Yohana 9
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yesu Amponya Aliyezaliwa Pasipo Kuwa na Uwezo wa Kuona
9 Yesu alipokuwa anatembea, alimwona mtu asiyeona tangu alipozaliwa. 2 Wafuasi wake wakamwuliza, “Mwalimu, kwa nini mtu huyu alizaliwa asiyeona? Dhambi ya nani ilifanya hili litokee? Ilikuwa ni dhambi yake mwenyewe au ya wazazi wake?” 3 Yesu akajibu, “Si dhambi yoyote ya huyo mtu wala ya wazazi wake iliyosababisha awe asiyeona. Alizaliwa asiyeona ili aweze kutumiwa kuonesha mambo makuu ambayo Mungu anaweza kufanya. 4 Kukiwa bado ni mchana, tunapaswa kuendelea kuzifanya kazi zake Yeye aliyenituma. Usiku unakuja, na hakuna mtu atakayeweza kufanya kazi wakati wa usiku. 5 Nikiwa bado nipo ulimwenguni, mimi ndiye nuru ya ulimwengu.”
6 Yesu aliposema haya, akatema mate chini kwenye udongo, akatengeneza tope na kumpaka yule asiyeona katika macho yake. 7 Yesu akamwambia, “Nenda ukanawe katika bwawa la Siloamu” (Siloamu maana yake ni “Aliyetumwa”.) Hivyo mtu yule akaenda katika bwawa lile, akanawa na kurudi akiwa mwenye kuona.
8 Majirani zake na wengine waliomwona akiomba omba wakasema, “Angalieni! Hivi huyu ndiye mtu yule aliyekaa siku zote na kuomba omba?”
9 Wengine wakasema, “Ndiyo! Yeye ndiye.” Lakini wengine wakasema, “Hapana, hawezi kuwa yeye. Huyo anafanana naye tu.”
Kisha yule mtu akasema, “Mimi ndiye mtu huyo.”
10 Wakamwuliza, “Kulitokea nini? Uliwezaje kupata kuona?”
11 Akawajibu, “Mtu yule wanayemwita Yesu alitengeneza tope akayapaka macho yangu. Kisha akaniambia ‘Nenda kanawe kwenye bwawa la Siloamu.’ Hivyo nikaenda kule na kunawa, na ndipo nikaweza kuona.”
12 Wakamwuliza, “Yuko wapi mtu huyo?”
Akajibu, “Mimi sijui aliko.”
Baadhi ya Mafarisayo Wana Maswali
13 Kisha watu wakampeleka huyo mtu kwa Mafarisayo. 14 Siku Yesu alipotengeneza yale matope na kuyaponya macho ya mtu huyo ilikuwa ni Sabato. 15 Hivyo Mafarisayo wakamwuliza huyo mtu, “Uliwezaje kuona?”
Akawajibu, “Alipaka matope katika macho yangu. Nikaenda kunawa, na sasa naweza kuona.”
16 Baadhi ya Mafarisayo wakasema, “Huyo mtu hatii sheria inayohusu siku ya Sabato. Kwa hiyo hatoki kwa Mungu.”
Wengine wakasema, “Lakini mtu aliye mtenda dhambi hawezi kufanya ishara kama hizi?” Hivyo hawakuelewana wao kwa wao. 17 Wakamuuliza tena huyo mtu, “Kwa vile aliponya macho yako, unasemaje juu ya mtu huyo?”
Akajibu, “Yeye ni nabii.” 18 Viongozi wa Kiyahudi walikuwa bado hawaamini kwamba haya yalimtokea mtu huyo; kwamba alikuwa haoni na sasa ameponywa. Lakini baadaye wakawaita wazazi wake. 19 Wakawauliza, “Je, huyu ni mwana wenu? Mnasema alizaliwa akiwa haoni. Sasa amewezaje kuona?”
