Font Size
Luka 12:54-56
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Luka 12:54-56
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Kuzielewa Nyakati
(Mt 16:2-3)
54 Ndipo Yesu akawaambia watu, “Mnapoona wingu likikua upande wa magharibi, mnasema, ‘Mvua inakuja,’ na muda si mrefu huanza kunyesha. 55 Mnapoona upepo unaanza kuvuma kutoka kusini mnasema, ‘Kutakuwa joto,’ na huwa hivyo. 56 Enyi wanafiki! Mnaweza kuiona nchi na anga na mkajua hali ya hewa itakavyokuwa. Kwa nini hamwelewi kinachotokea sasa?
Read full chapter
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
Copyright © 2017 by Bible League International