Sifa Za Kuhani Mkuu

Kwa maana kila kuhani mkuu anayechaguliwa miongoni mwa watu huteuliwa kumtumikia Mungu kwa niaba yao, kutoa sadaka na dhabihu kwa ajili ya dhambi zao. Anaweza kuwaonea huruma wale wasioel ewa na wanaopotoka kwa sababu yeye mwenyewe anasumbuliwa na udhaifu kama wao . Kwa sababu hii, anawajibika kutoa dhabihu kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe na kwa ajili ya dhambi za hao watu.

Hakuna mtu anayejichagulia heshima hii ya kuwa kuhani mkuu. Kila mmoja huitwa na Mungu kama vile Haruni alivyoitwa.

Kristo hakujichagulia mwenyewe utukufu wa kuwa kuhani mkuu. Bali aliteuliwa na Mungu ambaye alimwambia, “Wewe ni mwanangu, leo hii nimekuzaa;” na tena kama asemavyo mahali pengine, “Wewe ni kuhani milele, katika ngazi ile ya ukuhani ya Mel kizedeki. Yesu alipokuwa akiishi duniani, alitoa dua na maombi kwa kilio kikuu na machozi kwa Mungu ambaye angeweza kumwokoa na kumtoa katika kifo, naye Mungu alimsikia kwa sababu alikuwa mnyenyekevu na mtiifu. Ingawa alikuwa Mwana wa Mungu, aliji funza utii kutokana na mateso aliyopata; na baada ya kufanywa mkamilifu, akawa chanzo cha wokovu wa milele kwa wote wanaomtii, 10 akateuliwa na Mungu kuwa kuhani mkuu wa ngazi ile ile ya

Onyo Kuhusu Kuanguka

11 Kuhusu ukuhani huu, tunayo mengi ya kusema ambayo ni mag umu kuyaeleza, kwa maana ninyi si wepesi wa kuelewa. 12 Ingawa kwa wakati huu mngalipaswa kuwa walimu, lakini bado mnahitaji mtu wa kuwafundisha tena hatua za kwanza za neno la Mungu. Mnahitaji maziwa, wala si chakula kigumu. 13 Kwa maana anayeishi kwa maziwa peke yake bado ni mtoto mchanga, hana ujuzi katika mafund isho kuhusu neno la haki. 14 Bali chakula kigumu ni kwa ajili ya watu wazima, watu ambao wamekomaa akili kutokana na mafunzo ya mazoezi ya kupambanua kati ya mema na mabaya.

Basi sasa tutoke katika yale mafundisho ya msingi kuhusu Kristo, tupige hatua kufikia ukamilifu katika kuelewa kwetu. Hatupaswi tena kuwaeleza ninyi yale mafundisho ya msingi kuhusu kutubu na kuacha matendo yaletayo kifo, na kuhusu kumwamini Mungu pamoja na maagizo kuhusu ubatizo, kuwekea watu mikono, kufufuka kwa wafu na hukumu ya milele. Mungu akitujalia tutaendelea mbele.

Kwa maana haiwezekani tena kuwarejesha katika toba watu ambao waliwahi kuongoka, ambao wameonja uzuri wa mbinguni, wakashiriki Roho Mtakatifu, ambao wameonja wema wa neno la Mungu na nguvu za nyakati zijazo, kama wakikufuru. Kwa sababu wanamsulubisha tena Mwana wa Mungu mioyoni mwao na kumwaibisha hadharani. Ardhi ambayo baada ya kupata mvua ya mara kwa mara, hutoa mazao yanayowanufaisha wale ambao wanailima na kupokea bar aka kutoka kwa Mungu. Lakini kama ardhi hiyo itaotesha magugu na miiba, haina thamani, na inakaribia kulaaniwa. Mwisho wake ni kuchomwa moto.

Wanaopokea Ahadi Za Mungu

Ingawa tunasema hivi, ndugu zangu, kwa upande wenu tuna hakika ya mambo mazuri zaidi, yanayoandamana na wokovu. 10 Mungu si dhalimu hata asahau kazi yenu na upendo mliomwonyesha mlipowa saidia watu wake na mnavyoendelea kuwasaidia. 11 Tunapenda kila mmoja wenu aonyeshe bidii hiyo hiyo mpaka mwisho ili mpate kupo kea tumaini lenu. 12 Hatutaki muwe wavivu bali muige wale ambao kwa imani na subira hupokea yale yaliyoahidiwa na Mungu.

