1 Yohana 1:1-7
Neno: Bibilia Takatifu
Neno La Uzima
1 Tunawaandikieni kuhusu kile ambacho kimekuwapo tangu mwanzo, ambacho tumekisikia na kukiona kwa macho yetu; ambacho tumekigusa kwa mikono yetu; yaani Neno la uzima. 2 Uzima huo uli tokea, nasi tumeuona na tunaushuhudia, na tunawatangazieni uzima wa milele uliokuwa kwa Baba, nao ukadhihirishwa kwetu. 3 Tunawa tangazia hicho tulichokiona na kukisikia ili nanyi pia mpate kushirikiana nasi. Na ushirika tulio nao ni wetu na Baba na Mwa nae Yesu Kristo. 4 Tunawaandikieni mambo haya ili furaha yetu ikamilike.
Kutembea Nuruni
5 Huu ndio ujumbe tuliousikia kutoka kwake, ambao tunawatan gazia: Mungu ni nuru na ndani yake hamna giza kamwe. 6 Tukisema tuna ushirika naye huku tunaendelea kuishi gizani tunasema uongo, wala hatutendi yaliyo ya kweli. 7 Bali tukiishi nuruni, kama yeye alivyo nuru, tunakuwa na ushirika sisi kwa sisi na damu ya Mwanae Yesu, inatutakasa dhambi zote.
Read full chapterCopyright © 1989 by Biblica