23 Paulo akawakazia macho wajumbe wa baraza, akasema, “Ndugu zangu, mimi nimeishi nikiwa na dhamiri safi kabisa siku zote mbele za Mungu, mpaka leo.” Kuhani mkuu Anania akaamuru wale waliokuwa karibu na Paulo wampige kofi mdomoni. Ndipo Paulo akasema, “Mungu atakupiga, wewe ukuta uliopakwa chokaa! Unawe zaje kusikiliza kesi hii kwa mujibu wa sheria, na hapo hapo, kinyume cha sheria, unaamuru nipigwe?” Wale watu waliokuwa wamesimama karibu wakamwambia Paulo, “Mbona unamtukana kuhani mkuu wa Mungu?” Paulo akajibu, “Ndugu zangu, sikujua kwamba yeye ni kuhani mkuu. Kwa maana Maandiko yanasema, ‘Usimseme vibaya kiongozi wa watu wako.’ ” Paulo alipotambua ya kuwa baadhi ya wajumbe wa baraza walikuwa Masadukayo na wengine ni Mafarisayo alisema nao kwa sauti kubwa, “Ndugu zangu! Mimi ni Mfarisayo, mtoto wa Mafarisayo; na hapa nimeshitakiwa kuhusu tumaini juu ya ufufuo wa wafu.” Aliposema haya, Mafarisayo na Masadukayo wakafarakana na baraza zima likagawanyika. Kwa maana Masadukayo wanaamini kwamba hakuna ufufuo, wala hakuna malaika au roho; lakini Mafarisayo wanaamini haya yote. Kelele zikazidi sana; na baadhi ya waandishi wa sheria wa upande wa Mafarisayo, wakasimama wakiwapinga wengine wakasema, “Hatuoni kosa lo lote alilofanya mtu huyu! Huenda ikawa malaika au roho amezungumza naye kweli!” 10 Mabishano yalipozidi kuwa makali, yule jemadari aliogopa kuwa wangeweza kumrarua Paulo vipande vipande. Kwa hiyo akaamuru askari wakamtoe Paulo alipokuwa, arudishwe kwenye ngome ya jeshi. 11 Usiku uliofuata, Bwana akamtokea Paulo akasimama karibu naye akamwambia, “Jipe moyo! Kama ulivyonishuhudia hapa Yerusalemu, itakubidi unishuhudie na huko Rumi pia.”

Njama Za Wayahudi Kumwua Paulo

12 Kulipopambazuka Wayahudi wakala njama ya kumwua Paulo. Wakaweka nadhiri kwamba hawatakula wala kunywa mpaka wamemwua Paulo. 13 Waliofanya mpango huu walikuwa zaidi ya watu arobaini. 14 Wakaenda kwa kuhani mkuu na wazee wakasema, “Tumeweka nad hiri ya pamoja kwamba hatutakula wala kunywa mpaka tumwue Paulo. 15 Kwa hiyo ninyi pamoja na baraza, pelekeni ombi kwa jemadari ili Paulo aletwe barazani, mtoe udhuru kwamba mnataka kuchunguza kesi yake kwa usahihi zaidi. Sisi tutakuwa tayari kumwua hata kabla hajakaribia kufika hapa.” 16 Basi kumbe binamu yake Paulo alisikia kuhusu mpango huu. Akaenda katika ngome ya jeshi akamweleza Paulo mambo haya. 17 Paulo akamwita mmoja wa wale maaskari akamwambia, “Mchukue kijana huyu kwa jemadari, ana neno la kumwambia.” 18 Yule askari akamchukua yule kijana mpaka kwa jemadari akamwambia, “Yule mfungwa Paulo aliniita akaniambia nimlete huyu kijana kwako, kwa sababu ana neno la kukuambia.” 19 Yule jemadari akamchukua yule kijana kando akamwuliza, “Unataka kuniambia nini?” 20 Naye akasema, “Wayahudi wameku baliana wakuombe kesho umpeleke Paulo kwenye Baraza lao kwa kisingizio kwamba wanataka kuchunguza kesi yake kwa uangalifu zaidi. 21 Lakini usikubali ombi lao kwa maana zaidi ya watu aro baini wamekula njama kwamba hawatakula wala kunywa mpaka wamwue Paulo nao wamejiweka tayari kumvizia ukishakubali ombi lao.” 22 Yule jemadari akamruhusu yule kijana aende, akamwonya akisema, “Usimwambie mtu ye yote kwamba umenieleza habari hizi.”

