Ndugu Wa Yesu

46 Wakati alipokuwa akizungumza na watu, mama yake na ndugu zake walisimama nje wakataka kuongea naye. [ 47 Mtu mmoja akam wambia, “Mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanataka kuon gea na wewe.”] 48 Lakini akamjibu yule mtu aliyemwambia, “Mama yangu ni nani, na ndugu zangu ni nani?” 49 Akinyoosha kidole chake kwa wanafunzi wake, alisema , “Hawa hapa ndio mama yangu na ndugu zangu! 50 Kwa maana ye yote anayefanya mapenzi ya Baba yangu wa mbinguni, ndiye kaka, dada na mama yangu.”

Read full chapter