Yesu Awatuma Wanafunzi Kumi Na wawili

Yesu akawaita pamoja wanafunzi wake kumi na wawili na kuwapa mamlaka na uwezo wa kufukuza pepo wote na kuponya magonjwa yote. Kisha akawatuma waende wakautangaze Ufalme wa Mungu na kuponya wagonjwa.

Akawaagiza akisema, “Msichukue cho chote safarini, wala fimbo, wala mkoba, wala chakula, wala fedha; na msichukue nguo za kubadili. Mkikaribishwa katika nyumba yo yote muwe wageni wa nyumba hiyo hadi mtakapoondoka katika kijiji hicho. Po pote ambapo hamtakaribishwa, mnapoondoka kung’uteni mavumbi miguuni mwenu kama ishara ya hukumu ya Mungu juu yao.”

Wale wanafunzi wakaondoka wakaenda kutoka kijiji hadi kijiji wakihubiri Habari Njema na kuponya wagonjwa. Habari zil imfikia Herode mtawala wa Galilaya kuhusu miujiza iliyokuwa iki fanyika, naye akafadhaika kwa kuwa baadhi ya watu walikuwa wakisema, “Yohana Mbatizaji amefufuka!” Wengine wakasema, “Ni Eliya ametutokea” na wengine kwamba, “Mmoja wa manabii wa kale amefufuka.” Herode akasema, “Yohana nilimkata kichwa, ni nani huyu anayefanya maajabu haya ninayoambiwa?” Akajaribu sana amwone Yesu.

Yesu Awalisha Watu Elfu Tano

10 Wanafunzi waliporudi walimweleza Yesu yote waliyofanya. Akawachukua wakaenda peke yao mpaka mji mmoja uitwao Bethsaida. 11 Lakini watu wengi wakafahamu alipokwenda, wakamfuata. Akawa karibisha, akawafundisha tena kuhusu Ufalme wa mbinguni na akapo nya wangonjwa. 12 Ilipokaribia jioni, wale wanafunzi kumi na wawili wakamwambia Yesu, “Waruhusu watu hawa waondoke ili waweze kujitafutia chakula na mahali pa kulala katika vijiji na mashamba ya jirani kwa maana hapa tuko nyikani.” 13 Akawajibu, “Wapeni chakula.” Wakasema, “Tunayo mikate mitano tu na samaki wawili. Unataka tukanunue chakula cha kuwatosha watu wote hawa?” 14 Kwa kuwa walikuwapo wanaume wapatao elfu tano! Lakini Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Waketisheni katika makundi ya watu hamsini-hamsini.” 15 Wakawaketisha wote. 16 Yesu akaichukua mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama mbinguni, akavi bariki na kuvimega. Kisha akawapa wanafunzi wake wawagawie wale watu. 17 Kila mtu akala na kutosheka na vilipokusanywa vipande vilivyobaki, vilijaa vikapu kumi na viwili.

Petro Amkiri Bwana Yesu Kuwa Ndiye Kristo

18 Siku moja Yesu alipokuwa akisali faraghani akiwa na wana funzi wake aliwauliza, “Watu husema mimi ni nani?” 19 Wakam wambia, “Watu husema wewe ni Yohana Mbatizaji, wengine husema ni Eliya na wengine husema wewe ni nabii wa kale aliyefufuka kutoka kwa wafu.”

20 Kisha akawauliza, “Ninyi je, mnasema mimi ni nani?” Petro akajibu, “Wewe ndiye Kristo wa Mungu.” 21 Yesu akawaka taza wasimwambie mtu jambo hilo 22 akisema, “Imenipasa mimi Mwana wa Adamu kupata mateso mengi na kukataliwa na wazee, maku hani wakuu na walimu wa sheria. Nitauawa na siku ya tatu nitafuf uliwa.” 23 Kisha akawaambia wote, “Ye yote anayetaka kunifuata ni lazima ajikane nafsi yake, achukue msalaba wake kila siku, anifuate. 24 Kwa maana ye yote atakayeshughulikia zaidi usalama wa nafsi yake ataipoteza. Lakini ye yote atakayeipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataisalimisha. 25 Je, kuna faida gani kwa mtu kuupata ulimwengu mzima ambapo kwa kufanya hivyo ataipoteza nafsi yake? 26 Mtu ye yote atakayenionea aibu mimi na maneno yangu, na mimi Mwana wa Adamu nitamwonea aibu mtu huyo nitakapo kuja katika utukufu wangu na wa Baba na wa malaika watakatifu. 27 Ninawaambia kweli, baadhi ya watu waliosimama hapa hawatakufa mpaka watakapouona Ufalme wa Mungu.”

Bwana Yesu Abadilika Sura

28 Yapata siku nane baada ya kusema hayo, Yesu alikwenda kusali mlimani pamoja na Petro, Yakobo na Yohana. 29 Alipokuwa akiomba, sura yake ili badilika, mavazi yake yakawa meupe, yakimetameta na kung’aa. 30 Ghafla wakawepo watu wawili wakaanza kuzungumza naye. Walikuwa ni Musa na Eliya! 31 Nao walionekana katika utukufu wakizungumza na Yesu kuhusu kifo chake ambacho kingetokea Yerusalemu.

