1 Wakorintho 15:3-8
Neno: Bibilia Takatifu
3 Kwa maana niliyopokea ndio niliyowapa ninyi, nayo ni muhimu sana: kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama ilivy oandikwa katika Maandiko. 4 Na kwamba alizikwa na kufufuka siku ya tatu, kama ilivyoandikwa katika Maandiko. 5 Na kwamba alimto kea Kefa, kisha akawatokea wale kumi na wawili. 6 Baadaye akawa tokea ndugu waamini zaidi ya mia tano kwa pamoja, na wengi wao wangali hai, ingawa wengine wameshakufa. 7 Kisha akamtokea Yakobo, na ndipo akawatokea mitume wote. 8 Na mwisho wa wote, akanitokea na mimi, ambaye ni kama nilizaliwa kwa hali isiyo ya kawaida.
Read full chapter
1 Wakorintho 15:3-8
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
3 Niliwapa ujumbe nilioupokea. Niliwaambia ukweli muhimu zaidi ya kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama Maandiko yanavyosema; 4 kuwa alizikwa na alifufuliwa siku ya tatu, kama Maandiko yanavyosema 5 na kwamba alimtokea Petro kisha mitume kumi na wawili. 6 Baada ya hilo, aliwatokea waamini wengine zaidi ya mia tano kwa wakati mmoja. Wengi wao bado wanaishi sasa, lakini wengine wamekwisha kufa. 7 Kisha alimtokea Yakobo na baadaye aliwatokea mitume wote. 8 Mwisho wa yote kabisa alinitokea mimi. Nilikuwa tofauti, kama mtoto anayezaliwa wakati usiostahili.
Read full chapterCopyright © 1989 by Biblica
Copyright © 2017 by Bible League International