Kesho yake, walipokuwa wanaukaribia mji, Petro alipanda juu ghorofani kuomba mnamo saa sita. 10 Alipokuwa akisali aliona njaa akatamani kupata chakula. Lakini wakati kilipokuwa kinaan daliwa, alisinzia akaota ndoto. 11 Akaona katika ndoto mbingu zimefunguka na kitu kama shuka kubwa ikishushwa kwa ncha zake nne. 12 Ndani ya ile shuka walikuwemo aina zote za wanyama na nyoka na ndege. 13 Kisha sauti ikamwambia Petro, “Inuka, uchinje na ule mnyama ye yote umpendaye kati ya hawa.” 14 Petro akajibu, “La Bwana! Sijawahi kula cho chote ambacho kimetajwa na sheria zetu za Kiyahudi kuwa ni kichafu.” 15 Ile sauti ikarudia kusema naye mara ya pili, “Usiite cho chote alichokitakasa Bwana kuwa ni kichafu.” 16 Hii ilitokea mara tatu, ndipo ile shuka ikarudishwa mbinguni.

Read full chapter