Font Size
Marko 3:1-6
Neno: Bibilia Takatifu
Marko 3:1-6
Neno: Bibilia Takatifu
Yesu Amponya Mtu Aliyelemaa Mkono
3 Yesu aliingia tena katika sinagogi na mtu mmoja aliyelemaa mkono alikuwapo pia. 2 Baadhi ya watu waliokuwa wakimtega, ili wapate sababu ya kumshtaki, walimtazama kwa makini waone kama atamponya huyo kilema siku ya sabato. 3 Yesu akamwambia yule mwe nye mkono uliolemaa, “Njoo hapa mbele.”
4 Yesu akawauliza, “Ni lipi lililo halali siku ya sabato? Kufanya jema, au baya? Kusalimisha maisha au kuua?” Wakakaa kimya.
5 Yesu akawatazama kwa hasira, akahuzunishwa na ugumu wa mioyo yao. Akamwambia yule mtu, “Nyoosha mkono wako.” Akauny oosha, nao ukapona kabisa! 6 Kisha Mafarisayo wakatoka nje, wakaenda kushauriana na kundi la wafuasi wa Herode mbinu za kum wua Yesu.
Read full chapter
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Copyright © 1989 by Biblica