Paulo Apelekwa Kaisaria Kwa Gavana Feliksi

23 Yule jemadari akawaita maaskari wawili akawaambia, “Tay arisheni askari mia mbili watakaokwenda Kaisaria pamoja na askari wa farasi sabini, na askari wa mikuki mia mbili; nanyi muwe tay ari kuondoka leo saa tatu za usiku. 24 Pia tayarisheni na farasi watakaotumiwa na Paulo, mumpeleke salama mpaka kwa gavana Feliksi.” 25 Kisha akaandika barua kwa Feliksi kama ifuatavyo: 26 “Mimi Klaudio Lisia, nakuandikia wewe gavana mtukufu Feliksi. Salamu. 27 Mtu huyu alikamatwa na Wayahudi wakawa kar ibu kumwua, ndipo mimi nilipofika na askari wangu nikamwokoa kwa kuwa nilipata habari kwamba yeye ni raia wa Kirumi. 28 Nami nikampeleka mbele ya baraza lao ili nipate kujua kosa alilofanya. 29 Ndipo nikagundua ya kuwa alikuwa anashtakiwa kuhusu sheria yao, lakini hakuwa na kosa la kustahili kifo au kifungo. 30 Lakini nilipata habari kwamba kuna mpango wa kumwua nikaamua nimpeleke kwako mara moja, nikawaamuru washitaki wake walete mashtaka yao kwako.” 31 Basi wale askari wakamchukua Paulo usiku wakampeleka mpaka Antipatri kama walivyoamriwa. 32 Kesho yake wakarudi kituoni wakawaacha wale askari wa mikuki waendelee na safari pamoja na Paulo. 33 Walipofika Kaisaria walimpa Liwali ile barua na pia wakamkabidhi Paulo kwake. 34 Alipokwisha soma ile barua, alimwuliza Paulo ametoka jimbo gani. Alipofahamishwa kuwa anatoka Kilikia 35 alisema, “Nitasikiliza kesi yako mara tu washtaki wako watakapofika.” Akaamuru Paulo awekwe chini ya ulinzi katika ikulu ya Herode.

Mashtaka Ya Wayahudi Juu Ya Paulo

24 Baada ya siku tano, Kuhani Mkuu Anania akafika pamoja na baadhi ya wazee na wakili mmoja aitwaye Tertulo. Wakatoa mashtaka yao juu ya Paulo mbele ya Gavana. Na Paulo alipoitwa, Tertulo akaanza kutoa mashtaka akasema, “Mtukufu Feliksi, kutokana na uongozi wako wa busara tumekuwa na amani ya kudumu na tunatambua ya kuwa mabadiliko mengi muhimu yaliyotokea katika taifa letu yameletwa na uwezo wako wa kuona mbele. Wakati wote na kila mahali tunapokea mambo haya yote kwa shukrani za dhati. Lakini nisije nikakuchosha, nakuomba kwa hisani yako utusikilize kwa muda mfupi. Tumemwona mtu huyu kuwa ni mfanya fujo ambaye ana chochea maasi kati ya Wayahudi dunia nzima. Yeye ni kiongozi wa dhehebu la Wanazareti. Tena alijaribu kulichafua Hekalu letu lakini tulimkamata [tukataka kumhukumu kwa mujibu wa sheria zetu, lakini jemadari Lisia alikuja akamchukua kutoka kwetu kwa kutu mia nguvu akaamuru wanaomshtaki walete mashtaka yao mbele yako]. Wewe mwenyewe ukimwuliza maswali utathibitisha ukweli wa mashtaka yote tunayoleta mbele yako kumhusu yeye.” Wayahudi wakamwunga mkono wakithibitisha kwamba mashtaka yote yalikuwa ya kweli.

