Yesu Anamtokea Mariamu Magdalena

Baada ya Yesu kufufuka, alimtokea kwanza Mariamu Mag dalena, yule aliyemtoa pepo saba. 10 Mariamu akaenda akawaambia wale waliokuwa wakifuatana na Yesu. Wakati huo walikuwa bado wanalia na kuomboleza. 11 Lakini waliposikia kwamba Yesu yu hai na kwamba Mariamu alikuwa amemwona, hawakuamini.

Yesu Awatokea Wanafunzi Wawili

12 Baadaye Yesu aliwatokea kwa namna nyingine wanafunzi wawili walipokuwa wakienda shamba. 13 Nao pia walirudi wakawaam bia wenzao. Lakini pia hawakuamini.

Yesu Anawatokea Wale Wanafunzi Kumi Na Mmoja

14 Mwishowe, Yesu aliwatokea wale wanafunzi kumi na mmoja, wakiwa wanakula chakula. Akawakemea kwa kutokuamini kwao na kwa ugumu wa mioyo yao uliowafanya wakatae kuwasadiki wale waliomwona baada ya kufufuka.

15 Akawaambia, “Nendeni ulimwenguni kote, mkawahubirie watu wote Habari Njema. 16 Ye yote atakayeamini na kubatizwa ataoko lewa. Lakini ye yote ambaye atakataa kuamini, atahukumiwa.

17 “Na hizi ndizo ishara zitakazoandamana na wale wata kaoamini: Kwa kutumia jina langu watafukuza pepo; watasema kwa lugha mpya; 18 wataweza hata kuwakamata nyoka na kunywa sumu lakini wasidhurike; watawawekea wagonjwa mikono, nao watapona.”

Yesu Apaa Kwenda Mbinguni

19 Yesu alipokwisha kuwaambia maneno haya, alichukuliwa juu mbinguni, akaketi upande wa kulia wa Mungu.

Read full chapter

Baadhi ya Wafuasi Wamwona Yesu

(Mt 28:9-10; Yh 20:11-18; Lk 24:13-35)

Baada ya Yesu kufufuka alfajiri na mapema siku ya Jumapili, alimtokea kwanza Maria Magdalena, ambaye awali alifukuza mashetani saba kutoka kwake. 10 Baada ya Mariamu kumwona Yesu, alienda na kuwaeleza wanafunzi wake. Walikuwa wamehuzunishwa sana na walikuwa wakilia. 11 Lakini Mariamu aliwaambia kwamba Yesu yu hai. Aliwaambia ya kwamba yeye amemwona, lakini wao hawakumwamini.

12 Baada ya hayo, Yesu kwa namna tofauti akawatokea wanafunzi wake wawili walipokuwa wakitembea kuelekea mashambani. 13 Hawa kisha walirudi na wakawasimulia wengine wote, lakini nao hawakuwaamini.

Yesu Awatokea Wafuasi Wake

(Mt 28:16-20; Lk 24:36-49; Yh 20:19-23; Mdo 1:6-8)

14 Baadaye, Yesu aliwatokea wale mitume kumi na mmoja walipokuwa wakila. Naye akawakaripia kwa kutokuwa na imani. Walikuwa wakaidi na walikataa kuwaamini wale waliomwona Yesu baada ya kufufuka kwake.

15 Naye akawaambia, “Nendeni ulimwenguni pote, na mkahubiri Habari Njema kwa uumbaji wote. 16 Yeyote atakayeamini na kubatizwa ataokolewa, lakini yeyote asiyeamini atahukumiwa. 17 Na wale waaminio wataweza kufanya ishara hizi kama uthibitisho: watafukuza mashetani kwa jina langu; watasema kwa lugha mpya wasizojifunza bado; 18 watakamata nyoka kwa mikono yao; na ikiwa watakunywa sumu yoyote, haitawadhuru; wataweka mikono yao kwa wagonjwa, nao watapona.”

Yesu Arudi Mbinguni

(Lk 24:50-53; Mdo 1:9-11)

19 Hivyo baada ya Bwana Yesu kuzungumza nao, alichukuliwa mbinguni, kuketi katika mkono wa kuume wa Mungu. 20 Na mitume wakatoka na kwenda kuhubiri kila mahali, na Bwana alifanya kazi pamoja nao akithibitisha kuwa ujumbe wao ni wa kweli kwa ishara zilizofuatana na mahubiri yao.

Read full chapter