20 Wazazi wake wakajibu, “Tunafahamu kwamba mtu huyu ni mwana wetu. Na tunajua kuwa alizaliwa akiwa asiyeona. 21 Lakini hatujui kwa nini sasa anaweza kuona. Hatumjui aliyeyaponya macho yake. Muulizeni mwenyewe. Yeye ni mtu mzima anaweza kujibu mwenyewe.” 22 Walisema hivi kwa sababu waliwaogopa viongozi wa Kiyahudi. Viongozi walikwisha azimia kwamba, wangemwadhibu mtu yeyote ambaye angesema Yesu alikuwa Masihi. Wangewazuia hao wasije tena kwenye sinagogi. 23 Ndiyo maana wazazi wake walisema, “Yeye ni mtu mzima. Muulizeni yeye!”
24 Hivyo viongozi wa Kiyahudi wakamwita yule aliyekuwa haoni. Wakamwambia aingie ndani tena. Wakasema, “Unapaswa kumheshimu Mungu na kutuambia ukweli. Tunamjua mtu huyu kuwa ni mtenda dhambi.”
25 Yule mtu akajibu, “Mimi sielewi kama yeye ni mtenda dhambi. Lakini nafahamu hili: Nilikuwa sioni, na sasa naweza kuona!”
26 Wakawuuliza, “Alikufanyia nini? Aliyaponyaje macho yako?”
27 Akajibu, “Tayari nimekwisha kuwaambia hayo. Lakini hamkutaka kunisikiliza. Kwa nini mnataka kusikia tena? Mnataka kuwa wafuasi wake pia?”
28 Kwa hili wakampigia makelele na kumtukana wakisema, “Wewe ni mfuasi wake, siyo sisi! Sisi ni wafuasi wa Musa. 29 Tunafahamu kwamba Mungu alisema na Musa. Lakini wala hatujui huyu mtu anatoka wapi!”
30 Yule mtu akajibu, “Hili linashangaza kweli! Hamjui anakotoka, lakini aliyaponya macho yangu. 31 Wote tunajua kuwa Mungu hawasikilizi watenda dhambi, bali atamsikiliza yeyote anayemwabudu na kumtii. 32 Hii ni mara ya kwanza kuwahi kusikia kwamba mtu ameponya macho ya mtu aliyezaliwa asiyeona. 33 Hivyo lazima anatoka kwa Mungu. Kama asingetoka kwa Mungu, asingefanya jambo lolote kama hili.”
34 Viongozi wa Kiyahudi wakajibu, “Ulizaliwa ukiwa umejaa dhambi. Unataka kutufundisha sisi?” Kisha wakamwambia atoke ndani ya sinagogi na kukaa nje.
Kutoona Kiroho
35 Yesu aliposikia kuwa walimlazimisha huyo mtu kuondoka, alikutana naye na kumuuliza, “Je, unamwamini Mwana wa Adamu?”
36 Yule mtu akajibu, “Niambie ni nani huyo, bwana, ili nimwamini.” 37 Yesu akamwambia, “Umekwisha kumwona tayari. Mwana wa Adamu ndiye anayesema nawe sasa.”
38 Yule mtu akajibu, “Ndiyo, ninaamini, Bwana!” Kisha akainama na kumwabudu Yesu.
39 Yesu akasema, “Nilikuja ulimwenguni ili ulimwengu uweze kuhukumiwa. Nilikuja ili wale wasiyeona waweze kuona. Kisha nilikuja ili wale wanaofikiri wanaona waweze kuwa wasiyeona.”
40 Baadhi ya Mafarisayo walikuwa karibu na Yesu. Wakamsikia akisema haya. Wakamwuliza, “Nini? Unasema sisi pia ni wale wasiyeona?”
41 Yesu akasema, “Kama mngekuwa wasiyeona hakika, msingekuwa na hatia ya dhambi. Lakini kwa kuwa mnasema mnaona, basi bado mngali na hatia.”
John 9
New King James Version
A Man Born Blind Receives Sight
9 Now as Jesus passed by, He saw a man who was blind from birth. 2 And His disciples asked Him, saying, “Rabbi, (A)who sinned, this man or his parents, that he was born blind?”
3 Jesus answered, “Neither this man nor his parents sinned, (B)but that the works of God should be revealed in him. 4 (C)I[a] must work the works of Him who sent Me while it is (D)day; the night is coming when no one can work. 5 As long as I am in the world, (E)I am the light of the world.”