Paulo Ajitetea Mbele Ya Feliksi

10 Gavana Feliksi alipomruhusu Paulo ajitetee, yeye alisema, “Najua kwamba wewe umekuwa hakimu katika taifa hili kwa miaka mingi kwa hiyo natoa utetezi wangu bila wasi wasi. 11 Unaweza kuhakikisha kwa urahisi kuwa hazijapita zaidi ya siku kumi na mbili tangu nilipokwenda Yerusalemu kuabudu. 12 Hawa wanaonish taki hawakunikuta nikibishana na mtu ye yote au nikianzisha fujo katika Hekalu au katika sinagogi au mahali pengine po pote mjini. 13 Wala hawawezi kabisa kuthibitisha mambo haya wanayon ishtaki. 14 Lakini nakiri mbele yako kuwa mimi namwabudu Mungu wa baba zetu kwa kufuata ile ‘Njia’ ambayo wao wanaiita dhehebu. Ninaamini kila kitu kilichoandikwa katika Sheria ya Musa na Mana bii 15 na ninalo tumaini kwa Mungu ambalo hata na wao wanaliku bali, kwamba kutakuwa na ufufuo wa wote, walio na haki na wasio na haki. 16 Kwa hiyo ninafanya kila jitihada kuishi nikiwa na dhamiri safi mbele za Mungu na mbele za wanadamu. 17 Basi, baada ya kuwa nje ya Yerusalemu kwa miaka kadhaa nilikuja mjini kuwale tea watu wa taifa langu sadaka kwa ajili ya maskini na kutoa dha bihu. 18 Nilikuwa nimeshatakaswa waliponikuta Hekaluni nikifanya mambo haya, na hapakuwa na umati wa watu wala fujo yo yote. 19 Lakini kulikuwa na Wayahudi kutoka Asia, nadhani nao walista hili wawepo hapa mbele yako ili watoe mashtaka yao kama wanalo lo lote la kunishtaki. 20 La sivyo, watu hawa waseme ni kosa gani walilogundua nimefanya niliposhtakiwa mbele ya Baraza, 21 isipo kuwa lile jambo nililotangaza wazi wazi nilipojitetea mbele yao, kwamba, ‘Mimi nimeshtakiwa mbele yenu leo kuhusu ufufuo wa wafu.’

22 Ndipo Feliksi ambaye alikuwa anafahamu vizuri habari za Njia, akaamua kuahirishwa kwa kesi, akasema, “Mara jemadari Lisia atakapofika nitatoa hukumu yangu juu ya kesi hii.” 23 Akaamuru askari amweke Paulo kizuizini chini ya ulinzi lakini awe na uhuru kiasi, na marafiki zake wasizuiwe kumhudumia. 24 Baada ya siku chache Feliksi akaja na mkewe Drusila ambaye alikuwa Myahudi. Akatuma Paulo aitwe, wakamsikiliza akizungumza juu ya kumwamini Kristo Yesu. 25 Na Paulo alipokuwa akiwaeleza juu ya kuwa na kiasi na juu ya hukumu ya mwisho, Feliksi aliin giwa na hofu akasema, “Tafadhali sasa nenda, nitakuita tena nikipata nafasi.” 26 Wakati huo huo Feliksi alitazamia kwamba Paulo angempatia hongo, kwa hiyo akawa anamwita mara kwa mara kuzungumza naye. 27 Lakini baada ya miaka miwili kupita, Porkio Festo akachukua nafasi ya Feliksi kama Gavana; na kwa sababu Feliksi alitaka kujipendekeza kwa Wayahudi, akamwacha Paulo gere zani.

