Kwa maana niliyopokea ndio niliyowapa ninyi, nayo ni muhimu sana: kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama ilivy oandikwa katika Maandiko. Na kwamba alizikwa na kufufuka siku ya tatu, kama ilivyoandikwa katika Maandiko. Na kwamba alimto kea Kefa, kisha akawatokea wale kumi na wawili. Baadaye akawa tokea ndugu waamini zaidi ya mia tano kwa pamoja, na wengi wao wangali hai, ingawa wengine wameshakufa. Kisha akamtokea Yakobo, na ndipo akawatokea mitume wote. Na mwisho wa wote, akanitokea na mimi, ambaye ni kama nilizaliwa kwa hali isiyo ya kawaida.

Read full chapter

Niliwapa ujumbe nilioupokea. Niliwaambia ukweli muhimu zaidi ya kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama Maandiko yanavyosema; kuwa alizikwa na alifufuliwa siku ya tatu, kama Maandiko yanavyosema na kwamba alimtokea Petro kisha mitume kumi na wawili. Baada ya hilo, aliwatokea waamini wengine zaidi ya mia tano kwa wakati mmoja. Wengi wao bado wanaishi sasa, lakini wengine wamekwisha kufa. Kisha alimtokea Yakobo na baadaye aliwatokea mitume wote. Mwisho wa yote kabisa alinitokea mimi. Nilikuwa tofauti, kama mtoto anayezaliwa wakati usiostahili.

Read full chapter