siyo Taifa halisi ili liwafanye muone wivu.
Nitalitumia taifa ambalo halielewi ili mkasirike.”(G)
20 Kisha Isaya ana ujasiri wa kutosha kusema haya kwa ajili ya Mungu:
“Watu walionipata mimi hawakuwa wakinitafuta.
Nilijitambulisha kwa watu ambao hawakuwa wakinitafuta.”(H)
21 Lakini kuhusu watu wa Israeli Mungu anasema,
“Kutwa nzima nilisimama nikiwa tayari kuwakubali watu hawa,
lakini ni wakaidi na wamekataa kunitii.”(I)
Chinese Contemporary Bible Copyright © 1979, 2005, 2007, 2011 by Biblica® Used by permission. All rights reserved worldwide.
© 2017 Bible League International