Paulo Anajitetea Mbele Ya Festo

25 Siku tatu baada ya Festo kuwasili Kaisaria kuanza kazi, alisafiri kwenda Yerusalemu. Makuhani wakuu na viongozi wa Way ahudi wakamletea mashtaka yao juu ya Paulo, na wakamwomba Festo awafanyie upendeleo, amrudishe Paulo Yerusalemu; wakiwa na mpango wa kumwua Paulo njiani. Festo akawajibu, “Paulo yuko kizuizini huko Kaisaria, na mimi natarajia kwenda huko hivi kari buni. Kwa hiyo tumeni viongozi wenu tuongozane pamoja na kama huyu mtu amefanya kosa lo lote, wao walete mashtaka yao.” Festo alikaa nao kwa muda wa siku nane au kumi kisha akaondoka kwenda Kaisaria. Kesho yake akakaa katika baraza la mahakama, akaamuru Paulo aletwe. Paulo alipoletwa, wale Wayahudi wal iotoka Yerusalemu walisimama wakaanza kutoa mashtaka mengi mazito ambayo hawakuweza kuyathibitisha. Lakini Paulo alijitetea, akasema, “Sikufanya jambo lo lote kinyume cha sheria za Wayahudi au Hekalu au kinyume cha Kaisari. ” Festo akitaka kuwapendeza Wayahudi, alimwuliza Paulo, “Je, ungependa kwenda Yerusalemu ukahojiwe huko kuhusu mashtaka haya mbele yangu?” 10 Paulo akasema, “Mimi nasimama mbele ya baraza la mahakama ya Kaisari. Baraza hili ndilo lina wajibu wa kusikiliza kesi hii. Kama unav yojua sijawatendea Wayahudi uovu wo wote. 11 Kama mimi ni mhal ifu na nimetenda kosa linalostahili hukumu ya kifo, sijitetei ili nisiuawe; lakini kama mashtaka yao juu yangu hayana msingi, hakuna mtu atakayeweza kunitia mikononi mwao waniue. Ninakata rufaa, kesi yangu isikilizwe na Kaisari.” 12 Festo akajadiliana na baraza kisha akasema, “Umeomba rufaa usikilizwe na Kaisari; basi utakwenda kwa Kaisari.”

Paulo Afikishwa Mbele Ya Mfalme Agripa

13 Baada ya siku chache mfalme Agripa na Benike wakafika Kaisaria kumkaribisha Festo. 14 Kwa kuwa walikuwa wanakaa Kais aria kwa muda mrefu, Festo alipata nafasi ya kujadiliana na mfalme kesi ya Paulo; akamwambia, “Kuna mtu mmoja hapa ambaye Feliksi alimwacha gerezani kama mfungwa. 15 Nilipokwenda Yerus alemu, makuhani wakuu na wazee wa Wayahudi walileta mashtaka yao juu yake wakitaka ahukumiwe. 16 Lakini mimi niliwaambia kwamba sheria za Kirumi haziruhusu kumhukumu mtu aliyeshitakiwa kabla hajapata nafasi ya kukutana uso kwa uso na washitaki wake naye apewe nafasi ya kujitetea. 17 Walipofika hapa pamoja nami, siku kawia, bali nilikaa pamoja na baraza la mahakama nikaamuru mshta kiwa aletwe. 18 Lakini washtaki wake waliposimama, hawakutaja aina yo yote ya uhalifu kama nilivyotarajia, 19 bali walikuwa na mashtaka kuhusu mabishano fulani juu ya dini yao na juu ya mtu aitwaye Yesu ambaye alikufa, lakini Paulo alidai kwamba anaishi. 20 Sikujua jinsi ya kuchunguza mambo haya kwa hiyo nikamwuliza Paulo kama angelipenda kwenda Yerusalemu mashtaka haya yakasiki lizwe huko. 21 Lakini Paulo alipokata rufaa, akaomba akae kizuizini mpaka Kaisari atakapotoa uamuzi wake, niliamuru awekwe rumande mpaka nitakapompeleka kwa Kaisari.” 22 Agripa akasema, “Ningependa nimsikilize mtu huyu mwenyewe.”