32 Petro na wenzake ambao walikuwa wamelala usingizi mzito waliamka wakaona utukufu wa Yesu na wale watu wawili waliokuwa wamesimama pamoja naye. 33 Musa na Eliya walipoanza kuondoka, Petro akamwambia Yesu, “Bwana ni vizuri mno kwamba tuko hapa! Tutajenga vibanda vitatu - kimoja chako, kingine cha Musa na kin gine cha Eliya.” Lakini Petro hakujua anasema nini. 34 Petro alipokuwa bado anazungumza, pakatokea wingu kubwa na kivuli chake kikawafunika, na wale wanafunzi wakashikwa na hofu lile wingu lilipowafikia. 35 Sauti ikatoka kwenye wingu ikisema, “Huyu ni Mwanangu niliyemchagua, msikilizeni yeye.” 36 Baada ya sauti hiyo kusema, alionekana Yesu peke yake. Wale wanafunzi wakakaa kimya na kwa wakati huo hawakumwambia mtu ye yote yale waliyoy aona.

37 Kesho yake aliposhuka kutoka mlimani alikutana na umati mkubwa wa watu. 38 Ghafla, mtu mmoja kati yao akapiga kelele akasema, “Mwalimu, tafadhali nakuomba umwangalie mtoto wangu, ni mwanangu wa pekee. 39 Mara kwa mara pepo humshika na kumfanya apige kelele kisha humwangusha na kumtia kifafa akatokwa na povu mdomoni. Anamtesa sana na hamwachii ila kwa shida. 40 Nimewaomba wanafunzi wako wamwondoe huyo pepo lakini wameshindwa.” 41 Yesu akajibu, “Enyi watu mliopotoka, msio na imani, nitakaa nanyi na kuwavumilia mpaka lini? Mlete mwanao hapa.”

42 Yule mtoto alipokuwa akija, yule pepo akamwangusha, akam tia kifafa. Lakini Yesu akamwamuru yule pepo amtoke. Akamponya yule mtoto akamkabidhi kwa baba yake. 43 Watu wote walishangaa walipoona huo uweza mkuu wa Mungu. Wakati watu walipokuwa wanas taajabia hayo yote aliyokuwa akiyafanya Yesu, yeye aliwaambia wanafunzi wake: 44 “ Sikilizeni kwa makini haya nitakayowaambia sasa: mimi Mwana wa Adamu nitasalitiwa na kuwekwa mikononi mwa wanadamu.” 45 Lakini wanafunzi wake hawakuyaelewa maneno hayo. Maana ya maneno hayo ilikuwa imefichwa ili wasiweze kuelewa, nao waliogopa kumwuliza.

Yesu Afundisha Kuhusu Ukubwa

46 Wanafunzi wakaanza kubishana wao kwa wao kuhusu nani kati yao alikuwa mkuu zaidi. 47 Lakini Yesu aliyatambua mawazo yao, akamsimamisha mtoto mdogo karibu naye 48 kisha akawaambia, “Ye yote atakayemkaribisha mtoto huyu mdogo kwa jina langu atakuwa amenikaribisha; na ye yote atakayenikaribisha mimi atakuwa amem karibisha yeye aliyenituma; kwa maana yeye aliye mdogo kati yenu, ndiye aliye mkubwa kuliko wote.” 49 Yohana akasema, “Bwana, tumemwona mtu akifukuza pepo kwa jina lako tukamzuia kwa maana yeye si mmoja wetu.” 50 Yesu akasema, “Msimzuie kwa sababu ye yote ambaye hapingani nanyi, yuko upande wenu.”

Yesu Akataliwa Samaria

51 Siku zake za kurudi mbinguni zilipokaribia, Yesu aliamua kwamba lazima aende Yerusalemu na akaanza safari kuelekea huko. 52 Akatuma watu wamtangulie, nao wakaenda katika kijiji kimoja cha Samaria kumwandalia kila kitu. 53 Lakini watu wa kijiji hicho walikataa kumpokea kwa sababu ilikuwa dhahiri kwamba ali kuwa anakwenda Yerusalemu. 54 Basi wanafunzi wake Yakobo na Yohana walipoona hayo, wakasema: “Bwana, unataka tuamuru moto kutoka mbinguni uwaangamize?” 55 Yesu akageuka, akawakemea. 56 Wakaenda kijiji kingine.

Gharama Ya Kumfuata Yesu

57 Walipokuwa wakienda, mtu mmoja akamwambia Yesu, “Nitakufu ata po pote utakapokwenda.” 58 Yesu akamwambia, “Mbweha wanaishi kwenye mapango yao na ndege kwenye viota vyao lakini mimi Mwana wa Adamu sina mahali pa kulala na kupumzika.”

59 Yesu alimwambia mtu mwingine, “Nifuate.” Mtu huyo akamjibu, “Bwana, niache kwanza nikamzike baba yangu.” 60 Yesu akamwam bia, “Waache wafu wawazike wafu wao. Bali wewe nenda ukautan gaze Ufalme wa Mungu.” 61 Mtu mwingine akamwambia, “Bwana nitakufuata lakini naomba kwanza nikaage jamaa yangu.” 62 Yesu akamwambia, “Mtu ye yote ashikaye jembe kuanza kulima kisha akawa anageuka kutazama nyuma, hafai kwa Ufalme wa Mungu.” Yesu Awatuma Wafuasi Sabini na Wawili