Uhakika Wa Ahadi Ya Mungu

13 Mungu alipompa Ibrahimu ahadi, aliapa kwa jina lake mwe nyewe kwa kuwa hapakuwa na mkuu kuliko yeye ambaye angeweza kuapa kwa jina lake. 14 Alisema, “Hakika nitakubariki na kukupatia watoto wengi.” 15 Na hivyo baada ya kungoja kwa subira, Abra hamu alipata ahadi hiyo.

16 Watu huapa kwa mtu aliye mkuu kuliko wao, na kiapo hicho huthibitisha kinachosemwa na humaliza ubishi wote. 17 Kwa hiyo Mungu alipotaka kuwahakikishia warithi wa ahadi yake kuhusu maku sudi yake yasiyobadilika, aliwathibitishia kwa kiapo. 18 Mungu alifanya hivyo ili, kwa kutumia mambo haya mawili yasiyobadilika, na ambayo Mungu hawezi kusema uongo, sisi tuliokimbilia usalama kwake tutiwe moyo, tushikilie kwa uthabiti tumaini lililowekwa mbele yetu.

19 Tunalo tumaini hili kama nanga ya roho zetu yenye nguvu na imara. Tumaini hili linaingia hadi ndani ya pazia 20 ambamo Yesu ameingia akitutangulia; ameingia huko kwa niaba yetu. Yeye amekuwa kuhani mkuu milele, kama Melkizedeki.

Kuhusu Melkizedeki, Kuhani Mkuu

Huyu Melkizedeki alikuwa ni mfalme wa Salemu na kuhani wa Mungu aliye juu. Abrahamu alipokuwa akirudi kutoka vitani ambako aliua wafalme wengi, Melkizedeki alikutana naye, akambariki. Abrahamu akampatia Melkizedeki sehemu ya kumi ya vitu vyote. Kwanza, jina hilo Melkizedeki maana yake ni “Mfalme wa haki” na pia yeye ni “Mfalme wa Salemu,” maana yake, “Mfalme wa amani.”

Yeye hana baba wala mama wala ukoo; hana mwanzo wala hana mwisho, bali kama alivyo Mwana wa Mungu, yeye adumu kuwa kuhani milele.

Angalieni jinsi alivyo mkuu! Hata Abrahamu, baba yetu mkuu, alimpa sehemu ya kumi ya nyara zake. Hata wana wa Lawi ambao ni makuhani, wameamriwa na sheria ya Mose kuwatoza Waisraeli ndugu zao, ambao ni wazao wa Abrahamu, sehemu ya kumi ya mapato yao. Ingawa huyu Melkizedeki si wa ukoo wa Lawi, alipokea sehemu ya kumi kutoka kwa Abrahamu , na akambariki huyu ambaye alikwisha pokea ahadi za Mungu. Wala hakuna ubishi kuwa mtu mdogo hubarikiwa na mtu aliye mkuu kuliko yeye. Kwa upande wa makuhani wa ukoo wa Lawi, sehemu ya kumi inapokelewa na binadamu ambao hufa; lakini kwa upande huu wa Melkizedeki, sehemu ya kumi inapokelewa na mtu ambaye tunahakikishiwa kuwa anaishi. Mtu anaweza kusema kwamba Lawi, ambaye hupokea sehemu ya kumi, alitoa sehemu ya kumi kupitia kwa Abrahamu, 10 kwa maana Melkizedeki alipokutana na Abrahamu, Lawi alikuwa bado hajazaliwa. Mbegu yake ilikuwa bado iko mwilini mwa Abrahamu babu yake.

Yesu Na Melkizedeki

11 Kama ukamilifu ungaliweza kupatikana kwa njia ya ukuhani wa Walawi, kwa maana watu walipewa sheria kupitia kwao, ilikuwapo haja gani tena ya kuwepo kuhani mwingine, yaani kuhani kama Mel kizedeki, ambaye si kama Aroni? 12 Kwa maana yanapotokea maba diliko kwenye ukuhani, ni lazima pawepo na mabadiliko katika she ria. 13 Maana Bwana wetu ambaye ndiye anayesemwa katika mambo haya, alikuwa ni wa kabila lingine, na hakuna mtu katika kabila lake aliyewahi kuhudumu katika madhabahu. 14 Inafahamika wazi kuwa Bwana wetu alitoka katika kabila la Yuda, na Mose hakuwahi kusema lo lote juu ya makuhani kutoka katika kabila hilo. 15 Na hili tunalosema linakuwa wazi zaidi anapotokea kuhani mwingine kama Melkizedeki; 16 ambaye ukuhani wake hautokani na kanuni za ukoo wake, bali hutokana na uwezo wa maisha yasiyoharibika. 17 Kwa maana ameshuhudiwa hivi: “Wewe ni kuhani milele, kama wa Melkizedeki.”