6 When He had said these things, (F)He spat on the ground and made clay with the saliva; and He anointed the eyes of the blind man with the clay. 7 And He said to him, “Go, wash (G)in the pool of Siloam” (which is translated, Sent). So (H)he went and washed, and came back seeing.
8 Therefore the neighbors and those who previously had seen that he was [b]blind said, “Is not this he who sat and begged?”
9 Some said, “This is he.” Others said, [c]“He is like him.”
He said, “I am he.”
10 Therefore they said to him, “How were your eyes opened?”
11 He answered and said, (I)“A Man called Jesus made clay and anointed my eyes and said to me, ‘Go to [d]the pool of Siloam and wash.’ So I went and washed, and I received sight.”
12 Then they said to him, “Where is He?”
He said, “I do not know.”
The Pharisees Excommunicate the Healed Man
13 They brought him who formerly was blind to the Pharisees. 14 Now it was a Sabbath when Jesus made the clay and opened his eyes. 15 Then the Pharisees also asked him again how he had received his sight. He said to them, “He put clay on my eyes, and I washed, and I see.”
16 Therefore some of the Pharisees said, “This Man is not from God, because He does not [e]keep the Sabbath.”
Others said, (J)“How can a man who is a sinner do such signs?” And (K)there was a division among them.
17 They said to the blind man again, “What do you say about Him because He opened your eyes?”
He said, (L)“He is a prophet.”
18 But the Jews did not believe concerning him, that he had been blind and received his sight, until they called the parents of him who had received his sight. 19 And they asked them, saying, “Is this your son, who you say was born blind? How then does he now see?”
20 His parents answered them and said, “We know that this is our son, and that he was born blind; 21 but by what means he now sees we do not know, or who opened his eyes we do not know. He is of age; ask him. He will speak for himself.” 22 His parents said these things because (M)they feared the Jews, for the Jews had agreed already that if anyone confessed that He was Christ, he (N)would be put out of the synagogue. 23 Therefore his parents said, “He is of age; ask him.”
24 So they again called the man who was blind, and said to him, (O)“Give God the glory! (P)We know that this Man is a sinner.”
25 He answered and said, “Whether He is a sinner or not I do not know. One thing I know: that though I was blind, now I see.”
26 Then they said to him again, “What did He do to you? How did He open your eyes?”
27 He answered them, “I told you already, and you did not listen. Why do you want to hear it again? Do you also want to become His disciples?”
28 Then they reviled him and said, “You are His disciple, but we are Moses’ disciples. 29 We know that God (Q)spoke to (R)Moses; as for this fellow, (S)we do not know where He is from.”
30 The man answered and said to them, (T)“Why, this is a marvelous thing, that you do not know where He is from; yet He has opened my eyes! 31 Now we know that (U)God does not hear sinners; but if anyone is a worshiper of God and does His will, He hears him. 32 Since the world began it has been unheard of that anyone opened the eyes of one who was born blind. 33 (V)If this Man were not from God, He could do nothing.”
34 They answered and said to him, (W)“You were completely born in sins, and are you teaching us?” And they [f]cast him out.
True Vision and True Blindness
35 Jesus heard that they had cast him out; and when He had (X)found him, He said to him, “Do you (Y)believe in (Z)the Son of [g]God?”
36 He answered and said, “Who is He, Lord, that I may believe in Him?”
37 And Jesus said to him, “You have both seen Him and (AA)it is He who is talking with you.”
38 Then he said, “Lord, I believe!” And he (AB)worshiped Him.
39 And Jesus said, (AC)“For judgment I have come into this world, (AD)that those who do not see may see, and that those who see may be made blind.”
40 Then some of the Pharisees who were with Him heard these words, (AE)and said to Him, “Are we blind also?”
41 Jesus said to them, (AF)“If you were blind, you would have no sin; but now you say, ‘We see.’ Therefore your sin remains.
© 2017 Bible League International
Scripture taken from the New King James Version®. Copyright © 1982 by Thomas Nelson. Used by permission. All rights reserved.
