Yohana 7:1-9
Neno: Bibilia Takatifu
Yesu Ahudhuria Sikukuu Ya Vibanda Yerusalemu
7 Baada ya mambo haya, Yesu alikwenda sehemu mbalimbali za Galilaya. Aliamua kutokwenda Yudea kwa sababu Wayahudi huko wali taka kumwua. 2 Sikukuu ya Vibanda ilipokaribia, 3 ndugu zake Yesu walimwambia, “Ni vema utoke hapa uende Yudea ili wanafunzi wako wapate kuona miujiza unayofanya. 4 Mtu anayetaka kujulikana, hafanyi mambo yake kwa siri. Kwa kuwa unafanya mambo haya, jion yeshe kwa ulimwengu.” 5 Hata ndugu zake hawakumwamini.
6 Yesu akawajibu, “Wakati wangu wa kwenda huko haujafika. Ninyi mnaweza kwenda wakati wo wote. 7 Ulimwengu hauwachukii ninyi lakini unanichukia mimi kwa sababu ninawashuhudia kwamba matendo yao ni maovu. 8 Ninyi nendeni kwenye sikukuu, lakini mimi sitahudhuria sikukuu hii kwa sababu wakati wangu haujawadia.” 9 Baada ya kusema hivyo, akabaki Galilaya.
Read full chapterCopyright © 1989 by Biblica