Melkizedeki.”

18 Sheria ya mwanzo imewekwa kando kwa kuwa ilikuwa dhaifu na tena haikufaa. 19 Kwa maana sheria haikufanya kitu cho chote kuwa kikamilifu, na sasa tumeletewa tumaini bora zaidi ambalo linatuwezesha kumkaribia Mungu.

20 Na tumaini hilo halikutolewa pasipo kiapo! Wale waliofa nywa makuhani huko nyuma hapakuwepo kiapo. 21 Bali Yesu alipofa nywa kuhani aliwekewa kiapo wakati Mungu alipomwambia: “Bwana ameapa wala hatabadili nia yake, ‘Wewe ni kuhani milele.”’

22 Kwa ajili ya kiapo hiki, Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi.

23 Makuhani wa zamani walikuwa wengi kwa sababu kifo kiliwa zuia kuendelea daima na huduma yao. 24 Lakini yeye anaendelea na ukuhani wake daima kwa maana anaishi milele. 25 Kwa hiyo anaweza kwa wakati wote kuwaokoa wale wanaomkaribia Mungu kupitia kwake, kwa sababu yeye anaishi daima ili kuwaombea.

26 Huyu ndiye kuhani mkuu tunayemhitaji: yeye ni mtakatifu, asiye na lawama, asiye na dosari, aliyetenganishwa na wenye dhambi na aliyeinuliwa juu ya mbingu. 27 Yeye hahitaji kutoa dhabihu kila siku kwa ajili ya dhambi zake kwanza kisha dhambi za watu, kama wale makuhani wakuu wengine. Yeye alitoa dhabihu mara moja kwa wakati wote, alipojitoa mwenyewe. 28 Kwa maana sheria ya Mose huchagua watu wenye udhaifu kuwa makuhani wakuu. Lakini neno la Mungu la kile kiapo ambalo lilikuja baada ya sheria, lil imteua Mwana, ambaye amefanywa kuwa mkamilifu milele.

Kuhani Mkuu Wa Agano Jipya

Basi, katika hayo yote, tunalosema ni hili: tunaye huyo kuhani mkuu, ambaye ameketi upande wa kuume wa kiti cha Mwenyezi mbinguni. Yeye ni mhudumu wa patakatifu katika ile hema ya kweli iliyowekwa na Bwana, na wala si na wanadamu.

Kila kuhani huteuliwa ili atoe sadaka na dhabihu, kwa hiyo ilikuwa muhimu kwamba huyu kuhani naye awe na kitu cha kutoa. Kama angalikuwa duniani asingalikuwa kuhani kwa sababu wapo makuhani wanaotoa sadaka kwa mujibu wa sheria ya Mose. Wanahu dumu katika patakatifu iliyo mfano na kivuli cha ile iliyoko mbinguni. Ndio maana Mose alipokaribia kujenga ile hema takatifu aliamriwa na Mungu, akisema, “Hakikisha kuwa unafanya kila kitu kulingana na mfano ulioonyeshwa mlimani.” Lakini Yesu amepewa huduma iliyo bora zaidi kuliko yao, kama vile lile agano ambalo yeye ni mpatanishi wake, lilivyo bora zaidi kuliko lile la zamani. Agano hili jipya limejengwa juu ya ahadi bora zaidi.

Kama lile agano la kwanza lisingekuwa na upungufu, kusinge kuwapo na haja ya kuwa na agano jingine. Lakini Mungu hakurid hika na watu wake, akasema, “Siku zinakuja, asema Bwana, nitaka pofanya agano jipya na nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda. Agano hili halitakuwa kama lile nililofanya na baba zao siku ile nilipowashika mkono niwaongoze kutoka nchi ya Misri; kwa kuwa hawakuwa waaminifu kwa agano langu, nami nikawaacha, asema Bwana. 10 Hili ndilo agano nitakalofanya na nyumba ya Israeli siku zile zitakapowadia, asema Bwana: nitaweka sheria zangu akilini mwao, na kuziandika mioyoni mwao, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. 11 Haitakuwapo haja tena kwao kumfundisha kila mtu mwenzake, au kila mtu ndugu yake, na kusema, ‘Mfahamu Bwana,’ kwa maana wote watanifahamu, tangu aliye mdogo kabisa hadi mkubwa kuliko wote. 12 Nitawasamehe maovu yao, na dhambi zao sitazikum buka tena”.

13 Anapozungumza juu ya agano jipya Mungu anahesabu lile agano la kwanza kuwa limechakaa, na kitu kilichochakaa na kuzeeka kitatoweka baada ya muda mfupi.

