Add parallel Print Page Options

22 Kwa hakika unaweza kuiona imani hiyo ilifanya kazi pamoja na matendo yake. Kwa hiyo imani yake ilikamilishwa na matendo yake. 23 Ndipo yakatimizwa yale yaliyo kwenye Maandiko kuwa, “Ibrahimu alimwamini Mungu, na kwa imani hiyo akafanywa kuwa mwenye haki[a] kwa Mungu,”(A) na kwa sababu hiyo akaitwa “Rafiki wa Mungu”.(B) 24 Mnamwona mtu huyo amefanywa kuwa mwenye haki kwa Mungu kwa matendo yake wala siyo kwa imani peke yake.

Read full chapter

Footnotes

  1. 2:23 akafanywa kuwa mwenye haki Ama alithibitishwa kuwa mwenye haki kama vile tafsiri zingine za walimu wa Biblia wangependa kutumia.