Wataalamu Wa Nyota Wafika Kumwona Mtoto Yesu

Basi Yesu alipozaliwa katika mji wa Betlehemu huko Yudea, wakati wa utawala wa mfalme Herode, wataalamu wa mambo ya nyota kutoka Mashariki walifika Yerusalemu wakawa wakiuliza, kutoka kwao kuhusu wakati kamili ambao ile nyota ilionekana.

Mfalme Herode alipopata habari hizi alifadhaika sana na watu wote wa Yerusalemu wakawa na hali ya wasiwasi. Herode akaitisha mkutano wa makuhani wakuu na waandishi, akawataka wamweleze mahali ambapo Kristo angezaliwa.

Wakamjibu, “Atazaliwa Betlehemu ya Yudea, kwa maana nabii aliandika hivi kuhusu jambo hili: ‘Nawe Betlehemu, katika nchi ya Yuda, wewe si wa mwisho miongoni mwa watawala wa Yuda; kwa maana atatoka mtawala kwako atakayetawala watu wangu Israeli.’ ”

Ndipo Herode akawaita wale wataaamu wa nyota kwa siri aka pata uhakikisho Halafu akawatuma Bethlehemu akiwaagiza, “Nendeni mkamtafute huyo mtoto kwa bidii, na mkishampata, mnile tee habari ili na mimi niende kumsujudia.”

Baada ya kumsikiliza mfalme, wale wataalamu wa nyota wakaendelea na safari, na mbele yao wakaiona ile nyota waliyoiona mashariki ikiwatangulia, nao wakaifuata mpaka iliposimama juu ya mahali pale alipokuwa mtoto. 10 Walipoiona ile nyota walijawa na furaha isiyoelezeka.

11 Walipoingia ndani ya ile nyumba walimwona mtoto na mama yake Mariamu, wakainama chini kwa heshima kubwa wakamwabudu. Kisha wakafungua mikoba yao, wakampa zawadi: dhahabu, uvumba na manemane. 12 Na baada ya kuonywa katika ndoto wasirudi kwa Her ode , wakarudi makwao kwa kupitia njia nyingine.

Yosefu, Maria Na Mtoto Yesu Wakimbilia Misri

13 Walipokwisha kuondoka, malaika wa Bwana alimtokea Yosefu katika ndoto akamwambia, “Amka, umchukue mtoto na mama yake mkimbilie Misri na mkae huko mpaka hapo nitakapowaambia; kwa maana mfalme Herode ataanza msako wa kumtafuta huyu mtoto ili amwue.” 14 Kwa hiyo akaamka, akamchukua mtoto na mama yake usiku, wakaelekea Misri 15 na wakakaa huko mpaka Herode alipo fariki. Na hivyo likatimia neno alilosema Bwana hupitia nabii: ‘Nilimwita mwanangu kutoka Misri.’

16 Herode alipogundua kwamba wale wataalamu wa nyota wame mdanganya, alikasirika sana, akawatuma watu kuwaua watoto wote wa kiume wenye umri wa miaka miwili kwenda chini katika mji wa Betlehemu na sehemu zote za jirani, kufuatana na ule muda ambao wale wataalamu walikuwa wamemhakikishia. 17 Ndipo maneno yaliy osemwa hupitia nabii Yeremia yakatimia kama alivyosema:

18 “Sauti ilisikika huko Rama, kilio cha uchungu na maom bolezo; Raheli akiwalilia wanae; hakukubali kufarijiwa kwa sababu walikuwa wamekufa.”

19 Lakini Herode alipofariki, malaika wa Bwana alimtokea Yosefu katika ndoto huko Misri, 20 akamwambia, “Amka mchukue mtoto na mama yake, mrudi katika nchi ya Israeli kwa sababu wale waliotaka kumwua mtoto wamefariki.”

21 Basi Yosefu akaamka, akamchukua mtoto na mama yake wakar udi nchi ya Israeli. 22 Lakini alipopata habari kwamba Arkelao alikuwa akimiliki huko Yudea mahali pa baba yake Herode, aliogopa kwenda huko; na baada ya kuonywa tena katika ndoto, aliondoka akaenda wilaya ya Galilaya. 23 Akaenda kuishi katika mji ulioitwa Nazareti, na hivyo yakatimia yale yaliyosemwa kupitia manabii kwamba, “Ataitwa Mnazareti.”