Font Size
Luka 14:1-6
Neno: Bibilia Takatifu
Luka 14:1-6
Neno: Bibilia Takatifu
14 Siku moja ya sabato Yesu alipokuwa amekwenda kula chakula kwa mmoja wa viongozi wa Mafarisayo, watu walikuwa wakimtazama kwa makini. 2 Mtu mmoja mwenye ugonjwa wa kuvimba miguu na mikono akaja mbele yake. 3 Yesu akawauliza walimu wa sheria na Mafari sayo, “Je, sheria inaruhusu kumponya mtu siku ya sabato au hairuhusu?” 4 Wakakaa kimya. Basi Yesu akamshika yule mgonjwa akamponya, akamruhusu aende zake. 5 Kisha akawauliza, “Kama mmoja wenu angekuwa na mtoto au ng’ombe wake ambaye ametumbukia katika kisima siku ya sabato, hamtamvuta mara moja na kumtoa?” 6 Hawakuwa na la kujibu.
Read full chapter
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Copyright © 1989 by Biblica