Paulo Ajitetea Mbele Ya Agripa

23 Kesho yake Agripa na Bernike walifika kwa fahari kubwa wakaingia katika ukumbi wa mkutano pamoja na mahakimu wa kijeshi na watu mashuhuri wa mji. Ndipo kwa amri ya Festo Paulo akaletwa.

24 Festo akasema, “Mfalme Agripa, na ninyi nyote mlio hapa pamoja nasi leo, mnamwona hapa huyu mtu ambaye Wayahudi wote wa Yerusalemu na wa hapa Kaisaria wamenisihi, wakipiga makelele kwamba hastahili tena kuishi. 25 Lakini mimi sikuona kosa lo lote alilotenda linalostahili hukumu ya kifo; na kwa kuwa yeye mwenyewe amekata rufaa kesi yake isikilizwe na Kaisari, niliamua nimpeleke kwake. 26 Lakini sina mapendekezo kamili ya kumwandi kia mtukufu Kaisari juu ya huyu mshtakiwa. Kwa hiyo nimemleta hapa mbele yenu na hasa mbele yako wewe mfalme Agripa ili baada ya kumhoji mshtakiwa nipate jambo la kuandika. 27 Kwa maana ita kuwa si jambo la busara kumpeleka mfungwa kwa Kaisari bila kuon yesha wazi wazi mashtaka yanayomkabili.”

26 Mfalme Agripa akamwambia Paulo, “Unayo ruhusa kujite tea.” Paulo akanyoosha mkono wake, akaanza kujitetea akasema,

“Mfalme Agripa, najiona kuwa mwenye bahati kwamba ninatoa utetezi wangu mbele yako kuhusu mashtaka yote ya Wayahudi. Kwa sababu nafahamu ya kuwa wewe unajua kwa undani mila na maswala yote ya mabishano kati ya Wayahudi. Kwa hiyo nakusihi unisikilize kwa uvumilivu.

“Wayahudi wote wanajua jinsi nilivyoishi kutoka utotoni, kwa maana tangu mwanzo wa maisha yangu niliishi katika nchi yangu na pia Yerusalemu. Pia wamefahamu wakati wote, na wanaweza kushuhudia, ya kuwa nililelewa na kuishi kama Mfarisayo nikifuata masharti halisi ya madhehebu ya dini yetu. Na hata sasa nasi mama hapa nikiwa nashtakiwa kwa sababu nashikilia tumaini ambalo Mungu aliwaahidi baba zetu. Ahadi hii ndio inawafanya makabila kumi na mawili ya Israeli wamwabudu Mungu kwa bidii usiku na mchana wakitarajia kuipokea. Mtukufu Mfalme, ni kwa ajili ya tumaini hili Wayahudi wamenishtaki! Sijui ni kwa nini watu wanadhani ni jambo la ajabu lisilowezekana, kwamba Mungu anawafu fua wafu.

Mimi mwenyewe nilikuwa nimeamini kabisa kwamba sina budi kufanya kila niwezalo kupinga jina la Yesu wa Nazareti. 10 Nami ndivyo nilivyofanya kule Yerusalemu. Nilipewa mamlaka na makuhani wakuu, nikawatia kifungoni watakatifu wengi na walipokuwa wakihu kumiwa kuuawa mimi nilipiga kura kuunga mkono hukumu hiyo. 11 Pia niliwaadhibu mara nyingi katika masinagogi nikajaribu kuwalazimisha wakane imani yao. Nilikuwa nimejawa na ghadhabu juu yao nikawafuatilia na kuwatesa hata katika miji ya mbali.

