Kuhusu Mwana Wa Daudi

35 Yesu alipokuwa akifundisha Hekaluni, aliuliza, “Mbona walimu wa sheria wanasema kwamba Kristo ni Mwana wa Daudi? 36 Kwa maana Daudi akiongozwa na Roho Mtakatifu alisema, ‘Bwana alimwambia Bwana wangu: keti mkono wangu wa kulia mpaka niwashi nde na kuwafedhehesha maadui zako chini ya miguu yako.’ 37 Ikiwa Daudi mwenyewe anamwita Bwana, yawezekanaje tena Kristo akawa mwanawe?” Watu wote wakamsikiliza kwa furaha.

Read full chapter