2 Wathesalonike 1
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
1 Salamu kutoka kwa Paulo, Sila na Timotheo.
Kwa kanisa la Thesalonike lililo mali ya Mungu baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
2 Neema na amani viwe kwenu kutoka kwa Mungu Baba na Bwana wetu Yesu Kristo.
3 Kaka na dada zetu, tunamshukuru Mungu kwa ajili yenu. Na hivyo ndivyo tunavyopaswa kufanya, kwani mnatupa sababu ya kushukuru na imani yenu inakua zaidi na zaidi. Pamoja na hilo upendo ambao kila mmoja wenu anao kwa mwenzake nao unakua. 4 Hivyo tunayaeleza makanisa mengine ya Mungu namna tunavyojivuna kuhusu ninyi. Tunawaeleza jinsi mlivyoendelea kwa subira kuwa imara na waaminifu, ingawa mnateswa na kusumbuliwa na matatizo mengi.
Mungu Atafanya Mambo Kuwa Sawa
5 Huu ni uthibitisho kwamba Mungu ni wa haki katika hukumu zake. Hutaka kuwastahilisha katika ufalme wake. Kuteswa kwenu ni kwa ajili ya ufalme huo. 6 Ni haki kwa Mungu kuwaadhibu wale wanaowaletea matatizo. 7 Atawaletea unafuu wanaoteseka. Atawaletea ninyi nasi unafuu huo atakapokuja Bwana Yesu kutoka mbinguni ili wote wamwone, pamoja na malaika wake wenye nguvu zilizotukuka. 8 Atakuja na moto unaoteketeza kuwaadhibu wasiomjua Mungu na wanaokataa kuitii Habari Njema ya Bwana wetu Yesu. 9 Wataadhibiwa na maangamizi yasio na mwisho. Hawataruhusiwa kuwa na Bwana lakini watatengwa mbali na nguvu zake za utukufu. 10 Hii itatokea siku ambapo Bwana Yesu atakuja na kupokea heshima miongoni mwa watu wake watakatifu. Na wote wanaomwamini watamstaajabu. Na hii inawajumuisha ninyi kwa sababu mliamini yale tuliyowaambia.
11 Hii ndiyo sababu daima tunawaombea. Tunamwomba Mungu wetu awasaidie kuishi katika njia njema aliyoitaka alipowachagua. Wema mlionao unawafanya mtake kufanya mema. Na imani mliyonayo inafanya mfanye kazi. Tunaomba kwamba kupitia nguvu zake Mungu atayakamilisha yote mema mliyokusudia kufanya pamoja na kazi zote zinazotokana na imani yenu. 12 Kisha jina la Bwana wetu Yesu litaheshimiwa kwa sababu yenu, nanyi mtaheshimiwa kwa sababu yake, na mtaheshimiwa kwa sababu yake. Hii inaweza kutokea tu kwa neema ya Mungu wetu na Bwana Yesu Kristo.
帖撒罗尼迦后书 1
Chinese Contemporary Bible (Simplified)
1 我保罗同西拉和提摩太写信给帖撒罗尼迦属于我们父上帝和主耶稣基督的教会。
2 愿我们的父上帝和主耶稣基督赐给你们恩典和平安!
感恩与劝勉
3 弟兄姊妹,我们应当为你们常常感谢上帝,这是合宜的,因为你们的信心不断增长,彼此相爱的心也不断增加。 4 因此,我们在上帝的众教会中夸奖你们在各种迫害和患难中的坚忍和信心。 5 你们这种表现正是上帝公义审判的明证,使你们配进上帝的国,你们正在为这国受苦。
6 上帝是公义的,祂必以患难来报应那些迫害你们的人。 7 当主耶稣和祂大能的天使在烈焰中从天上显现时,祂必使你们这些受苦的人和我们同得安慰, 8 惩罚那些不认识上帝、不听从有关我们主耶稣之福音的人。 9 那些人要受的刑罚就是离开主的面和祂荣耀的权能,永远灭亡。 10 主降临的那日,祂要在祂的众圣徒中得到荣耀,使所有的信徒惊叹不已。你们也会在当中,因为你们相信了我们做的见证。
11 因此,我们常常为你们祷告,愿我们的上帝看你们配得祂的呼召,用大能成全你们一切美好的心愿和凭信心所做的工作。 12 这样,按照我们的上帝和主耶稣基督所赐的恩典,主耶稣基督的名便在你们身上得到荣耀,你们也在祂身上得到荣耀。
© 2017 Bible League International
Chinese Contemporary Bible Copyright © 1979, 2005, 2007, 2011 by Biblica® Used by permission. All rights reserved worldwide.