Add parallel Print Page Options

Mambo Maovu Yatatokea

Kaka na dada, tuna jambo la kuwaambia juu ya kuja kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Tunataka kuzungumza nanyi juu ya wakati huo tutakapokusanyika pamoja naye. Msikubali kufadhaishwa na kutiwa kuhofu ikiwa mtasikia kwamba siku ya Bwana tayari imekwishawadia. Wengine wanaweza kusema kwamba wazo hili limetoka kwetu katika jambo alilotuambia Roho, au tulilosema, au katika barua tuliyoiandika. Msidanganywe na chochote wanachoweza kusema kuhusu kuja kwa Bwana. Siku hiyo ya Bwana haitakuja mpaka itanguliwe na kukengeuka kwa wanadamu na kumwacha Mungu. Na siku hiyo haitakuja mpaka ajitokeze kwanza Mtu wa Uovu, yule ambaye ana uhakika kuwa ataangamizwa.[a] Huyo atasimama kinyume na kujiweka mwenyewe juu ya kila kitu ambacho watu wanaabudu au kudhani kuwa kinafaa kuabudiwa. Ataenda na kuingia ndani ya Hekalu[b] na kukikalia kiti cha enzi, akidai kuwa yeye ni Mungu.

Niliwaambia zaidi ya mara moja nilipokuwa huko kwamba mambo yote haya yangetokea. Je, mnakumbuka? Na mnafahamu kinachomzuia Mtu wa Uovu. Huyo hataruhusiwa kuonekana mpaka wakati sahihi utakapofika. Tayari nguvu ya uovu inatenda kazi ulimwenguni sasa. Lakini yupo mmoja anayeizuia nguvu hiyo. Na ataendelea kuizuia mpaka atakapoondolewa. Kisha huyo Mtu wa Uovu atatokea. Lakini Bwana Yesu atamuua kwa pumzi inayotoka katika kinywa chake. Bwana atakuja katika namna ambayo kila mtu atamwona, na huo utakuwa mwisho wa Mtu wa Uovu.

Kuja kwa Mtu wa Uovu itakuwa kazi ya Shetani. Atakuja na nguvu kuu, na atafanya aina zote za miujiza ya uongo, ishara, na maajabu. 10 Mtu wa Uovu atatumia kila aina ya uovu kuwatia ujinga wote walio njiani kuelekea kuangamia. Wamepotea kwa sababu walikataa kuupenda ujumbe wenye ukweli kuhusu Yesu na kuokolewa. 11 Hivyo Mungu atawaacha wadanganyike hata kuamini uongo.[c] 12 Wote watahukumiwa kwa sababu hawakuamini ujumbe wa kweli na kwa kuwa walifurahia kufanya maovu.

Mmechaguliwa kwa ajili ya Wokovu

13 Ndugu zangu, ninyi ni watu mnaopendwa na Bwana. Na imetupasa tumshukuru Mungu daima kwa sababu yenu. Hayo ndiyo tunayotakiwa kuyatenda, kwa sababu Mungu aliwaita kuwa miongoni mwa watu[d] wa kwanza kuokolewa. Mmeokolewa na Roho aliyewafanya muwe watu wa Mungu walio watakatifu kupitia kuiamini kweli. 14 Mungu aliwaita ninyi mpate wokovu. Aliwaita kwa kutumia Habari Njema tuliwahubiri. Mliitwa ili mshiriki katika utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo. 15 Hivyo simameni imara na kuendelea kuamini mafundisho tuliyowapa tulipokuwa huko na kupitia barua yetu.

16-17 Tunaomba kwamba Bwana Yesu Kristo na Mungu Baba yetu awafariji na kuwaimairisha katika kila jambo jema mnalotenda na kusema. Mungu alitupenda na kutupa kupitia neema matumaini ya ajabu na faraja isiyo na mwisho.

Footnotes

  1. 2:3 ataangamizwa Au “Kusababisha uharibifu”. Kwa maana ya kawaida, “ni mwana wa uharibifu”.
  2. 2:4 Hekalu Pengine Hekalu katika Yerusalemu. Tazama Hekalu katika Orodha ya Maneno.
  3. 2:11 uongo Ina maana ya kuamini uongo (mkubwa) juu ya Muasi (ya kwamba Muasi ndiye Mungu).
  4. 2:13 kuwa … watu Nakala zingine za Kiyunani zimeongeza, “kuanzia mwanzo”.

