Kufufuka Kwa Wafu

12 Basi kama tumehubiri ya kwamba Kristo alifufuliwa kutoka kwa wafu, inakuwaje baadhi yenu mnasema hakuna ufufuo wa wafu? 13 Lakini kama hakuna ufufuo wa wafu, basi Kristo hakufufuliwa. 14 Na ikiwa Kristo hakufufuliwa kutoka kwa wafu, mahubiri yetu ni bure na imani yenu ni bure. 15 Na zaidi ya hayo, tunaonekana kuwa tunamshuhudia Mungu uongo, kwa sababu tumeshuhudia kumhusu Mungu ya kuwa alimfufua Kristo kutoka kwa wafu. Na kumbe hakumfu fua, kama kweli wafu hawafufuliwi. 16 Kwa kuwa kama wafu hawa fufuliwi, basi hata Kristo hajafufuliwa. 17 Na ikiwa Kristo hajafufuliwa, imani yenu ni bure; nanyi bado mngali katika dhambi zenu. 18 Pia waamini wote waliokufa wakimwamini Yesu wamepotea. 19 Na kama imani yetu ndani ya Kristo ni kwa ajili ya maisha haya tu, basi sisi tunastahili kuhurumiwa kuliko watu wengine wo wote duniani. 20 Lakini ukweli ni kwamba Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, matunda ya kwanza ya wote waliolala.

Read full chapter

Tutafufuliwa Kutoka kwa Wafu

12 Tunamwambia kila mtu kuwa Kristo alifufuliwa kutoka kwa wafu. Hivyo kwa nini baadhi yenu mnasema watu hawatafufuliwa kutoka kwa wafu? 13 Ikiwa hakuna atakayefufuliwa kutoka kwa wafu, basi Kristo hakufufuliwa kutoka kwa wafu. 14 Na ikiwa Kristo hakufufuliwa, ujumbe tunaowahubiri ni bure. Na imani yenu ni bure. 15 Nasi tutakuwa na hatia ya kutoa ushuhuda wa uongo kuhusu Mungu, kwa sababu tumewahubiri watu kuhusu Yeye, kwa kusema kuwa alimfufua Kristo kutoka kwa wafu. Na ikiwa hakuna anayefufuliwa kutoka kwa wafu, basi Mungu hakumfufua Kristo. 16 Ikiwa wale waliokufa hawatafufuliwa, basi Kristo hakufufuliwa pia. 17 Na ikiwa Kristo hakufufuliwa kutoka kwa wafu, basi imani yenu ni bure; bado mngali watumwa wa dhambi zenu. 18 Na watu wa Kristo waliokwisha kufa wamepotea. 19 Ikiwa tumaini letu katika Kristo ni kwa ajili tu ya maisha haya hapa duniani, basi watu watuhurumie sisi kuliko mtu mwingine yeyote.

20 Lakini hakika Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu; ndiye wa kwanza miongoni mwa wafu wote watakaofufuliwa.

Read full chapter