我保羅同西拉和提摩太寫信給帖撒羅尼迦屬於我們父上帝和主耶穌基督的教會。

願我們的父上帝和主耶穌基督賜給你們恩典和平安!

感恩與勸勉

弟兄姊妹,我們應當為你們常常感謝上帝,這是合宜的,因為你們的信心不斷增長,彼此相愛的心也不斷增加。 因此,我們在上帝的眾教會中誇獎你們在各種迫害和患難中的堅忍和信心。 你們這種表現正是上帝公義審判的明證,使你們配進上帝的國,你們正在為這國受苦。

上帝是公義的,祂必以患難來報應那些迫害你們的人。 當主耶穌和祂大能的天使在烈焰中從天上顯現時,祂必使你們這些受苦的人和我們同得安慰, 懲罰那些不認識上帝、不聽從有關我們主耶穌之福音的人。 那些人要受的刑罰就是離開主的面和祂榮耀的權能,永遠滅亡。 10 主降臨的那日,祂要在祂的眾聖徒中得到榮耀,使所有的信徒驚歎不已。你們也會在當中,因為你們相信了我們做的見證。

11 因此,我們常常為你們禱告,願我們的上帝看你們配得祂的呼召,用大能成全你們一切美好的心願和憑信心所做的工作。 12 這樣,按照我們的上帝和主耶穌基督所賜的恩典,主耶穌基督的名便在你們身上得到榮耀,你們也在祂身上得到榮耀。

Salamu kutoka kwa Paulo, Sila na Timotheo.

Kwa kanisa la Thesalonike lililo mali ya Mungu baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.

Neema na amani viwe kwenu kutoka kwa Mungu Baba na Bwana wetu Yesu Kristo.

Kaka na dada zetu, tunamshukuru Mungu kwa ajili yenu. Na hivyo ndivyo tunavyopaswa kufanya, kwani mnatupa sababu ya kushukuru na imani yenu inakua zaidi na zaidi. Pamoja na hilo upendo ambao kila mmoja wenu anao kwa mwenzake nao unakua. Hivyo tunayaeleza makanisa mengine ya Mungu namna tunavyojivuna kuhusu ninyi. Tunawaeleza jinsi mlivyoendelea kwa subira kuwa imara na waaminifu, ingawa mnateswa na kusumbuliwa na matatizo mengi.

Mungu Atafanya Mambo Kuwa Sawa

Huu ni uthibitisho kwamba Mungu ni wa haki katika hukumu zake. Hutaka kuwastahilisha katika ufalme wake. Kuteswa kwenu ni kwa ajili ya ufalme huo. Ni haki kwa Mungu kuwaadhibu wale wanaowaletea matatizo. Atawaletea unafuu wanaoteseka. Atawaletea ninyi nasi unafuu huo atakapokuja Bwana Yesu kutoka mbinguni ili wote wamwone, pamoja na malaika wake wenye nguvu zilizotukuka. Atakuja na moto unaoteketeza kuwaadhibu wasiomjua Mungu na wanaokataa kuitii Habari Njema ya Bwana wetu Yesu. Wataadhibiwa na maangamizi yasio na mwisho. Hawataruhusiwa kuwa na Bwana lakini watatengwa mbali na nguvu zake za utukufu. 10 Hii itatokea siku ambapo Bwana Yesu atakuja na kupokea heshima miongoni mwa watu wake watakatifu. Na wote wanaomwamini watamstaajabu. Na hii inawajumuisha ninyi kwa sababu mliamini yale tuliyowaambia.

11 Hii ndiyo sababu daima tunawaombea. Tunamwomba Mungu wetu awasaidie kuishi katika njia njema aliyoitaka alipowachagua. Wema mlionao unawafanya mtake kufanya mema. Na imani mliyonayo inafanya mfanye kazi. Tunaomba kwamba kupitia nguvu zake Mungu atayakamilisha yote mema mliyokusudia kufanya pamoja na kazi zote zinazotokana na imani yenu. 12 Kisha jina la Bwana wetu Yesu litaheshimiwa kwa sababu yenu, nanyi mtaheshimiwa kwa sababu yake, na mtaheshimiwa kwa sababu yake. Hii inaweza kutokea tu kwa neema ya Mungu wetu na Bwana Yesu Kristo.