Wataalamu Wa Nyota Wafika Kumwona Mtoto Yesu

Basi Yesu alipozaliwa katika mji wa Betlehemu huko Yudea, wakati wa utawala wa mfalme Herode, wataalamu wa mambo ya nyota kutoka Mashariki walifika Yerusalemu wakawa wakiuliza, kutoka kwao kuhusu wakati kamili ambao ile nyota ilionekana.

Mfalme Herode alipopata habari hizi alifadhaika sana na watu wote wa Yerusalemu wakawa na hali ya wasiwasi. Herode akaitisha mkutano wa makuhani wakuu na waandishi, akawataka wamweleze mahali ambapo Kristo angezaliwa.

Wakamjibu, “Atazaliwa Betlehemu ya Yudea, kwa maana nabii aliandika hivi kuhusu jambo hili: ‘Nawe Betlehemu, katika nchi ya Yuda, wewe si wa mwisho miongoni mwa watawala wa Yuda; kwa maana atatoka mtawala kwako atakayetawala watu wangu Israeli.’ ”

Ndipo Herode akawaita wale wataaamu wa nyota kwa siri aka pata uhakikisho Halafu akawatuma Bethlehemu akiwaagiza, “Nendeni mkamtafute huyo mtoto kwa bidii, na mkishampata, mnile tee habari ili na mimi niende kumsujudia.”

Read full chapter