Font Size
Ufunua wa Yohana 20:1-3
Neno: Bibilia Takatifu
Ufunua wa Yohana 20:1-3
Neno: Bibilia Takatifu
Utawala Wa Miaka Elfu Moja
20 Kisha nikaona malaika akija kutoka mbinguni akiwa ameshika ufunguo wa lile shimo la kuzimu, na mnyororo mkubwa mkononi. 2 Akalishika lile joka, yule nyoka wa kale ambaye ni Ibilisi au Shetani, akamfunga kwa muda wa miaka elfu moja. 3 Akamtupa kuzi muni; akamfungia huko na kumzibia kabisa, asipate nafasi ya kudanganya mataifa tena mpaka hiyo miaka elfu moja iishe. Baada ya hapo ataachiliwa kwa muda mfupi.
Read full chapter
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Copyright © 1989 by Biblica