Font Size
Luka 6:1-5
Neno: Bibilia Takatifu
Luka 6:1-5
Neno: Bibilia Takatifu
Bwana Wa Sabato
6 Siku moja ya sabato Yesu alikuwa akipita katika mashamba ya ngano. Wanafunzi wake wakawa wakivunja masuke ya ngano, wakayafi kicha na kula punje zake. 2 Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, “Mbona mnavunja sheria kwa kuvuna ngano siku ya sabato?”
3 Yesu akawajibu, “Ninyi hamsomi Maandiko? Hamjasoma alicho fanya Mfalme Daudi wakati yeye na wafuasi wake walipokuwa na njaa? 4 Aliingia Hekaluni, akachukua ile mikate ya madhabahuni -ambayo huliwa na makuhani peke yao -akala, kisha akawapa na wafuasi wake wakala!” 5 Akaongezea kusema, “Mimi Mwana wa Adamu ni Bwana wa sabato.”
Read full chapter
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Copyright © 1989 by Biblica