Marko 8:1-9
Neno: Bibilia Takatifu
Yesu Alisha Watu Elfu Nne
8 Muda si mrefu baadaye, umati mkubwa wa watu ulikusanyika tena. Kwa kuwa walikuwa hawana chakula, Yesu akawaita wanafunzi wake akawaambia, 2 “Ninawaonea huruma hawa watu. Wamekuwa nami kwa muda wa siku tatu sasa na hawana chakula. 3 Nikiwaruhusu waende bila kula, watazimia njiani na baadhi yao wametoka mbali.”
4 Wanafunzi wake wakamjibu, “Lakini hapa nyikani tutapata wapi chakula cha kutosha kuwalisha?”
5 Yesu akawauliza, “Mna mikate mingapi?” Wakajibu, “Saba.”
6 Akawaambia watu wakae chini. Kisha akaichukua ile mikate saba na baada ya kushukuru akaimega, akawapa wanafunzi wake wawa gawie watu. Wanafunzi wake wakafanya hivyo. 7 Walikuwa pia na visamaki vichache, Yesu akavibariki, akawaamuru wanafunzi wake wawagawie watu. 8 Watu walikula wakatosheka na baadaye wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia wakajaza vikapu saba. 9 Na watu waliokula walikuwa wapata elfu nne. Baada ya kuwaaga,
Read full chapter
Marko 8:1-9
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yesu Awalisha Watu Zaidi ya 4,000
(Mt 15:32-39)
8 Wakati mwingine katika siku zile kundi kubwa la watu lilikusanyika na halikuwa na chakula. Yesu akawaita wanafunzi wake na kuwaambia, 2 “Nawahurumia watu hawa, kwa sababu hata sasa wamekuwa nami kwa siku tatu, na hawana kitu cha kula.”
3 Nikiwaacha waende majumbani mwao wakiwa na njaa, wataanguka njiani; na baadhi yao wametoka mbali.
4 Wanafunzi wake wakamjibu, “Wapi mtu yeyote atapata chakula cha kutosha mahali hapa jangwani cha kuwalisha watu hawa?”
5 Yesu akawauliza, “Mnayo mikate mingapi?” Wakajibu, “Saba.”
6 Kisha Yesu akaliagiza kundi la watu kuketi chini ardhini Akachukua mikate ile saba, akashukuru, akaimega na kuwapa wanafunzi wake waigawe. Nao wakaigawa kwenye kundi. 7 Kulikuwapo pia samaki wadogo wachache. Yesu akawabariki wale samaki na kuwaambia waigawe nayo pia.
8 Watu walikula na kushiba. Wakakusanya vikapu saba vilivyojaa mabaki. 9 Ilikuwa kama watu 4,000. Kisha Yesu akawaacha waende.
Read full chapterCopyright © 1989 by Biblica
Copyright © 2017 by Bible League International