Agano La Kwanza Na Agano Jipya

Basi hata lile agano la kwanza lilikuwa na kanuni zake za ibada pamoja na mahali pa kuabudia hapa duniani. Hema la kuabu dia liliandaliwa likiwa na chumba cha kwanza ambamo mlikuwa na chombo cha kuwekea taa, na meza na mikate iliyowekwa wakfu. Chumba hiki kiliitwa Patakatifu. Nyuma ya pazia la pili, pali kuwa na chumba kiitwacho Patakatifu pa Patakatifu. Chumba hiki kilikuwa na madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba na sanduku la agano ambalo lilifunikwa kwa dhahabu pande zote. Sanduku hili lilikuwa na chombo cha dhahabu chenye ile mana na ile fimbo ya Aroni iliyochipuka, na yale mawe ya agano. Juu ya sanduku kulikuwa na makerubi wa utukufu ambao kivuli chao kilifunika kiti cha rehema. Lakini mambo haya sasa hatuwezi kuyaeleza kwa undani.

Vitu vyote vilipokwisha kupangwa namna hii, makuhani wal iingia mara kwa mara katika kile chumba cha kwanza kutoa huduma yao ya ibada. Lakini ni kuhani mkuu peke yake ambaye aliruhu siwa kuingia katika chumba cha ndani mara moja tu kwa mwaka. Tena ilibidi aingie huko na damu ambayo aliitoa kwa ajili yake mwe nyewe na kwa ajili ya dhambi za watu walizotenda pasipo kujua. Kwa njia hii, Roho Mtakatifu alikuwa akionyesha kwamba maadamu hema ya kwanza ilikuwa bado imesimama, njia ya kuingia katika Patakatifu pa Patakatifu ilikuwa bado haijafunguliwa. Hii ili kuwa ni kielelezo kwa wakati wa sasa, kuonyesha kwamba sadaka na dhabihu zilizotolewa zilikuwa haziwezi kutakasa dhamiri ya mtu anayeabudu. 10 Hizi zilikuwa ni sheria zinazohusu chakula na vinywaji na taratibu mbalimbali za utakaso wa nje, kanuni ambazo zingetumika mpaka wakati wa matayarisho ya utaratibu mpya.

Damu Ya Kristo Husafisha Dhamiri

11 Kristo alipokuja kama kuhani mkuu wa mambo mema ambayo tayari yamekwisha wasili, alipitia kwenye hema ya kuabudia ambayo ni kuu zaidi na bora zaidi na ambayo haikujengwa na binadamu, yaani ambayo si sehemu ya ulimwengu huu ulioumbwa. 12 Yeye aliingia patakatifu pa patakatifu mara moja tu kwa wakati wote, akichukua, si damu ya mbuzi na ndama, bali damu yake mwenyewe, na hivyo kutupatia ukombozi wa milele.

13 Kwa maana ikiwa damu ya mbuzi na mafahali na majivu ya ndama hunyunyizwa juu ya watu wachafu kidini ikawatakasa kwa kuwaondolea uchafu wao wa nje, 14 damu ya Kristo ambaye kwa njia ya Roho wa milele alijitoa mwenyewe kwa Mungu kama sadaka isiyokuwa na doa, itazisafisha dhamiri zetu zaidi sana kutokana na matendo yaletayo kifo, na kutuwezesha kumtumikia Mungu aliye hai.

15 Kwa sababu hii Kristo ni mjumbe wa agano jipya ili wale walioitwa wapokee urithi wa milele ulioahidiwa na Mungu; kwa kuwa alikufa awe fidia itakayowaweka huru na dhambi walizotenda chini ya agano la kwanza.

16 Ili hati ya urithi itambuliwe ni lazima pawepo na uthi bitisho kwamba huyo aliyeiandika amekwisha kufa. 17 Kwa maana hati ya urithi huwa na uzito tu wakati mtu amekwisha kufa; haiwezi kutumika wakati yule aliyeiandika angali hai. 18 Hii ndio maana hata lile agano la kwanza halikuweza kutekelezwa pasipo damu kumwagika. 19 Wakati Musa alipowatangazia watu amri zote za sheria, alichukua damu ya ndama na ya mbuzi, pamoja na maji na sufu nyekundu na hisopo akanyunyizia kitabu cha sheria na watu wote, 20 akasema, “Hii ndio damu ya agano ambalo Mungu amewaamuru kulitii.” 21 Vivyo hivyo akanyunyizia damu hiyo kwe nye lile hema na vifaa vyote vilivyotumika kwa ibada. 22 Hakika katika sheria, karibu kila kitu hutakaswa kwa damu; na pasipo kumwaga damu, hakuna msamaha wa dhambi.