12 “Nilikuwa katika mojawapo ya safari hizi nikielekea Dameski, nikiwa na kibali na amri kutoka kwa makuhani wakuu. 13 Mtukufu Mfalme, nilipokuwa njiani, mnamo saa sita mchana, niliona mwanga mkali kuliko wa jua kutoka mbinguni, ukaniangazia mimi na wale niliokuwa nao, pande zote. 14 Na wote tulipokuwa tumeanguka chini nilisikia sauti ikisema nami kwa lugha ya Kie brania, ‘Sauli, Sauli! Mbona unanitesa? Unajiumiza mwenyewe.’ 15 Nikauliza, ‘Ni nani wewe Bwana?’ Naye akasema, ‘Mimi ni Yesu unayenitesa. 16 Lakini sasa inuka usimame, kwa maana nimejidhi hirisha kwako ili nikuteue uwe mtumishi wangu, ukawaambie wengine mambo yote uliyoyaona kwangu leo, na yale nitakayokuonyesha baad aye. 17 Nitakuokoa kutoka kwa watu wako na watu wa mataifa. 18 Ninakutuma ukawafungue macho yao ili watoke kwenye giza waingie nuruni na watoke katika nguvu za shetani wamgeukie Mungu; ili wapokee msamaha wa dhambi na wapate nafasi pamoja na wote ambao wanatakaswa kwa kuniamini.’

19 Kwa hiyo mtukufu Agripa, sikuweza kuacha kutii haya maagizo ya maono kutoka mbinguni, 20 bali niliwahubiria kwanza watu wa Dameski kisha Yerusalemu na nchi yote ya Yudea na watu wa mataifa mengine pia. Niliwahimiza watubu dhambi zao wamgeukie Mungu na kuishi maisha yanayodhihirisha kwamba kweli wametubu. 21 Ni kwa sababu hii Wayahudi walinikamata nilipokuwa Hekaluni, wakataka kuniua. 22 Lakini mpaka wakati huu nimepata msaada uto kao kwa Mungu, na kwa hiyo nasimama hapa nikitoa ushuhuda wangu kwa watu wote, wakubwa kwa wadogo. Nami sisemi lo lote ila yale ambayo Musa na manabii walitabiri yangetokea: 23 kwamba Kristo atateswa naye kwa kuwa atakuwa wa kwanza kufufuka kutoka kwa wafu, atatangaza mwanga wa wokovu kwa Wayahudi na watu wa mataifa.”

24 Paulo alipofikia hapa katika utetezi wake Festo aliin gilia kati akasema kwa sauti kubwa, “Paulo, umeehuka! Kusoma sana kumekufanya uehuke !” 25 Lakini Paulo akajibu, “Mimi si mwehu, Mtukufu Festo, bali nasema yale yaliyo kweli na ya kuami nika. 26 Mfalme Agripa anajua habari za mambo haya, ndio sababu najieleza wazi wazi mbele yake. Kwa sababu ninahakika kuwa yeye aliyaona mambo haya kwa kuwa hayakufichwa pembeni. 27 Mfalme Agripa, Unawaamini manabii? Ninajua kwamba unaamini.” 28 Kisha Agripa akamjibu, “Unadhani kuwa kwa muda huu mfupi unaweza kuni fanya nikubali kuwa mkristo!” 29 Paulo akasema, “Singejali kama ni kwa muda mfupi au mrefu, lakini shauku yangu ni kwamba wewe na wote wanaonisikiliza leo muwe kama mimi nilivyo, isipo kuwa tu hii minyororo.’ ’ 30 Ndipo Mfalme akasimama na Gavana na Bernike na wengine wote waliokuwa wameketi nao wakasimama. 31 Na walipokuwa faraghani pamoja wakasema, “Mtu huyu hafanyi jambo lo lote linalostahili kifo au kifungo.” 32 Agripa akamwambia Festo, “Mtu huyu angeweza kuachiliwa huru kama hakuwa amekata rufaa kesi yake isikilizwe na Kaisari.”