Kumwabudu Mungu Kwa Mpango

26 Tuseme nini basi ndugu zangu? Mnapokutana pamoja, kila mtu ana wimbo, au neno la mafundisho, mafunuo, ujumbe katika lugha ngeni, au tafsiri ya lugha. Kila jambo lifanyike kwa sha baha ya kujengana. 27 Kama mtu akisema kwa lugha, basi waseme si zaidi ya wawili au watatu, mmoja baada ya mwingine; na lazima awepo mtu wa kutafsiri. 28 Lakini kama hakuna mtu wa kutafsiri, huyo mzungumzaji akae kimya kanisani na aseme na nafsi yake mwe nyewe na Mungu. 29 Watu wawili au watatu walio na unabii wa neno la Mungu waseme, na wengine wapime kwa makini yale yanayosemwa. 30 Kama mmoja wa wale waliokaa akipata mafunuo kutoka kwa Mungu, anayezungumza aache kusema. 31 Kwa maana wote mnaweza kutoa una bii, mtu mmoja mmoja, ili kila mtu anayesikiliza apate kufund ishwa na kutiwa moyo. 32 Roho za unabii ziko chini ya mamlaka ya manabii. 33 Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko bali ni Mungu wa amani. Kama ilivyo desturi katika mikutano ya watu wa Mungu,

Read full chapter

Mikutano Yenu Inapaswa Kuwasaidia Wote

26 Basi ndugu, mnapaswa kufanya nini? Mnapokusanyika, mtu mmoja ana wimbo, mwingine ana mafundisho na mwingine ana kweli mpya kutoka kwa Mungu. Mmoja anasema kwa lugha nyingine na mwingine anafasiri lugha hiyo. Cho chote mnachofanya lazima kiwe na lengo la kumfanya kila mmoja wenu akue katika imani. 27 Mnapokusanyika, ikiwa kuna yeyote atasema na kanisa katika lugha, iwe watu wawili tu au isiwe zaidi ya watu watatu. Na wanapaswa wanene kwa zamu, mmoja baada ya mwingine. Na mwingine afasiri kile wanachosema. 28 Lakini ikiwa hakuna mfasiri, basi mtu yeyote anayesema kwa lugha nyingine anapaswa kunyamaza kimya. Wanapaswa kuzungumza katika nafsi zao wenyewe ama na Mungu.

29 Na manabii wawili au watatu tu ndiyo wanapaswa kuzungumza. Wengine watathmini kile wanachosema. 30 Na ujumbe kutoka kwa Mungu ukimjia mtu aliyekaa, mzungumzaji wa kwanza anapaswa kunyamaza. 31 Nyote mnaweza kutabiri mmoja baada ya mwingine. Kwa njia hii kila mmoja anaweza kufundishwa na kutiwa moyo. 32 Roho za manabii ziko chini ya udhibiti wa manabii[a] wenyewe. 33 Mungu si Mungu wa machafuko lakini ni Mungu wa amani. Hii ni kanuni kwa ajili ya mikutano yote ya watu wa Mungu.

Read full chapter

Footnotes

  1. 14:32 Roho za manabii … udhibiti wa manabii Yaani, manabii wanaweza wakajizuia na kusubiri zamu yao kwa utaratibu mzuri.