23 Kwa hiyo ilikuwa muhimu vitu hivi ambavyo ni mfano wa vile vya mbinguni vitakaswe kwa njia hizi, lakini vitu halisi vya mbinguni vilihitaji dhabihu bora kuliko hizi. 24 Kwa maana Kristo hakuingia kwenye hema ya kuabudia iliyotengenezwa na bina damu kama mfano wa hema halisi. Yeye aliingia mbinguni penyewe, ambapo sasa anatuwakilisha mbele za Mungu. 25 Wala hakuingia mbinguni kujitoa mwenyewe mara kwa mara, kama kuhani mkuu ain giavyo Patakatifu pa Patakatifu kila mwaka na damu ambayo si yake. 26 Ingekuwa hivyo, ingalimpasa Kristo kuteswa mara nyingi tangu kuumbwa kwa ulimwengu. Lakini ilivyo ni kwamba ametokea mara moja tu kwa wakati wote, katika siku hizi za mwisho, ili atokomeze dhambi kwa kujitoa mwenyewe kuwa dhabihu. 27 Na kama ambavyo mwanadamu ameandikiwa kufa mara moja tu, na baada ya hapo kukabili hukumu; 28 hali kadhalika Kristo alitolewa kama dhabihu mara moja tu ili azichukue dhambi za watu wengi; naye atakuja mara ya pili, si kuchukua dhambi, bali kuwaletea wokovu wale wanaomngojea kwa hamu.

Dhabihu Ya Kristo Ilikuwa Ya Mwisho

10 Basi kwa kuwa sheria ni kivuli tu cha mambo mema yajayo na wala si mambo yenyewe, haiwezi kamwe, kwa njia ya dhabihu zito lewazo mwaka hadi mwaka, kuwakamilisha wale wanaoabudu. Kama isingekuwa hivyo, dhabihu hizo zingekuwa hazitolewi tena. Maana hao waabuduo wasingalijiona tena kuwa wana hatia kwa ajili ya dhambi zao baada ya kutakaswa mara moja. Badala yake, dhabihu hizo zilikuwa ni ukumbusho wa dhambi mwaka hadi mwaka. Kwa maana damu ya mafahali na mbuzi, haiwezi kamwe kuondoa dhambi.

Kwa sababu hii, Yesu alipokuja duniani alisema: “Hukutaka dhabihu na sadaka bali umeniandalia mwili. Hukupendezwa na sadaka za kuteketezwa wala sadaka zitolewazo kwa ajili ya dhambi. Ndipo nikasema, ‘Nipo hapa, kama ilivyoandikwa katika gombo la sheria kunihusu; nimekuja kutimiza mapenzi yako wewe Mungu.’ ”

Kwanza alisema, “Dhabihu na sadaka, sadaka za kuteketezwa wala sadaka zitolewazo kwa ajili ya dhambi hukutaka, wala huku pendezwa nazo,” ingawa hizi zilitolewa kwa mujibu wa sheria. Kisha akasema, “Niko hapa, nimekuja kutimiza mapenzi yako.” Anaweka kando ule utaratibu wa kwanza na kuanzisha utaratibu wa pili. 10 Na kwa mapenzi hayo, sisi tumetakaswa kwa njia ya sadaka ya mwili wa Yesu Kristo alioutoa mara moja tu, kwa wakati wote.

11 Kila kuhani husimama siku hadi siku akifanya huduma yake ya ibada na akitoa tena na tena dhabihu zile zile ambazo haziwezi kuondoa dhambi. 12 Lakini Kristo alipokwisha kutoa dhabihu yake kwa ajili ya dhambi mara moja tu kwa wakati wote, aliketi upande wa kulia wa Mungu. 13 Tangu wakati huo anangoja mpaka Mungu atakapowafanya maadui zake kuwa kiti cha miguu yake. 14 Maana kwa dhabihu moja tu amewafanya kuwa wakamilifu milele wale wote wanaotakaswa.

15 Roho Mtakatifu pia anatushuhudia kuhusu jambo hili. Kwanza anasema: 16 “Hili ndilo agano nitakalofanya nao baada ya siku hizo, asema Bwana. Nitaziweka sheria zangu mioyoni mwao na kuziandika akilini mwao.” 17 Kisha anasema: “Dhambi zao na makosa yao sitayakumbuka tena kamwe.”

18 Basi, haya yakishasamehewa, hakuna tena dhabihu inayoto lewa kwa ajili ya dhambi.