Divai ilipowaishia, mama yake Yesu alimwambia, “Hawana divai.” Yesu akamjibu, “Mama, mbona unanihusisha kwenye jambo hili? Wakati wangu bado haujafika.” Mama yake akawaambia watumishi, “Lo lote atakalowaambia, fanyeni. ”

Read full chapter

Hapo arusini divai ilipungua, mama yake Yesu akamwambia mwanaye, “Hawana divai ya kutosha.”

Yesu akajibu, “Mama, kwa nini unaniambia mambo hayo? Wakati sahihi kwangu kufanya kazi haujafika bado.”

Mama yake akawaambia wahudumu wa arusi, “Fanyeni lo lote lile atakalowaambia.”

Read full chapter