主再来的先兆

弟兄姊妹,关于主耶稣基督再来和我们到祂那里相聚的事情, 我们现在奉劝你们:无论是什么灵,或是传闻,或是冒充我们写的信,说主的日子已经到了,你们都不要轻易动摇,也不要惊慌。 不管别人用什么诡计,你们都不要上当。因为那日子来临之前,必有离经叛道的事发生,而那不法之徒,就是那注定灭亡的人也要出现。 他会抵挡主,高抬自己超过一切所谓的神明和人们崇拜的对象,甚至坐在上帝的殿中以上帝自居!

我还在你们那里的时候,曾告诉过你们这些事,你们忘记了吗? 现在,你们知道是什么拦阻他,使他等到特定的时间才出现。 其实那不法之徒的阴谋已经在酝酿中,然而现在有一位在拦阻他。等到拦阻他的那位一离开, 他就会出现,但主耶稣会用自己口中的气毁灭他,用从天降临的荣光废掉他。

他来要按照撒旦的伎俩行各样虚假的异能、神迹和奇事, 10 用尽各样诡计欺骗那些将要灭亡的人,因为他们不喜欢接受那能拯救他们的真理。 11 上帝就让他们是非不辨,去相信那些虚假的谎言, 12 使一切不相信真理、反喜爱不义的人都被定罪。

要坚定不移

13 主所爱的弟兄姊妹,我们应该时常为你们感谢上帝,因为上帝一开始就拣选了你们,为了使你们借着圣灵得以圣洁,并且相信真理,从而得救。 14 上帝借着我们所传的福音呼召了你们,使你们可以得到我们主耶稣基督的荣耀。 15 所以,各位弟兄姊妹,务要坚定不移,无论是我们信上的教导还是口头的教导,你们都要坚守。

16 愿主耶稣基督和爱我们、开恩将永远的安慰和美好的盼望赐给我们的父上帝, 17 安慰你们的心,使你们在一切善行善言上刚强。

The Man of Lawlessness

Concerning the coming of our Lord Jesus Christ(A) and our being gathered to him,(B) we ask you, brothers and sisters, not to become easily unsettled or alarmed by the teaching allegedly from us—whether by a prophecy or by word of mouth or by letter(C)—asserting that the day of the Lord(D) has already come.(E) Don’t let anyone deceive you(F) in any way, for that day will not come until the rebellion(G) occurs and the man of lawlessness[a] is revealed,(H) the man doomed to destruction. He will oppose and will exalt himself over everything that is called God(I) or is worshiped, so that he sets himself up in God’s temple, proclaiming himself to be God.(J)

Don’t you remember that when I was with you I used to tell you these things?(K) And now you know what is holding him back,(L) so that he may be revealed at the proper time. For the secret power of lawlessness is already at work; but the one who now holds it back(M) will continue to do so till he is taken out of the way. And then the lawless one will be revealed,(N) whom the Lord Jesus will overthrow with the breath of his mouth(O) and destroy by the splendor of his coming.(P) The coming of the lawless one will be in accordance with how Satan(Q) works. He will use all sorts of displays of power through signs and wonders(R) that serve the lie, 10 and all the ways that wickedness deceives those who are perishing.(S) They perish because they refused to love the truth and so be saved.(T) 11 For this reason God sends them(U) a powerful delusion(V) so that they will believe the lie(W) 12 and so that all will be condemned who have not believed the truth but have delighted in wickedness.(X)

Stand Firm

13 But we ought always to thank God for you,(Y) brothers and sisters loved by the Lord, because God chose you as firstfruits[b](Z) to be saved(AA) through the sanctifying work of the Spirit(AB) and through belief in the truth. 14 He called you(AC) to this through our gospel,(AD) that you might share in the glory of our Lord Jesus Christ.

15 So then, brothers and sisters, stand firm(AE) and hold fast to the teachings[c] we passed on to you,(AF) whether by word of mouth or by letter.

16 May our Lord Jesus Christ himself and God our Father,(AG) who loved us(AH) and by his grace gave us eternal encouragement and good hope, 17 encourage(AI) your hearts and strengthen(AJ) you in every good deed and word.

Footnotes

  1. 2 Thessalonians 2:3 Some manuscripts sin
  2. 2 Thessalonians 2:13 Some manuscripts because from the beginning God chose you
  3. 2 Thessalonians 2:15 Or traditions