Font Size
Matayo 13:3-9
Neno: Bibilia Takatifu
Matayo 13:3-9
Neno: Bibilia Takatifu
3 Kisha akawaambia mambo mengi kwa mifano, akasema: “Mpanzi alikwenda kupanda mbegu. 4 Alipokuwa akitawanya mbegu, baadhi zikaanguka njiani, ndege wakaja wakazila. 5 Nyingine zikaanguka kwenye mawe, ambapo hapakuwa na udongo wa kutosha. Zikakua haraka kwa sababu udongo ulikuwa kidogo. 6 Lakini jua kali lilipowaka, mimea hiyo ilinyauka na kukauka kwa sababu mizizi yake haikwenda chini. 7 Mbegu nyingine zilianguka kwenye miiba. Miiba hiyo ikakua ikazisonga. 8 Mbegu nyingine zilianguka kwenye udongo mzuri zikatoa mazao, nyingine mara mia moja zaidi ya mbegu zilizopandwa, nyingine mara sitini na nyingine mara the lathini. 9 Mwenye nia ya kusikia na asikie.”
Read full chapter
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Copyright © 1989 by Biblica